Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,890
939
BOMBA LA MAFUTA GHAFI LA AFRIKA MASHARIKI (EACOP)

✍🏻 Huu ni mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Kabaale – Hoima nchini Uganda kwenda kwenye peninsula ya Chongoleani mkoani Tanga nchini Tanzania. Mradi huu una urefu wa jumla ya kilomita 1443 kati ya hizo kilomita 296 zipo nchini Uganda na kilomita 1147 zipo Tanzania.


Bomba linapita katika mikoa nane ya Tanzania Bara ambayo ni;

1.Kagera (Bukoba Vijijini, Muleba na Biharamulo);
2.Geita (Chato, Geita, Bukombe na Mbogwe);
3.Shinyanga (Kahama Mjini);
4.Tabora (Nzega Vijijini, Nzega Mjini na Igunga);
5.Singida (Iramba, Mkalama na Singida Mjini);
6.Dodoma (Kondoa na Chemba);
7.Manyara (Hanang na Kiteto) na
8.Tanga (Kilindi, Handeni Mji, Handeni Vijijini, Korogwe, Muheza na Tanga Mji).

✍🏻 Matokeo ya utafiti uliofanywa na kampuni za kimataifa za utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi za TOTAL, TULLOW na CNOOC ulibaini uwepo wa mafuta ghafi takribani mapipa bilioni 6.5. Kutokana na ugunduzi huo imebainika uwezekano wa kuvuna mapipa kati ya bilioni 1.2 hadi 1.7. Kutokana na mahusiano ya ushirikiano ya muda mrefu na faida za kupitisha bomba nchini Tanzania Serikali ya Uganda na wawekezaji wa mkondo wa juu waliamua kujenga mradi huu kupitia Tanzania kutoka Hoima Uganda hadi Bandari ya Tanga.

✍🏻 Gharama za kukamilisha ujenzi wa mradi wa bomba zinatarajia kufikia takribani Shilingi Trilioni 8 za Kitanzania. Bomba hili litajengwa na kuendeshwa na kampuni za TOTAL ya Ufaransa, CNOOC ya China na TULLOW ya Uingereza, kwa ubia na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

✍🏻 Mradi umetoa ajira 200 kwa watanzania katika kazi za awali. Vilevile kampuni 100 za kitanzania zimepata kazi katika kipindi hiki. Watanzania wame elimishwa kuhusu mradi huu na manufaa yake. Zaidi ya wafanyabiashara 2000 wamepitishwa kwenye fursa zilizopo kwenye mradi. Watanzania wanaozunguka eneo la mradi kutoka wilaya nane (8) wamehamasishwa pamoja na serikali za mitaa.

#AlipoMamaVijanaTupo
#KaziIendelee

IMG-20220213-WA0007.jpg


IMG-20220213-WA0008.jpg


IMG-20220213-WA0009.jpg


IMG-20220213-WA0010.jpg


IMG-20220213-WA0011.jpg


IMG-20220213-WA0012.jpg
 
Hainingii akilin kbsa huu mradi Kwann hayo mafuta wasiya process hpo Happ uganda kwa kuleta mitambo Happ Happ ili Kuja kusafisha mafut ghafi why ?

Wazungu wahuni Sanaa

Na Africa had tuje kuamka si leo had 2100 haiwezekani niwe na mafuta alfu nimbiwe nisafirishe ulaya wakayachuje

HV Nigeria nao wanasafirisha au Ni hapo Happ wanaprocess?

Wakiprocesa Happ happo Uganda maaana yake Ni kwmab Bei ya mafuta Uganda itakuwa very cheap na hakutakuwa na mfumuko wa Bei ktk soko la dunia kwa kuwa mafuta yanapatikana hapo hapo

Mungu tusaidie waafrica tuamke na unyonyaji huu tunayofanyiwa
 
Wananchi walionufaika wako wapi au unasema watakaonufaika?? Niko kandokando mwa mradisijaona kitu.
 
NAOMBA KUJUA:
Tofauti na bandari ya Tanga. Bomba lina faida gani kwenye mikoa, wilaya, kata na vijiji vingine inakopita??
 
NAOMBA KUJUA:
Tofauti na bandari ya Tanga. Bomba lina faida gani kwenye mikoa, wilaya, kata na vijiji vingine inakopita??
Kipindi ujenzi kutakuwa ajira za muda hadi likiisha kujengwa baada hapo faida yetu sote kwa mgswanyo waliokubaliana......
 
Kipindi ujenzi kutakuwa ajira za muda hadi likiisha kujengwa baada hapo faida yetu sote kwa mgswanyo waliokubaliana......
Unaweza kuweka huo mgawanyo wa ajira na ujira alkadhalika manufaa baada ya ujenzi kukamilika??
Je, wanaopisha maeneo ya mradi wamekuwa equally/fairly compensated??
 
Huu mradi umekuwa ukisua sua kwa muda mrefu saana tumeusubiri lakini wapi, wanasiasa punguzeni shobo na miradi ya watu.
 
Back
Top Bottom