EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,356
Alikua anaumwa na tumbo kisha akamuomba Shija amsindikize hospitali,
wakaongozana moja kwa moja mpaka hospitali ya Mwananyamala na
hatimae kutoa maelezo na baada ya muda madaktari wakahisi atakua na
tatizo ktka utumbo ambapo mmoja wao alisema itakua ni utumbo umekatika au
jeraha.
Hivyo wakabidi wamfanyie upasuaji lakini baada ya upasuaji walibaini hakuwa na
tatizo katika utumbo, wakafanya wanachojua na mwishowe wakamshona sehemu
waliyoifanyia upasuaji.
Hali hiyo ilimfanya john aendelee kuzidiwa nakumbidi apelekwe Muhimbili,
na huko ndiko walikobaini kuwa tatizo ni KONGOSHO.
Operesheni za aina hii nimeshazisikia sana. Kuna mwingine aliambiwa eti ana matatizo na mfereji wa kukojoa kwa hiyo the only solution ni kufanyiwa operesheni ili awekewe mrija wa kutolea mkojo.
Bahati nzuri huyo daktari aliyekuwa anataka kumfanyia huo upasuaki alidai rushwa na jamaa hakuwa na pesa so akawa anazunguka kukopa.
Akashauriwa na washikaji ni bora aitumie hiyo pesa kwenda kumwona specialist, alipomwona akapewa antibiotics, jamaa alipona na anapeta mpaka leo.