Bomu la wanafunzi litaiangusha hii serikali!

Bomu la wanafunzi litaiangusha hii serikali!

Labs za vyuo vingi computers zimekufa inatakiwa mwanafunzi anunue laptop yake, lectures wanatoa softcopy Kama una computer basi ukaprint hiyo ni cost nyingine, vyuo vingi havina hostels za kutosha inampelekea mwanafunzi akapange chumba nje ya chuo, ada ya chuo haipungui 1.25 million Kwa vyuo vingi hapa Tz Na hapo hujaweka Na gharama nyingine za bima n.k. Nauli+usumbufu Kwenye mabasi pia ni tatizo. Kama mtu alisoma shule za serikali o-level na A-level kutokana na uwezo mdogo wa pesa wa wazaZi wake basi usitarajie wataweza kumlipia mtoto huyo ada ya chuo na akasoma Kwa amani bila ya kuwa na stress. Mikopo Kwa elimu ya juu ni muhimu kuliko ambavyo serikali inafikiria especially Kwa nchi masikini ambazo unakuta mzazi hajasoma na hajui chochote kuhusu elimu ya juu.
Nachoona serikali inawaadhibu wanafunzi wa vyuo Kwa kosa lililofanywa na viongozi wa awamu zilizopita, awamu zilizopita zilishindwa kuicommand HESLB idai mikopo Kwa wanafunzi waliomaliza, sitaki kuamini bodi ya mikopo ilishindwa kupata mbinu ya kurudisha pesa zao kutoka Kwa wadaiwa wake hadi inafikia watu wa 1994 hawajalipa mikopo. Kuna sehemu nyingi za kuwabana watu na ukawapata like TRA, ubalozini, Serikali za mitaa, viwanja vya ndege n.k.
Solution ni Serikali kuhakikisha HESLB inalipwa madeni yake Kwa wanafunzi waliomaliza hadi itapokuwa stable kujitegemea na Sio kuwapa bajeti ndogo Kwa kisingizio cha ufinyu wa pesa. Nchi haiwezi kuendelea Kwa kusomesha wanasayansi tu, kila fani ina MCHANGO wake katika jamii Kama ikitumiwa vizuri. Bado naona kuna tatizo kubwa Kwenye elimu yetu.
Nakumbuka kuna rafiki yangu aliniambia tatizo la watanzania ni "njaa", mtu akiwa Na njaa anakuwa mvivu wa kufikiri. Yani ukiangalia wabunge wengi wakuu wa mikoa Na wilaya, wakurugenzi wamenufaika na mikopo ya elimu ya juu pamoja Na kusoma masomo ya arts lakini wanajisahau kabisa kutetea wadogo zao. So sad
 
Nini maana ya mkopo????
It means ni pesa unayopewa uitumie alaf baadae utairejesha....
Sasa serikali mbona inawanyanyasa wanafunzi kana kwamba ni pesa ya msaada?????
Hili ndio kubwa la kushangaza kuliko yote!
 
Haki ya kusomesha inaanza kwa mzazi,mkopo haujaandikwa popote kwenye katiba,serikali haiwezi kuanguka kwa siasa hizi nyepesi.Somesheni watoto kwa pesa yenu,serikali inawajibu wa kujenga miundombinu ya elimu acheni kujisahau
Wengine majibu yenu huwa yananitamanisha hii ingekuwa tv tuonane uso kwa macho!
 
kwenye hili lakopo refer hotuba ya mkulu wakati anaomba kura alisemaje?
 
Wapi imeandikwa kua lazima ukopeshwe.Tumechelewa sana kwa mambo ya kubweteka haya
Kamuulize kwanza huyo anayewanyima watoto mikopo yeye alilipa shilingi ngapi wakati anasoma?!
 
Bomu la wanafunzi kwa serikali ya ccm halina impact kubwa saaana maana huwa wanacheza na vyuo tu, si unajua huwa wanafunga vyuo kabla ya uchaguzi
 
Kamuulize kwanza huyo anayewanyima watoto mikopo yeye alilipa shilingi ngapi wakati anasoma?!
Mtaendelea kulia lia na kulalamika tu.walipieni watoto wenu si mkakope benki?suala la kusomesha mtoto sio la serikali hilo ni la familia,mkopo sio lazima
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Kukojoa ukojoe wewe,utegemee mwanao asomeshwe kwa mkopo wa serikali,watapata wenye vigezo kwa 100%,wengine kakopeni benki msomeshe wanenu,mmebweteka na kuona kama vile lazima,ile ilikua juhudi ya serikali kuingiza wanafunzi kwa wingi.Sasa kuna UDOM,MUHAS,UCLAS na UDSM vinatosha kabisa kufikia malengo ya serikali
Nadhani haya ni maoni ya mtu ambaye hajui umuhimu wa elimu au yeye ni mmoja wa watendaji wakuu serikalini anayepaswa kutetea maovu ya serikali au ni fisadi anayetumia rasilimali za taifa kiharamu hivyo ana vihela vya kubabaishia watu wengine.
Kumbuka haya yote huwa na mwisho kama si duniani basi ni kaburini.
 
Mtaendelea kulia lia na kulalamika tu.walipieni watoto wenu si mkakope benki?suala la kusomesha mtoto sio la serikali hilo ni la familia,mkopo sio lazima
Toa ushahidi wa malipo ya elimu yako hapa ili tujue unaongea vitendo sio porojo.
 
Wapi imeandikwa kua lazima ukopeshwe.Tumechelewa sana kwa mambo ya kubweteka haya
Kumbe kwa uelewa wako mkopo ni hisani kwa wanafunzi.
Na ni hela inatoka mfukoni mwa mtu kwa kadri anavyotaka.
La hasha kila kitu kimeandikwa nakupitishwa bungeni ndio maana ikapitishwa bajeti ya billioni 400 kwa minajiri hiyo,
Kwa hiyo inatekelezwa sheria si utashi wa mtu,kwa hiyo kama mtu anakidhi vigezo anastahili kunufahika na mkopo.
Mwisho wa siku anapashwa kurudisha mkopo na riba.
Usiwe mvivu wakufikiri hizo hela zilitungiwa sheria na kwa taarifa yako ni kodi yako na yangu ndio maana iko kwenye bajeti.
Wewe ulitaka iandikwe vipi zaidi mswaada kupitishwa bungeni nakuwa sheria,angalia mihemko ya kisiasa italupeleka taifa pabaya.
 
Ni heri niseme hivi. Viongozi wote na watumishi wote waliopo serekalini. Mashirika ya umma. Wafaniabiashara waliosoma. Mafundi wote waliosoma. Hakuna hata mmoja wao aliye soma kwa mkopo au fedha za wazazi wake. Wote tumesoma kwa fedha ya serekali ya Tanzania. Ukiwa wewe ni mzazi mwema huwezi kumkopesha mtoto wako ada ya shule. Badala yake mzazi anapaswa kufanyia kila juhudi ili mtoto asome. Waliopendekeza mpango wa mikopo kwa wanafunzi wetu ni watu wenye umaskini wa mawazo. Hawana tofauti na wale waliofikiri kuwa kwanza kinawezekana kwa kutumia pawatila. Watanzania tuukatae mpango huu. Badala yake tuunde mfuko wa elimu ambao utachangiwa na watanzania wote ili kila mtoto mwenye sifa ya kusoma asome bila shida. Tupanue hili wazo litatusaidia.
 
Acheni porojo zenu hum...
Mlipewa option mbili....Elimu bure mpaka O~Level na Elimu bure mpaka chuo kikuu...
Mkachagua Elimu bure mpaka O~level sasa mnacholalamika ni nn

Hapa kazi tuu....Rudini kwenu mkalime mvua zimeanza kunyesha
 
There is something called KARMA, if you think you have everything today to the extent of ignoring what people are going through because they dont have enough money then just wait. Whether today or the day after karma will find you then you'll regret all this nonsense you are writing now.
Hio KARMA inatokea kwa binadamu tu? Well mbona mnaikomalia serikali ikoposhe wanafunzi tu kwani haina majukumu mengine? Yenyewe hata kama bajeti imeisha na wanafunzi wengine hawakopesheki mnataka tu, kwa sababu ya KARMA, hovyo sana wewe.
 
Hio KARMA inatokea kwa binadamu tu? Well mbona mnaikomalia serikali ikoposhe wanafunzi tu kwani haina majukumu mengine? Yenyewe hata kama bajeti imeisha na wanafunzi wengine hawakopesheki mnataka tu, kwa sababu ya KARMA, hovyo sana wewe.
Huu ujumbe ni wa kwako wewe unayejifanya shida za watanzania huzijui kiasi cha kutoa maneno ya kashfa. Soma vizuri hamna sehemu nimeandika serikali. Mimi nakuapia maisha yatakugonga hutokaa uamini kama ni wewe!
 
na vyeo vimeisha,utaishia kupata ukamanda wa CCM tu.
Akili ndogo.Kwani unaijua sheria iliyoanzisha HESLB?Au ccm akili tumboni?
Hio sheria ya HESLB ilitungwa na serikali ipi? Mbona unalazimisha utofauti? HESLB ya serikali ambayo siyo CCM ?
 
Labs za vyuo vingi computers zimekufa inatakiwa mwanafunzi anunue laptop yake, lectures wanatoa softcopy Kama una computer basi ukaprint hiyo ni cost nyingine, vyuo vingi havina hostels za kutosha inampelekea mwanafunzi akapange chumba nje ya chuo, ada ya chuo haipungui 1.25 million Kwa vyuo vingi hapa Tz Na hapo hujaweka Na gharama nyingine za bima n.k. Nauli+usumbufu Kwenye mabasi pia ni tatizo. Kama mtu alisoma shule za serikali o-level na A-level kutokana na uwezo mdogo wa pesa wa wazaZi wake basi usitarajie wataweza kumlipia mtoto huyo ada ya chuo na akasoma Kwa amani bila ya kuwa na stress. Mikopo Kwa elimu ya juu ni muhimu kuliko ambavyo serikali inafikiria especially Kwa nchi masikini ambazo unakuta mzazi hajasoma na hajui chochote kuhusu elimu ya juu.
Nachoona serikali inawaadhibu wanafunzi wa vyuo Kwa kosa lililofanywa na viongozi wa awamu zilizopita, awamu zilizopita zilishindwa kuicommand HESLB idai mikopo Kwa wanafunzi waliomaliza, sitaki kuamini bodi ya mikopo ilishindwa kupata mbinu ya kurudisha pesa zao kutoka Kwa wadaiwa wake hadi inafikia watu wa 1994 hawajalipa mikopo. Kuna sehemu nyingi za kuwabana watu na ukawapata like TRA, ubalozini, Serikali za mitaa, viwanja vya ndege n.k.
Solution ni Serikali kuhakikisha HESLB inalipwa madeni yake Kwa wanafunzi waliomaliza hadi itapokuwa stable kujitegemea na Sio kuwapa bajeti ndogo Kwa kisingizio cha ufinyu wa pesa. Nchi haiwezi kuendelea Kwa kusomesha wanasayansi tu, kila fani ina MCHANGO wake katika jamii Kama ikitumiwa vizuri. Bado naona kuna tatizo kubwa Kwenye elimu yetu.
Nakumbuka kuna rafiki yangu aliniambia tatizo la watanzania ni "njaa", mtu akiwa Na njaa anakuwa mvivu wa kufikiri. Yani ukiangalia wabunge wengi wakuu wa mikoa Na wilaya, wakurugenzi wamenufaika na mikopo ya elimu ya juu pamoja Na kusoma masomo ya arts lakini wanajisahau kabisa kutetea wadogo zao. So sad
You have a point, ila unapoweka hii point yako jaribu na kuiweka kwenye sera ya "cost sharing".
 
Kamuulize kwanza huyo anayewanyima watoto mikopo yeye alilipa shilingi ngapi wakati anasoma?!
Hivi VETA na vyuo vya ualimu kwa mfano, nani huwa anawapa mikopo?
 
Nini maana ya mkopo????
It means ni pesa unayopewa uitumie alaf baadae utairejesha....
Sasa serikali mbona inawanyanyasa wanafunzi kana kwamba ni pesa ya msaada?????
Kukopeshwa ni lazima?
 
Kumbe kwa uelewa wako mkopo ni hisani kwa wanafunzi.
Na ni hela inatoka mfukoni mwa mtu kwa kadri anavyotaka.
La hasha kila kitu kimeandikwa nakupitishwa bungeni ndio maana ikapitishwa bajeti ya billioni 400 kwa minajiri hiyo,
Kwa hiyo inatekelezwa sheria si utashi wa mtu,kwa hiyo kama mtu anakidhi vigezo anastahili kunufahika na mkopo.
Mwisho wa siku anapashwa kurudisha mkopo na riba.
Usiwe mvivu wakufikiri hizo hela zilitungiwa sheria na kwa taarifa yako ni kodi yako na yangu ndio maana iko kwenye bajeti.
Wewe ulitaka iandikwe vipi zaidi mswaada kupitishwa bungeni nakuwa sheria,angalia mihemko ya kisiasa italupeleka taifa pabaya.
Wewe hovyo sana, mkopo wa wanafunzi hauna riba.
 
Back
Top Bottom