siriusblack
JF-Expert Member
- Apr 30, 2013
- 223
- 307
Gaidi aweza kutoka dini yoyote na ethnicity yoyote . Kuna motives mbalimbali za ugaidi na sio dini pekee, mtu anaweza akalaghaiwa kwa fedha, akawa na chuki , hata mfadhaiko (depression) tu huweza kupelekea mtu kufanya vitendo vya kigaidi na mwishowe kudhuru wenzake . Kwa hiyo yawezekana kabisa tukio la Arusha ni la kigaidi na wahusika ni Wakristu wenyewe kwa sababu zao wenyewe.
Sina hakika kama kuna mtu yeyote, awe Muislam au Mkristo anafurahia ugaidi kwasababu wanaodhurika au kufa ni ndugu zetu kabisa . Ugaidi haukubaliki popote iwe Africa, Asia , Amerika au popote ulimwenguni
Sina hakika kama kuna mtu yeyote, awe Muislam au Mkristo anafurahia ugaidi kwasababu wanaodhurika au kufa ni ndugu zetu kabisa . Ugaidi haukubaliki popote iwe Africa, Asia , Amerika au popote ulimwenguni
Mwakilishi wa Vatikan UN amechemsha! kwanza bomu la Arusha halina uhusiano na Ugaidi kwasababu waliokamatwa mpaka sasa hivi ni Vijana wa Kikristo na hata Kardinali Pengo kathibitisha hilo! pili huyu Mwakilishi wa Vatikan UN ni Mhindi, na huko kwao India milipuko ya mabomu na ulipuaji wa Majumba ya ibada nikitu cha Kawaida! hasa tukio kubwa la kulipua na kuchoma Msikiti mkubwa wa kihistoria huko Ayodha India mwaka 1992 na kuuliwa mamia ya Waislamu na Baniani lakini Muhindi huyu haoni huko kwao bali macho yake yako Arusha na Afrika!
Huu ni ubaguzi wa rangi unaoonyeshiwa na Mwakilishi huyu wa Papa UN! Milipuko ya mabomu India na Asia hayajafikishwa UN kwanini iwe ni Afrika tu? unaweza kulinganisha mabomu yanayolipuka Afrika na yale ya Asia?