Bomu Arusha - Vatican yawasilisha taarifa UN

Bomu Arusha - Vatican yawasilisha taarifa UN

Status
Not open for further replies.
huyu askofu aanze kwanza kwao INDIA kuna matukio ya ubakaji kula kukicha .... wakatoliki wamelipuana wenyewe kwa wenyewe ...


mna roho mbaya kama majini mnayofuga........watu 'misheni' imewalisha imewavisha imewatibu imewasomesha bure leo shukrani yenu ni kuua.
 
mna roho mbaya kama majini mnayofuga........watu 'misheni' imewalisha imewavisha imewatibu imewasomesha bure leo shukrani yenu ni kuua.

1) sijalishwa na misheni

2) sijasomeshwa na misheni

3) aliyetupa bomu ni victor ambrose "MKRISTO" huyo ndiyo mtuhumiwa number moja kwa mujibu wa serikali ikishirikiana na FBI ambao walifika siku ya pili tu baada ya tukio


 
bomu.jpg

Askofu Mkuu Frances Chullikatt

Tukio la bomu latua UN
Tukio la kutupwa bomu katika Kanisa Katoliki la Joseph Mfanyakazi, Arusha limetua katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN) baada ya kuwasilishwa na Balozi wa Vatican UN, Askofu Mkuu Frances Chullikatt. Askofu Chullikatt anakuwa kiongozi wa kwanza wa Vatican kutoa tamko kuhusiana na shambulizi hilo ambalo mmoja wa viongozi wake alikuwapo.

Bomu hilo lilirushwa katika kanisa hilo wakati likizinduliwa na Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Francisco Padilla Mei 5, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi zaidi ya 50. Wakati wa shambulizi hilo, Askofu Padilla na Askofu Mkuu wa Jimbo la Arusha, Josephat Lebulu walionusurika.

Akihutubia Kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, New York, Marekani juzi, Askofu Chullikatt alisema tukio lililotokea Arusha linadhihirisha kuwa kuna umuhimu ya kupambana na ugaidi katika Afrika ili kuimarisha amani na usalama wa kimataifa.“Unahitajika mshikamano na ushirikiano wa pamoja wa mataifa mbalimbali katika kuchukua hatua za maisha na kulinda haki za binadamu,” alisema Askofu Chullikatt, ambaye amekuwa mwakilishi wa Vatican kwenye Umoja wa Mataifa tangu mwaka 2010.

Askofu Chullikatt, ambaye ni mzaliwa wa India, alisema suala la ugaidi linahitaji kuzuiwa duniani kote na hasa Afrika kutokana na matukio hayo kuharibu maisha ya binadamu na kutokea katika maeneo wanayofanyia ibada. Askofu Chullikatt alisema pale ugaidi unapofanyika kwa kutumia dini, waumini na viongozi wao ni lazima wahakikishe wanapambana nao ili kuutokomeza.

Alisema suala la ugaidi linahitaji viongozi wa kisiasa, kijamii na kidini kulilaani kwani ni la kikatili katika maisha ya binadamu hivyo si vyema kukaa kimya suala hilo linapotokea. Askofu Chullikatt alisema ugaidi unaotokea Afrika unatakiwa kuangaliwa kimataifa ili kuzipa uwezo nchi hizo kupambana na kuzuia matukio hayo.

Shambulio la bomu dhidi ya kanisa la Arusha lilikuwa tukio la pili la ugaidi uliolenga kushambulia wageni nchini. Mara ya kwanza ilitokea mwaka 1998, wakati Ubalozi wa Marekani nchini ulipolipuliwa kwa bomu na kusababisha vifo vya watu kumi na moja huku 85 wakijeruhiwa.


unatakiwa uelewe yeye co raia wa India bali ni Vatican.

Soma kimya kimya hapo kwenye RED then uniambie mtazamo wa huyo Askofu juu ya suala la Arusha.
 
Mwakilishi wa Vatikan UN amechemsha! kwanza bomu la Arusha halina uhusiano na Ugaidi kwasababu waliokamatwa mpaka sasa hivi ni Vijana wa Kikristo na hata Kardinali Pengo kathibitisha hilo! pili huyu Mwakilishi wa Vatikan UN ni Mhindi, na huko kwao India milipuko ya mabomu na ulipuaji wa Majumba ya ibada nikitu cha Kawaida! hasa tukio kubwa la kulipua na kuchoma Msikiti mkubwa wa kihistoria huko Ayodha India mwaka 1992 na kuuliwa mamia ya Waislamu na Baniani lakini Muhindi huyu haoni huko kwao bali macho yake yako Arusha na Afrika!

Huu ni ubaguzi wa rangi unaoonyeshiwa na Mwakilishi huyu wa Papa UN! Milipuko ya mabomu India na Asia hayajafikishwa UN kwanini iwe ni Afrika tu? unaweza kulinganisha mabomu yanayolipuka Afrika na yale ya Asia?

Mkuu Kadogoo unamaanisha kuna dini special kwa ajili ya kufanya ugaidi au ulimaanisha nini?
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom