Hawa TRL waende Nairobi wakaone serikali imewezaje kujenga reli kutoka Mombasa mpaka Nairobi bila kubomoa makazi ya watu. Kwanini kituo cha kushushia ama kubebea abiria kisijengwe nje ya Dodoma badala ya kulazimisha kijengwe kwenye kituo cha zamani.[/QU
Mkuu hakuna cha kujifunza kutoka Kenya kwa sababu zifuatazo
1-Kenya ardhi ni mali ya mtu binafsi sio ya serikali
2-Hakuna aliyevamia sehemu ambayo siyo yake akawekeza
3-Reli ya kisasa ilipopita ni sehemu halali ya shirika la reli Kenya
Hapa kweli
1-Ardhi si mali ya mtu,bali ni mali ya serikali
2-Serikali inakodisha ardhi yake kwa wawekezaji kwa miaka ama 33 ama 66 ama 99
3-Sehemu walipowekeza wawekezaji,kwa maana wamachinga pale DODOMA halikuwa eneo lao.
4-Sisi Watanzania tumezoea kuvamia maeneo,na kuwekeza bila kufuata utaratibu,matokeo yake tunafanya shughuli zetu kisiasa zaidi,badala ya kiserikali,matokeo yake ni kubomolewa kila kukicha.