Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,169
- 48,451
Jana nilipokuwa naangalia kwenye mitandao ya kijamii niliona picha mbali mbali za bomoabomoa ya nyumba inayoendelea Dar es salaam. Pamoja na huzuni, hasira, navilio vilivyokuwa vimetawala zoezi hilo, mimi kwa mtizamo wangu nimeona kwamba zoezi lenyewe litaziathiri sana taasisi za kifedha na uchumi wa nchi kwa ujumla.
Kati ya nyumba zilizobomolewa miongoni mwake kuna nyumba ambazo ziliwekwa dhamana kwa mikopo pia kuna nyumba ambazo zilitumika kama ni anwani za wakopaji. Na kwenye maeneo hayo pia kuna nyumba zilizokuwa zinatumika kama nyumba za biashara zilizotathiminiwa kupata kigezo cha kukopeshwa.
Nyumba za aina hiyo zinapobomolewa zinaleta sintofahamu kubwa sana kwa taasisi za kifedha. Kwa mfano nyumba iliyowekwa dhamana na mkopaji imebomolewa na nyumba iliyotumika kama anwani ya mkopaji nayo imebolewa, na eneo ilikokuwa inafanyika biashara iliyokopeshwa nayo imebomolewa. Hapa taasisi ya kifedha iliyokopesha inawezaje kulipwa?
Halafu eneo lote linalobomolewa, serikali imewahi kujua ni biashara ya thamani kiasi gani ilikuwa inafanyika kwenye eneo hilo? Leo wote waliokuwa wanawazuia bidhaa wafanyabiashra wa eneo hilo wamepoteza wateja na waliokuwa wateja nao wamepoteza mitaji. Ni kwa kiasi gani biashara iliyopootezwa kwenye eneo hilo italeta athari kwenye uchumi wa Dar es salaam na Taifa kwa ujumla?
Wafanyakazi wa serikali ambao watakuwa wanashughulika na matokeo ya ubomoaji huo,ni kwa kiasi gani watashusha ufanisi wao kazini na pia wanawezaje kuhimili makato ya mikopo yao waliyokopa ili kuendeshea shughuli za kujiongezea kipato kwenye maeneo nyumba zilikobomolewa?
Kati ya nyumba zilizobomolewa miongoni mwake kuna nyumba ambazo ziliwekwa dhamana kwa mikopo pia kuna nyumba ambazo zilitumika kama ni anwani za wakopaji. Na kwenye maeneo hayo pia kuna nyumba zilizokuwa zinatumika kama nyumba za biashara zilizotathiminiwa kupata kigezo cha kukopeshwa.
Nyumba za aina hiyo zinapobomolewa zinaleta sintofahamu kubwa sana kwa taasisi za kifedha. Kwa mfano nyumba iliyowekwa dhamana na mkopaji imebomolewa na nyumba iliyotumika kama anwani ya mkopaji nayo imebolewa, na eneo ilikokuwa inafanyika biashara iliyokopeshwa nayo imebomolewa. Hapa taasisi ya kifedha iliyokopesha inawezaje kulipwa?
Halafu eneo lote linalobomolewa, serikali imewahi kujua ni biashara ya thamani kiasi gani ilikuwa inafanyika kwenye eneo hilo? Leo wote waliokuwa wanawazuia bidhaa wafanyabiashra wa eneo hilo wamepoteza wateja na waliokuwa wateja nao wamepoteza mitaji. Ni kwa kiasi gani biashara iliyopootezwa kwenye eneo hilo italeta athari kwenye uchumi wa Dar es salaam na Taifa kwa ujumla?
Wafanyakazi wa serikali ambao watakuwa wanashughulika na matokeo ya ubomoaji huo,ni kwa kiasi gani watashusha ufanisi wao kazini na pia wanawezaje kuhimili makato ya mikopo yao waliyokopa ili kuendeshea shughuli za kujiongezea kipato kwenye maeneo nyumba zilikobomolewa?