Bodi ya Pamba: Mfano wa kuigwa Duniani

Bodi ya Pamba: Mfano wa kuigwa Duniani

Siyo bure nimepita kanda ya ziwa wiki mbili zilizopita hali ni mbaya sana wakulima wanalalamika kweli, wengi wanalima choroko.
 
Choroko haitawapeleka popote. Hao wakulima watulie tunahitaji pamba kwa wingi viwandani
 
tukumbuke Bila pamba hakuna kiwanda cha nguo.
cc. Pamba Sports Club a.k.a Wana-TP Lindanda.
 
Sisi wakulima wa Pamba kanda ya Ziwa tunajivunia bodi ya Pamba Tanzania kwa kufanya kazi zake kwa WELEDI mkubwa katika kututafutia masoko ndani na nje ya nchi kwa uharaka sana. Wakulima wenzangu wa pamba ni mashahidi kwa hili kwani tunajivunia pamba na jasho letu wengi wetu tumeweza kuwekeza katika miraid mikubwa mikubwa ya maendeleo na kilio cha kisasa kabisa (Teknolojia za kisasa) Kama ingekuwa uwezo wangu ningepandisha hadhi bodi hii na iwe wizara kamili (WIZARA ya MAENDELEO ya PAMBA)
** WEBSITE: www.cotton.or.tz
NB: Wafanyakazi wa bodi hii wanastahili pongezi hasa tukiazimisha siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi)
Uzuri wa taasisi yoyote ni pale ambapo inaweza kuwasaidia watu wakati wa matatizo. Kwa kusema hivyo nina maana bodi ya Pamba kama imeweza kuwasaidia wananchi wake kupata soko wakati wa matatizo ya soko ni bodi nzuri. Kama soko limepatikana tu kwa sababu ya nguvu ya soko yaani mahitaji ya pamba ni makubwa duniani na hivyo kupelekea bei kuwa juu bodi haihitaji kusifiwa sana
 
Back
Top Bottom