RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391
Sehemu ya kumi na sita
"Sijaelewa unazungumzia nini kijana?" Dr Luis alisema hofu dhahiri ikiwa katika sauti yake.
"Nimesema nataka ututengenezee kirusi cha DH+" Imma Ogbo alirudia tena.
"Unafaham nini kuhusu kirusi cha DH+?" Dr Luis aliuliza huku akiwa katika hali ya wasiwasi.
"Hapa kuna mgawanyo wa kazi. Wewe hauna jukumu la kuuliza maswali. Jukumu lako ni moja tu, kutekeleza kila nikwambiacho" Imma Ogbo alisema.
"Hawa watu wamejuaje kuhusu kirusi cha DH+. Dh+ ni kirusi kibaya sana. Endapo nikitengeneza kirusi cha DH+ na kuwakabidhi watu hawa ambao sijui wanataka kukifanyia nini itakuwa ni hatari sana. Katu siwezi kuwatengenezea kirusi cha DH+. Najua madhara yake ambayo hadi sasa yanamtesa Mheshimiwa rais" Dr Luis akawaza.
"Dr Luis umenielewa nikichokwambia?" Imma Ogbo aliuliza.
Dr Luis alikaa kimya.
"Dr Luis, napenda tuumalize mjadala huu kistaarabu. Sitaki tuumizane ili utekeleze nikwambiacho. Utatutengenezea kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.
Dr Luis alikaa kimya.
"Hii ni mara ya mwisho kukwambia kistaarabu. Naona unataka kuujua upande wangu wa pili. Mimi ni tafsiri sahihi ya neno ukatiri!!"
"Nitawatengenezea kirusi cha DH+, lakini kwa masharti mawili" Dr Luis alisema kwa uwoga.
"Haujaja kutupa masharti hapa!!" Imma Ogbo alifoka.
"Basi kama hutaki nikupe masharti, nisrme tu sitowatengenezea hiko kirusi. Nifanyeni mnavyoweza" Dr Luis alisema.
"Narudia kwa mara ya mwisho Dr Luis, sitaki nitumie nguvu ili kutekeleza hiki nikwambiacho!" Imma Ogbo alisema.
Dr Luis alikaa kimya.
"Bila hayo masharti yako, upo tayari ututengenezee kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.
"Siwezi kuwatengenezea" Dr Luis alijibu kwa ufupi. Huku macho yake yalimaanisha alichokuwa amekisema.
Mara, simu ya Imma Ogbo iliita. Alikuwa ni mzee Msangi.
"Eeeh nambie mzee..bado naendelea na mahojiano.." Imma Ogbo alisema simuni.
"Tumesikiliza majadiliano yako na Dr Luis. Naomba mpe nafasi akwambie hayo masharti" Mzee Msangi alisema.
"Ni nje ya utaratibu mzee. Hatuwezi kupewa masharti na mtu tuliyemteka" Imma Ogbo alisema.
"Mimi ni bosi wako hapa. Naomba fanya nilichokuagiza!" Mzee Msangi alifoka.
"Siwezi kufanya maagizo yako. Hujanileta wewe hapa! Mimi napewa oda na aliyenileta tu, ambaye ni..."
"Come on Imma Ogbo. Toka humo ndani!!" Mzee Msangi alifoka.
"Mzee unajua unachokifanya. Kwanza umekosea kufatilia majadiliano haya. Ndio maana kamera zote za huku zimezimwa. Bila shaka umeweka kamera zako za siri. Hilo ni kosa. Haya ni majadiliano ya siri. Kwahiyo ulikuwa unanichunguza? Umeniuzi sana. Na sasa unataka kuingilia kazi isiyokuhusu. Jua haya si majukumu yako. Na sipo tayari kuteleza usemayo" Imma Ogbo alisema.
Kwa hasira Mzee Msangi alikata simu.
"Twendeni huko shimoni!" Mzee Msangi aliwaambia wenzake. Kila mmoja akatoa bastola yake.
"Imma Ogbo hastahili kuifanya kazi hii" Mzee msangi alisema wakiwa katika korido kuelekea katika chumba cha mateso kilichokuwa chini kabisa ya jengo hilo.
Dakika saba ziliwafikisha shimoni. Cha kushangaza waliukuta mlango wazi. Na tangu kimejengwa chumba hiko hakikuwahi kuwa wazi. Kwa umakini mkubwa wakina mzee Msangi waliingia mle ndani.
Walikutana na jambo la kushangaza sana..
Hakuwepo Imma Ogbo wala Dr Luis...
Harakaharaka Dr Luis alitoa simu yake na kumpigia mkuu wa ulinzi wa lile jengo.
"Simon, kuna watu wawili wametoroka humu ndani. Hakikisha hatoki mtu ndani ya jengo hili. Fikisha taarifa kwa watu wako wote!" Mzee Msangi alifoka.
"Sawa mkuu" Simon alijibu.
Dakika hiyohiyo msako wa kuwasaka Imma Ogbo na Dr Luis ulianza mle ndani ya nyumba.
"Huyu kijana hajui kwa namna gani amefanya jambo la hatari sana. Hajui Dr Luis ni mtu wa muhimu kwetu kwa kiasi gani? Atajutia kwa hiki alichokifanya" Mzee Msangi aliwaza.
Mara simu yake iliita. Alikuwa Simon.
"Vipi Simon mmewapata?" Mzee Msangi aliuliza.
"Hatujafanikiwa mzee. Lakini nyuma ya nyumba tumekuta walinzi wetu watatu wameuwawa. Bila shaka hawa watu wameruka ukuta kwa nyuma. Msako inabidi utoke ndani ya jengo" Simon alisema.
"Umeruhusuje hilo Simon?" Mzee Msangi aliuliza.
"Jamaa walikata mawasiliano. Hata kamera zetu hazikuweza kuwanasa wakati wanatoroka. Wakati mafundi wakijaribu kurudisha nawasiliano yetu, kumbe hao watu ndio walikuwa wanatoroka" Simon alisema.
"Daah tumefanya kosa kubwa sana. Tutamwambia nini Roho?" Mzee Msangi aliwaza.
"Nitakuelekeza cha kufanya Simon. Ngoja nifikirie kidogo" Mzee Msangi alisema.
Ilipokatika simu ya Simon, mzee Msangi akapiga simu kwa Mark the Sniper.
"Vipi mzee, sisi bado tunaliwinda windo lendo" Mark alisema simuni.
"Mark kuna tatizo huku" Mzee Msangi alisema sauti yake ikiwa na uwoga.
"Tatizo gani tena mzee?" Mark aliuliza.
"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis!!"
"Unasemaje mzee?"
"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis" Mzee Msangi alirudia kusema.
"Kwanini Imma amefikia hatua hiyo?"
"Kulitokea kutoelewana na kutoelewana kidogo kati yangu na Imma. Na yeye nd'o akachukua hatua ya kumtorosha Dr Luis" Mzee Msangi alisema.
"Hilo limewezekana vipi? Katika nyumba yenye kamera za ulinzi na walinzi kama hiyo?"
"Imma Ogbo ameweza, ameua walinzi wetu watatu, huku akiacha ameuharibu kabisa mfumo wetu wa ulinzi" Mzee Msangi alisema.
"Hiyo ni mbaya sana kwetu. Si unajua Roho anarudi leo usiku. Na kesho asubuhi inabidi akutane na Dr Luis kwa mahojiano. Tutamweleza nini sasa na tulishamueleza kuwa yupo mikononi mwetu?"
"Yaani hata sielewi. Hapa nimechanyikiwa. Naomba rudini hapa tuone tunafanya nini? Lakini, lazima tumsake Imma Ogbo, apatikane kabla hakujakuchwa. Hii ni kwa kulinda kazi yetu" Mzee Msangi alisema.
"Sasa kuhusu hawa majamaa. Si unajua Ninja na yule mwanajeshi wamewateka wakina Daniel. Hapa tunaelekea Tegeta kwenda kuwamaliza hawa jamaa" Mark alisema.
"Haina shida. Ninja atamaliza kila kitu. Ninyi rudini kwanza huku ili tulimalize hili. Kisha tutamalizana na hao majamaa, kwakuwa wapo mikononi mwetu hakitoharibika kitu"
"Sawa mzee"
Mark The Sniper alisema. Alimwamuru dereva wao ageuze gari na kuelekea Kigamboni.
Mambo yalikuwa yameharibika. Na mharibuji alikuwa ni Imma Ogbo.
"Jamaa wanageuza gari.." Adrian alisema baada ya kuangalia katika vioo vya pembeni.
"Wamestukia nini kama tumemuua mwenzao?" Daniel aliuliza.
"Sidhani kama wamestukia. Sasa yatupasa na sisi tugeuze tuwafatilie wanaenda wapi??" Adrian alisema.
"Jamani, watoto wanguu.." David alisema kwa kulalama.
Daniel na Adrian walimwangalia tu yule mwanajeshi msaliti. Hakuna aliyesema kitu. Huku hasira dhahiri zikionekana usoni mwao.
Adrian akageuza gari na kuanza kuwafatilia wale majamaa. Sasa mchezo ukageuka. Sasa wafatiliaji wakageuka kuwa wafatiliwaji...
"Bila shaka wanatupeleka alipo Dr Luis" Daniel akawaza.
Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
Shusha mzigoRIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391
Sehemu ya kumi na sita
"Sijaelewa unazungumzia nini kijana?" Dr Luis alisema hofu dhahiri ikiwa katika sauti yake.
"Nimesema nataka ututengenezee kirusi cha DH+" Imma Ogbo alirudia tena.
"Unafaham nini kuhusu kirusi cha DH+?" Dr Luis aliuliza huku akiwa katika hali ya wasiwasi.
"Hapa kuna mgawanyo wa kazi. Wewe hauna jukumu la kuuliza maswali. Jukumu lako ni moja tu, kutekeleza kila nikwambiacho" Imma Ogbo alisema.
"Hawa watu wamejuaje kuhusu kirusi cha DH+. Dh+ ni kirusi kibaya sana. Endapo nikitengeneza kirusi cha DH+ na kuwakabidhi watu hawa ambao sijui wanataka kukifanyia nini itakuwa ni hatari sana. Katu siwezi kuwatengenezea kirusi cha DH+. Najua madhara yake ambayo hadi sasa yanamtesa Mheshimiwa rais" Dr Luis akawaza.
"Dr Luis umenielewa nikichokwambia?" Imma Ogbo aliuliza.
Dr Luis alikaa kimya.
"Dr Luis, napenda tuumalize mjadala huu kistaarabu. Sitaki tuumizane ili utekeleze nikwambiacho. Utatutengenezea kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.
Dr Luis alikaa kimya.
"Hii ni mara ya mwisho kukwambia kistaarabu. Naona unataka kuujua upande wangu wa pili. Mimi ni tafsiri sahihi ya neno ukatiri!!"
"Nitawatengenezea kirusi cha DH+, lakini kwa masharti mawili" Dr Luis alisema kwa uwoga.
"Haujaja kutupa masharti hapa!!" Imma Ogbo alifoka.
"Basi kama hutaki nikupe masharti, nisrme tu sitowatengenezea hiko kirusi. Nifanyeni mnavyoweza" Dr Luis alisema.
"Narudia kwa mara ya mwisho Dr Luis, sitaki nitumie nguvu ili kutekeleza hiki nikwambiacho!" Imma Ogbo alisema.
Dr Luis alikaa kimya.
"Bila hayo masharti yako, upo tayari ututengenezee kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.
"Siwezi kuwatengenezea" Dr Luis alijibu kwa ufupi. Huku macho yake yalimaanisha alichokuwa amekisema.
Mara, simu ya Imma Ogbo iliita. Alikuwa ni mzee Msangi.
"Eeeh nambie mzee..bado naendelea na mahojiano.." Imma Ogbo alisema simuni.
"Tumesikiliza majadiliano yako na Dr Luis. Naomba mpe nafasi akwambie hayo masharti" Mzee Msangi alisema.
"Ni nje ya utaratibu mzee. Hatuwezi kupewa masharti na mtu tuliyemteka" Imma Ogbo alisema.
"Mimi ni bosi wako hapa. Naomba fanya nilichokuagiza!" Mzee Msangi alifoka.
"Siwezi kufanya maagizo yako. Hujanileta wewe hapa! Mimi napewa oda na aliyenileta tu, ambaye ni..."
"Come on Imma Ogbo. Toka humo ndani!!" Mzee Msangi alifoka.
"Mzee unajua unachokifanya. Kwanza umekosea kufatilia majadiliano haya. Ndio maana kamera zote za huku zimezimwa. Bila shaka umeweka kamera zako za siri. Hilo ni kosa. Haya ni majadiliano ya siri. Kwahiyo ulikuwa unanichunguza? Umeniuzi sana. Na sasa unataka kuingilia kazi isiyokuhusu. Jua haya si majukumu yako. Na sipo tayari kuteleza usemayo" Imma Ogbo alisema.
Kwa hasira Mzee Msangi alikata simu.
"Twendeni huko shimoni!" Mzee Msangi aliwaambia wenzake. Kila mmoja akatoa bastola yake.
"Imma Ogbo hastahili kuifanya kazi hii" Mzee msangi alisema wakiwa katika korido kuelekea katika chumba cha mateso kilichokuwa chini kabisa ya jengo hilo.
Dakika saba ziliwafikisha shimoni. Cha kushangaza waliukuta mlango wazi. Na tangu kimejengwa chumba hiko hakikuwahi kuwa wazi. Kwa umakini mkubwa wakina mzee Msangi waliingia mle ndani.
Walikutana na jambo la kushangaza sana..
Hakuwepo Imma Ogbo wala Dr Luis...
Harakaharaka Dr Luis alitoa simu yake na kumpigia mkuu wa ulinzi wa lile jengo.
"Simon, kuna watu wawili wametoroka humu ndani. Hakikisha hatoki mtu ndani ya jengo hili. Fikisha taarifa kwa watu wako wote!" Mzee Msangi alifoka.
"Sawa mkuu" Simon alijibu.
Dakika hiyohiyo msako wa kuwasaka Imma Ogbo na Dr Luis ulianza mle ndani ya nyumba.
"Huyu kijana hajui kwa namna gani amefanya jambo la hatari sana. Hajui Dr Luis ni mtu wa muhimu kwetu kwa kiasi gani? Atajutia kwa hiki alichokifanya" Mzee Msangi aliwaza.
Mara simu yake iliita. Alikuwa Simon.
"Vipi Simon mmewapata?" Mzee Msangi aliuliza.
"Hatujafanikiwa mzee. Lakini nyuma ya nyumba tumekuta walinzi wetu watatu wameuwawa. Bila shaka hawa watu wameruka ukuta kwa nyuma. Msako inabidi utoke ndani ya jengo" Simon alisema.
"Umeruhusuje hilo Simon?" Mzee Msangi aliuliza.
"Jamaa walikata mawasiliano. Hata kamera zetu hazikuweza kuwanasa wakati wanatoroka. Wakati mafundi wakijaribu kurudisha nawasiliano yetu, kumbe hao watu ndio walikuwa wanatoroka" Simon alisema.
"Daah tumefanya kosa kubwa sana. Tutamwambia nini Roho?" Mzee Msangi aliwaza.
"Nitakuelekeza cha kufanya Simon. Ngoja nifikirie kidogo" Mzee Msangi alisema.
Ilipokatika simu ya Simon, mzee Msangi akapiga simu kwa Mark the Sniper.
"Vipi mzee, sisi bado tunaliwinda windo lendo" Mark alisema simuni.
"Mark kuna tatizo huku" Mzee Msangi alisema sauti yake ikiwa na uwoga.
"Tatizo gani tena mzee?" Mark aliuliza.
"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis!!"
"Unasemaje mzee?"
"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis" Mzee Msangi alirudia kusema.
"Kwanini Imma amefikia hatua hiyo?"
"Kulitokea kutoelewana na kutoelewana kidogo kati yangu na Imma. Na yeye nd'o akachukua hatua ya kumtorosha Dr Luis" Mzee Msangi alisema.
"Hilo limewezekana vipi? Katika nyumba yenye kamera za ulinzi na walinzi kama hiyo?"
"Imma Ogbo ameweza, ameua walinzi wetu watatu, huku akiacha ameuharibu kabisa mfumo wetu wa ulinzi" Mzee Msangi alisema.
"Hiyo ni mbaya sana kwetu. Si unajua Roho anarudi leo usiku. Na kesho asubuhi inabidi akutane na Dr Luis kwa mahojiano. Tutamweleza nini sasa na tulishamueleza kuwa yupo mikononi mwetu?"
"Yaani hata sielewi. Hapa nimechanyikiwa. Naomba rudini hapa tuone tunafanya nini? Lakini, lazima tumsake Imma Ogbo, apatikane kabla hakujakuchwa. Hii ni kwa kulinda kazi yetu" Mzee Msangi alisema.
"Sasa kuhusu hawa majamaa. Si unajua Ninja na yule mwanajeshi wamewateka wakina Daniel. Hapa tunaelekea Tegeta kwenda kuwamaliza hawa jamaa" Mark alisema.
"Haina shida. Ninja atamaliza kila kitu. Ninyi rudini kwanza huku ili tulimalize hili. Kisha tutamalizana na hao majamaa, kwakuwa wapo mikononi mwetu hakitoharibika kitu"
"Sawa mzee"
Mark The Sniper alisema. Alimwamuru dereva wao ageuze gari na kuelekea Kigamboni.
Mambo yalikuwa yameharibika. Na mharibuji alikuwa ni Imma Ogbo.
"Jamaa wanageuza gari.." Adrian alisema baada ya kuangalia katika vioo vya pembeni.
"Wamestukia nini kama tumemuua mwenzao?" Daniel aliuliza.
"Sidhani kama wamestukia. Sasa yatupasa na sisi tugeuze tuwafatilie wanaenda wapi??" Adrian alisema.
"Jamani, watoto wanguu.." David alisema kwa kulalama.
Daniel na Adrian walimwangalia tu yule mwanajeshi msaliti. Hakuna aliyesema kitu. Huku hasira dhahiri zikionekana usoni mwao.
Adrian akageuza gari na kuanza kuwafatilia wale majamaa. Sasa mchezo ukageuka. Sasa wafatiliaji wakageuka kuwa wafatiliwaji...
"Bila shaka wanatupeleka alipo Dr Luis" Daniel akawaza.
Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212392
Sehemu ya Kumi na nane
Songelael Ntenga P.A.K Mwanasheria mlevi alikuwa amekaa makao makuu ya usalama wa Taifa. Alikuwa amekaa ofisini, mbele yake kukiwa na meza kubwa yenye mafaili mbalimbali, yakiyopepewa na upepo wa feni.
"Sijazoea kabisa hizi kazi za kukaa ofisini. Mi furaha yangu ni kuwa katika hekaheka mtaani na kuwasaka wahalifu. Lakini kwasasa Chifu amenipa heshima kubwa sana ya kuwa mkuu wa kitengo cha mawasiliano hapa makao makuu. Lakini, roho yangu haijakongeka hata kidogo. Nimemiss sana mikimiki ya mitaani, na kufumbua mafumbo magumu yanayoumiza kichwa. Naupenda sana upelelezi..Hakuna ka.." Mwanasheria mlevi akakatishwa katika mawazo yake. Simu yake ya mkononi iliyokuwa juu ya faili moja, ilikuwa inaita.
"Nani huyu anayenipigia simu? Namba hii wanaojua ni watu wachache sana, lakini sio namba ngeni?" Mwanasheria mlevi alijiuliza.
Akaipokea.
"Daniel Mwaseba hapa naongea" Sauti ilisema simuni.
"Daniel, kulikoni? Mbona umenipigia kwa namba ngeni?" Mwanasheria mlevi aliuliza.
"Tutaongea kwa kirefu baadae Mwanasheria. Lakini kwa sasa kuna kazi moja naomba uisaidie" Daniel aliongea harakaharaka.
"Kazi gani hiyo Daniel?" Mwanasheria aliuliza.
"Najua kwasasa upo katika kitengo cha mawasiliano hapo makao makuu. Sasa kuna namba moja ya simu nataka uichunguze. Nataka unambie namba hiyo inamilikiwa na nani? Na watu gani inayowasiliana nao mara kwa mara?" Daniel alisema.
"Nitumie hiyo namba Daniel. Hesabu hilo limekwisha. Nitakupa majibu soon. Eeh nambie kingine unachohitaji kutoka kwangu?" Mwansheria aliuliza.
"Kwasasa nahitaji hilo tu la namba. Ni muhimu sana, nikitaka kitu kingine nitawasiliana na wewe" Daniel alisema.
"Halafu unadrive Daniel? Unaenda kwa kimada nini?" Mwanasheria mlevi alibadili namba.
"Hapana, ila nipo kwenye gari. Kuna wachawi ninawafukuzia hapa"
Mwanasheria mlevi akapiga ngumi ya nguvu katika meza.
"Nimemiss sana maisha hayo!" Akasema kwa hisia.
Daniel Mwaseba alikuwa ameshakata simu.
Muda huohuo, Mwanasheria mlevi akatoka mle ofisini. Akaenda kwenye chumba cha pili ambapo kulikuwa na kompyuta mbili katika meza tofauti. Akaenda kukaa katika kiti, mbele ya kompyuta mojawapo. Sekunde hiyohiyo, mlio wa meseji ulisikika katika simu yake. Ilikuwa ni namba ya simu aliyotumiwa na Daniel Mwaseba. Akaingiza ile namba katika kompyuta ambayo ilikuwa na program ya kutambua namba za watu.
Majibu aliyokutana nayo huko...yalimwacha mdomo wazi....
***
Viongozi mbalimbali walikuwa wamejaa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Ilikuwa ni siku maalum ambayo rais Mgaya alikuwa amemaliza ziara ya wiki moja nchini Nigeria, hivyo anarejea nyumbani. Ziara ya wiki moja nchini Nigeria iliisha kwa mafanikio makubwa sana, baada ya rais Mgaya na rais Abayo wa Nigeria kusaini mikataba mikubwa mbalimbali ya ushirikiano, lakini mkataba mkuwa ulikuwa ni ushirikiano katika suala la mafuta.
Itifaki ilizingatiwa katika uwanja wa ndege. Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kama mkuu wa mkoa mwenyeji alikuwa amesimama na viongozi mbalimbali. Makamu wa rais, waziri mkuu, spika wa bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na jaji mkuu walikuwa wakipiga makofi wakati rais Mgaya akishuka ndani ya ndege ya shirika la ndege la Tanzania.
Vikundi mbalimbali vya ngoma vilikuwa vinaburudisha pale uwanjani. Huku wanasarakasi nao wakibiringita ardhini kuonesha umahiri wao.
Rais Mgaya, aliyekuwa amevaa suti nzuri ya kijivu. Alikuwa anashuka katika ngazi ndefu za ndege akifuatiwa na walinzi wake kwa nyuma. Alionekana ni mtu mwenye furaha machoni kwa kumwangalia, hakuna aliyekuwa anajua lililokuwa linapita kichwani mwake. Alikuwa hana furaha hata chembe.
Pale uwanja wa ndege ilifanyika hafla fupi ya pongezi. Viongozi mbalimbali walihutubia, na mwishoni kabisa hotuba ikimaliziwa na mheshimiwa rais Mgaya.
Baada ya hotuba hiyo, msafara ulianza kuelekea ikulu. Ndani ya gari rais Mgaya alitulia kimya. Alionekana ndani ya gari kimwili, lakini mawazo yake yalikuwa yanawaza kitu kimoja tu, Dr Luis.
"Mzee Msangi ameniangusha sana katika kazi hii. Nimemtumia katika kazi zangu za siri nyingi na ngumu sana. Lakini nashangaa ameshindwa kufanya kazi hii ndogo sana. Kazi ilikuwa ni kumteka Dr Luis na kumuua!!.
Zoezi la kwanza lilifanikiwa kwa ufanisi mkubwa sana, sasa iweje washindwe kumuua mtu aliyekuwa mikononi mwao?.
Ni kosa kubwa sana amefanya, haitakiwi hata kidogo Dr Luis awe hai. Siku akifumbua mdomo wake na kusema siri zangu. Basi ndoto ya kugombea awamu ya pili ya urais itakuwa imefutika. Na hilo sitaki litokee kwa namna yoyote ile. Nitatumia nguvu zangu zote kama rais kuhakikisha Dr Luis anakufa!
Nilitegemea kupokea simu ya mzee Msangi kuwa zoezi limekamilika, eti ananambia Dr Luis ametoroshwa na Imma Ogbo.
Who is Immanuel Ogbo. Ni rais Abayo wa Nigeria ndiye aliyenitambulisha kwa mtu anayeitwa Imma Ogbo. Nikifika Ikulu nitampia simu nimweleze kitendo alichokifanya mtu wake. Hakutumwa kuja kufanya kazi ya kuteka watu hapa..." Rais Mgaya alikatishwa mawazo yake na simu.
Alikuwa ni mkuu wa Polisi IGP John Rondo.
"Shikamoo mheshimiwa rais" IGP Rondo aliamkia.
"Marhaba IGP, vipi mnaendeleaje na kazi ya kumtafuta Dr Luis?" Rais Mgaya aliuliza.
"Na hilo ndilo lililonifanya nikupigie mheshimiwa rais. Nimeongea na Daniel Mwaseba sasahivi. Anasema zoezi linaenda kufika mwisho. Hivi sasa wanaenda mahali alipofichwa Dr Luis huko Kigamboni. Hivyo Dr Luis atakuwa mikononi mwetu sio muda mrefu kutokea sasa" IGP Rondo alisema.
"Kazi nzuri sana IGP wangu. Mimi nipo njiani naelekea ikulu. Nitakupigia nitakapofika ikulu" Rais Mgaya alisema na kukata simu.
Alikuwa ameyakatisha maongezi harakaharaka kwa makusudi.
Kisha akampigia simu mzee Msangi....
Je nini kitatokea? tuwe wote katika sehemu ijayo.