Bongo Movies wanaboa sana!

Bongo Movies wanaboa sana!

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
27,066
Reaction score
27,441
Leo nilikuwa naangalia filamu ya Bongo Movie, kupitia king'amuzi cha Azam Tv, nikakutana na maneno ya kiingereza cha ajabu kilichotumiwa katika tafsiri (subtitles), lengo likiwa kutoa tafsri kwa watazamaji wasiojua kiswahili.

Kuna 'subtitle' ilikuwa inasomeka 'I see tones of blood in your face...what is happen for you?'. Nilipata wakati mgumu kutatafuta tafsri ya hii sentensi. Lakini kwa kuwa mhusika aliyekuwa akiulizwa swali hilo alikuwa na matone ya damu usoni kwake nikakisia kwamba mtafsiri alikuwa na maana ya: 'Naona matone ya damu usoni kwako...nini kimekutokea?'

Subtitle nyingine ni ile iliyokuwa imasomeka: 'Keep quite' ikiwa na maana ya 'Nyamaza'.

Nashindwa kuelewa hawa watengeneza filamu huwatumia watu gani kutafsiri filamu zao. Watakuwa wanamchukua JB, King'wendu au Mrisho Mpoto na kuwapa kazi ya kutafsiri filamu wakati hawajui kiingereza.

Ikiwa wasanii wetu wataendelea kutengeneza filamu za ovyo kama hizi kamwe wasitegemee kazi zao kupata soko la kimataifa. Waendelee tu kuibiwa na wahindi.

:yield:
 
Kwanza hii Bongo movie naipa survival rate ya miaka 10....Baada ya hapo itakuwa imeshapoteza umaarufu au kufa kabisa....
 
Dawa ni kuchukua madada zao katika fani na kuwachapa nao.maana hawabadilik...i
 
Dawa ni kuchukua madada zao katika fani na kuwachapa nao.maana hawabadilik...i

na ndicho hasa wanachotaka--msichana akishaigiza filamu moja tu utamuona anaanza kujirahisisha kwa mapedeshee. wanaudhi sana.
 
Back
Top Bottom