Bomu la wanafunzi litaiangusha hii serikali!

Bomu la wanafunzi litaiangusha hii serikali!

Huu ujumbe ni wa kwako wewe unayejifanya shida za watanzania huzijui kiasi cha kutoa maneno ya kashfa. Soma vizuri hamna sehemu nimeandika serikali. Mimi nakuapia maisha yatakugonga hutokaa uamini kama ni wewe!
Ndg hapa hatujadiri personalities tunaongelea serikali.
 
Ndg hapa hatujadiri personalities tunaongelea serikali.
Unless you mean personal sijaelewa hapo kwenye personalities unamaanisha nini hasa.
Na je wewe haya majibu unayotoa unatoa kama serikali?
 
Watoto gani hawaendi shule, wapo wa ngapi kati ya wangapi ambao hawasomi? Hivi wanafunzi wa veta, vyuo vya ualimu, nursing, vyuo vya utalii wanasoma kwa mkopo upi wa serikali, nenda Kenya au Uganda, Drc tuambie ni wanafunzi kiasi gani wanakopeshwa na serikali ukilinganisha na Tanzania?
Kila nchi imejiwekea utaratibu wakuendeleza elimu kwa wananchi wake kama ambavyo sisi tumepitisha sheria ya Bodi ya mikopo.
Fedha za kuwakopesha wahitaji zinatengwa kila mwaka sasa tatizo linatoka wapi.
Au bajeti ya Bodi ya mikopo ilikikuwa hewa pamoja nakuekezwa kuwa bajeti ya mwaka huu imeongezeka sana lakini wanufahika wa mikopo wanasekana kutoka 55'000 wa mwaka jana hadi 25'000 mwaka huu
 
Kila nchi imejiwekea utaratibu wakuendeleza elimu kwa wananchi wake kama ambavyo sisi tumepitisha sheria ya Bodi ya mikopo.
Fedha za kuwakopesha wahitaji zinatengwa kila mwaka sasa tatizo linatoka wapi.
Au bajeti ya Bodi ya mikopo ilikikuwa hewa pamoja nakuekezwa kuwa bajeti ya mwaka huu imeongezeka sana lakini wanufahika wa mikopo wanasekana kutoka 55'000 wa mwaka jana hadi 25'000 mwaka huu

Je kama hawana sifa ya kukopeswa unataka wapewe tu kwa kuwa hela idadi ni imepungua na hivyo hela itakuwepo tu?
Je hao 55,000 ni mwaka wa kwanza tu au wanafunzi wote waliodahiriwa (mwaka wa kwanza na kuendelea).
 
Hio sheria ya HESLB ilitungwa na serikali ipi? Mbona unalazimisha utofauti? HESLB ya serikali ambayo siyo CCM ?
jibu hoja,ni sheria ipi ilianzisha Heslb?hujui muulize kiongozi wako Magufuli
 
Sihitaji kiki, mkopo wa wanafunzi si shamba la bibi? Unapewa mkopo kwa taratibu na kwa vigezo.
Hujanijibu wewe ni msemaji wa serikali? Au wewe ni serikali?
Halafu acha kujichanganya, unafikiri ambao hawajapata hawana vigezo?
No wonder unajitutumua humu ili mkono uende kinywani, kichwani hamna kitu humo. I feel for people who have to live with you on daily basis, you're so empty headed!
 
Mtaendelea kulia lia na kulalamika tu.walipieni watoto wenu si mkakope benki?suala la kusomesha mtoto sio la serikali hilo ni la familia,mkopo sio lazima
wacha wee..

unaongea ukiwa umeshiba kwa raha zako...
 
Yaani kwa hoja hizi ndio mnajiaminisha kuwa serikali itatikisika kwa suala la mikopo? Hizi kelele zote ni njaa ya kushika pesa na wala si kusoma.

Unafahamu mkopo unatolewa chini ya sera ya cost sharing? Kama ni cost sharing basi nikuulize wewe unayelilia mkopo umechangia nini?
kodi.
 
Watoto gani hawaendi shule, wapo wa ngapi kati ya wangapi ambao hawasomi? Hivi wanafunzi wa veta, vyuo vya ualimu, nursing, vyuo vya utalii wanasoma kwa mkopo upi wa serikali, nenda Kenya au Uganda, Drc tuambie ni wanafunzi kiasi gani wanakopeshwa na serikali ukilinganisha na Tanzania?

Hii ni Tanzania sio Kenya wala Uganda.Kama Mwasisi wa Taifa letu aliweza kusomesha Bure kuanzia Ada mpaka nauli tena kwa kutegemea Mazao kwa nini tushindwe sasa?.Unafananisha na Kenya na Uganda,Ina maana unatamani na Mabaya yaliyoko Kenya na Uganda?
 
UVCCM...kwa heshima na taadhima muwasihi hao vijana waliokosa mikopo wasijaribu kuandamana..watakion kilichomyima kuku mkojo.
Kamanda wa mafunzo wa jeshi la polisi....tafadhali fanyisha askari mazoezi ya utayari kama yale ....
Jet fighters zipashwe moto zimekaa muda bila kuruka.
Wakuu wa mikoa andaeni siku za kimikoa
Kama usafi..nk..nk
 
hao wanao ropoka wazaz wao wanauwezo wa kusomeshwa bila matatizo angalien n upande wa pili si mumkopeshe huyo mwanafunz atimize ndoto kaze sio kukatishan njian jmn sio wote wanauwezo hali zinatofautian n mazingira y mzazi.
 
Hujanijibu wewe ni msemaji wa serikali? Au wewe ni serikali?
Halafu acha kujichanganya, unafikiri ambao hawajapata hawana vigezo?
No wonder unajitutumua humu ili mkono uende kinywani, kichwani hamna kitu humo. I feel for people who have to live with you on daily basis, you're so empty headed!

Tatizo umekariri na unataka mambo yaende unavyotaka, hata kwa kuruka kanuni (huo ni udhaifu).
Taratibu zipo clear, kama unaona una vigezo na umeachwa unaruhusiwa kukata rufaa.
 
Tunakokwenda siyo. Maelfu ya wanafunzi wamekosa mikopo, wako mitaani na bila shaka watalazimika kuandamana kudai haki yao ya msingi, yaani Elimu. Polisi watatumia nguvu nyingi kuwanyamazisha, ila haitawezekana, kwa maana kwamba wananchi nao watawaunga mkono. Na hili swala litakuwa ni tatizo ambalo halitazimika kamwe.

Nadhani serikali iangalie hili swala la mikopo kwa wananfunzi kwa jicho la pili. Hili ni bomu na tishio kubwa sana kwa huu utawala
Siyo kwa nchi hii.
 
Acheni porojo zenu hum...
Mlipewa option mbili....Elimu bure mpaka O~Level na Elimu bure mpaka chuo kikuu...
Mkachagua Elimu bure mpaka O~level sasa mnacholalamika ni nn

Hapa kazi tuu....Rudini kwenu mkalime mvua zimeanza kunyesha
Hapana ndugu yangu, tulichagua elimu bure hadi chuo kikuu lakini wenye nguvu wakatupora, ndiyo maana vituo vya kuhakiki kura vikaingiliwa na computer kuharibiwa. Sasa sote tunaisoma namba.
 
Kwa nini serikali isiweke utaratibu wa kukopesha wafanyakazi wanaojiendeleza na wenye uhakika wa kulipa hata kwa pensheni yao? Na pia watoe mikopo kwa kozi za vipaumbele vya taifa sababu huyu mfanyakazi anyekuja kusoma na ukasema ajisomeshe kumbuka anakuwa na madeni benki kibao ili kujiletea Maendeleo yake na familia!
 
Kitu cha kuelewa ni kwamba kukopeshwa ni hiyari tu ya mkopeshaji ila kulipa ni lazima .

Kuna sehemu nimeona tulipokwama baada ya watu miaka ya nyuma waliokopa kuacha kulipa ndio ile hela haizunguki tena sasa Bodi inatakiwa ijiendeshe kupitia fedha hizo na sio serikali kutoa fedha kila Mara .

Waliosoma kwa mikopo walipe ili wengine wakopeshwe.
 
Haki ya kusomesha inaanza kwa mzazi,mkopo haujaandikwa popote kwenye katiba,serikali haiwezi kuanguka kwa siasa hizi nyepesi.Somesheni watoto kwa pesa yenu,serikali inawajibu wa kujenga miundombinu ya elimu acheni kujisahau
Ingekuwa ivyo serkali ili kuwa na maana gan kuweka elimu bure
 
ndo sababu watu hawarudishi mkopo kwa mda, wanachelewa kutupa wategemee si tuwahi si ufala huo
 
Back
Top Bottom