technically
JF-Expert Member
- Jul 3, 2016
- 13,634
- 58,270
Unatoa elimu Bure kuanzia darasa la kwanza mpaka form four...
Unatoa mkopo chuo kikuu miaka mitatu..
Unamwandaa kijana awe mwalimu na sio fani nyingine yeyote....
Kijana anamaliza degree hana kazi yupo mtaani unategemea akafanye kazi gani?.....
Si ni bora wangeandaliwa walimu wachache wanaoweza kuajiriwa kirahisi?.....
Tukiongea tunaambiwa wapiga dili hasa mtu kusoma kutoka darasa la kwanza mpaka chuo kikuu unafikiri anakuwa kapoteza kiasi gani cha pesa za serikali na za wazazi je izo pesa zinarudi vipi kama ni jobless?..
Tufike wakati tuwe na uchungu kwa vijana wanaosoma kwa shida kiukweli ni mateso ..
Serikali itoe ajira watu warudishe mikopo walipe kodi wengine wasome kama hatutoi ajira maana yake kuna muda utafika hata pesa ya kukopesha wanafunzi itakosa...
Serikali imetengeneza walimu walio mtaani 91,000 na mwezi wa saba wengine wanamaliza wewe unatoa ajira 4500 ambao hata 10% haifiki ..
Halafu wanafunzi hawana walimu uko shuleni wanakaa chini .
Walimu waliopo hawalipwi vizuri tuwe na uchungu jamani mambo haya ndio mambo ya msingi tuwe na hofu ya Mungu.
Akiba ya pesa tunaambiwa ipo si tuwape wadogo zetu ma watoto wetu kazi ?
Kodi sasa hivi si inalipwa kwa wakati sasa shida nini kuwapa kazi wadogo zetu na watoto wetu...?
Hata mkisema mimi sio mzalendo au mimi ni mpiga dili sawa tu nimeshazoea ila nitaongea ukweli mpaka naenda kaburini...
Unatoa mkopo chuo kikuu miaka mitatu..
Unamwandaa kijana awe mwalimu na sio fani nyingine yeyote....
Kijana anamaliza degree hana kazi yupo mtaani unategemea akafanye kazi gani?.....
Si ni bora wangeandaliwa walimu wachache wanaoweza kuajiriwa kirahisi?.....
Tukiongea tunaambiwa wapiga dili hasa mtu kusoma kutoka darasa la kwanza mpaka chuo kikuu unafikiri anakuwa kapoteza kiasi gani cha pesa za serikali na za wazazi je izo pesa zinarudi vipi kama ni jobless?..
Tufike wakati tuwe na uchungu kwa vijana wanaosoma kwa shida kiukweli ni mateso ..
Serikali itoe ajira watu warudishe mikopo walipe kodi wengine wasome kama hatutoi ajira maana yake kuna muda utafika hata pesa ya kukopesha wanafunzi itakosa...
Serikali imetengeneza walimu walio mtaani 91,000 na mwezi wa saba wengine wanamaliza wewe unatoa ajira 4500 ambao hata 10% haifiki ..
Halafu wanafunzi hawana walimu uko shuleni wanakaa chini .
Walimu waliopo hawalipwi vizuri tuwe na uchungu jamani mambo haya ndio mambo ya msingi tuwe na hofu ya Mungu.
Akiba ya pesa tunaambiwa ipo si tuwape wadogo zetu ma watoto wetu kazi ?
Kodi sasa hivi si inalipwa kwa wakati sasa shida nini kuwapa kazi wadogo zetu na watoto wetu...?
Hata mkisema mimi sio mzalendo au mimi ni mpiga dili sawa tu nimeshazoea ila nitaongea ukweli mpaka naenda kaburini...