SoC03 Bodi ya Mikopo (HESLB) Tanzania

Stories of Change - 2023 Competition

Yvo

New Member
May 8, 2023
2
7
Bodi ya mikopo ya elimu ya juu (Higher Education Students' Loans Board) Tanzania ilianzishwa mwaka 2005 na Rais wa tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt.Benjamini William Mkapa chini ya Wizara ya elimu yenye jukumu la kutoa mikopo Kwa wanafunzi wa elimu ya juu kuanzia shahada ya kwanza Kwa vigezo maalumu vilivyowekwa ,Mkopo inatolewa katika sehemu ya malipo ya ada, kujikimu, mafunzo Kwa vitendo, viandikwa na taaluma maalumu.
Screenshot_20230511-135207_1.jpg

Chanzo ;(Bodi ya Mikopo)

Njia za kuimarisha utawala bora katika bodi ya mikopo.

Kutoa mkopo Kwa kuzingatia vigezo walivyoviweka. Bodi ina vigezo maalum ili Mwanafunzi apate mkopo mfano kiwango cha ufaulu,Uhitaji wa mkopo(Yatima, TASAF,Ulemavu ).Vigezo hivi mda mwingine havifwati bali kunakuwa na udanganyifu unaopelekea upendeleo Kwa baadhi ya wanafunzi wasio na vigezo hii ni kutokana na ukilitimba unaofanywa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu.Hivyo teknolojia itumike katika uchakataji wa upataji wa mikopo.

Uwepo wa ofisi zote Mahali pamoja zinazohusika na Mikopo.Taasisi kama RITA, Mahakama,Posta,NIDA.Hii itasaidia kuokoa muda na ukamilishwaji wa nyaraka Kwa ufanisi Kwa waombaji. Mfano kuongeza ofisi katika wilaya zote tofauti na sasa ambapo zipo katika ngazi ya mkoa tu.Hii itaongeza uwajibikaji na ufanisi na kupelekea utawala bora.

Kuondoa vipaumbele vya Utoaji wa mikopo katika baadhi ya taaluma. Bodi iondoe kigezo hichi cha kutoa kipaumbele Cha mkopo kwa wanafunzi Waliosoma masomo ya Sayansi tu mfano udaktari, uhandisi,mfano katika"SAMIA SCHOLARSHIPS" ilivyofanya bali ifikirie na masomo ya sanaa mfano,habari,ualimu wa sanaa,utawala,utalii, tafsiri na ukalimami,kwa sababu wengi waliokosa mkopo ni masikini.Hii italeta usawa Kwa wote.

"SAMIA SCHOLARSHIP" ya Mwaka 2022/2023 iboreshwe mwaka huu wa masomo 2023/2024. Miongoni mwa vigezo ni kutoa ufadhili Kwa tahasusi za Sayansi tu, Kama vile (PCB, PCM, PGM, CBG, PMC's) Kwa wavulana wenye daraja la kwanza alama 3-5 na wasichana alama 3-6 ambapo waliopata hizo alama hizo mwaka 2022 matokeo ya kidato Cha Sita ni wanafunzi toka shule za watu binafsi wenye uwezo wa kumudu gharama za chuo na mkopo kwao sio kipaumbele. wachache Sana ni Toka shule za serikali.Hivyo basi serikali ione wajibu na Kwa tahasusi za sanaa waliofanya vizuri ili kuleta usawa Kwa wote.
1683805287903.jpg

Chanzo:Wizara ya elimu,Sayansi na teknolojia

Kutoa Fedha za mafunzo Kwa vitendo Kwa wanafunzi wote.Baadhi ya taaluma taaluma wanapata fedha za mafunzo kwa vitendo na wengine kuachwa wakati mwaka wa kwanza wa masomo wanahitajika kwenda kufanya mafunzo Kwa vitndeo mfano wa taaluma ni shahada ya sanaa katika elimu. Hivyo hupata ugumu wakati ukifika wa kwenda kufanya mafunzo Kwa vitendo katika shule za msingi na Sekondari hivyo bodi iwajibike Kwa hilo.

Kuimarisha mifumo ya TEHEMA na Kanzi data.Ili kuongeza ufanisi na ubora katika Utoaji wa mikopo mfano Kanzi data iunganishe Mifumo ya Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) na la Ufundi, Tume ya Vyuo vikuu Tanzania(T.C.U),Posta, RITA, NIDA ili iokoe muda wa umalizikaji wa nyaraka Kwa Kipindi kifupi,Pia Mifumo mda mwingi imekua inasumbua Kwa kutikisika hivyo taarifa kuvurugika, mfano wanufaika wa mikopo kutokupata fedha Kwa wakati , kupata fedha zaidi au pungufu ya kiwango alichopangiwa.Hii itasaidia kupunguza upotevu wa Kwa bodi fedha wakati wa kutoa mikopo.

Kutoa elimu Kwa wanafunzi na Jamii .Elimu inatakiwa itolewe Kwa wanafunzi Kipindi wakiwa shuleni (Kwa kidato Cha Sita) na vyuo vya kati kabla hawajamaliza ili kuandaa mapema mahitaji na nyaraka kabla ya dirisha la mikopo kufunguliwa, mfano cheti cha kuzaliwa, vifo ,namba ya nida,barua ya udhamini wa masomo,uthibitisho wa daktari kutokana na ulemavu,gharama za ada kwenda bodi,muhuri wa wakili,steshenari hii itasaidia kujiandaa mapema tofauti na sasa ambapo elimu inatolewa kidogo mfano katika makambi ya J.K.T Kipindi cha wahitimu wa kidato cha Sita na ualimu wakiwa makambini Kwa mujibu wa Sheria ambapo si wote wanahudhuria .Hii ikifanyika italeta uwajibikaji na Kuongezeka kwa utawala bora.

Kiujumla haya yakifanyika Kwa weredi wa hali ya juu basi itafanya bodi ya mikopo kuwa na uwezo wa kutoa mikopo Kwa wanafunzi Kwa usawa,haki na kuondoa sintofahamu katika jamii.Pia italeta chachu ya wanafunzi kusoma na kuondoa mzigo Kwa wazazi au walezi juu ya gharama na hivo kuongeza kiwango cha elimu na wataalamu wenye tija katika jamii ya Tanzania.
 
Bodi ya mikopo Elimu ya juu (Higher Education Students Loans Board) nchini Tanzania iliyoanzishwa mwaka 2007 kama maono ya Rais wa tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt.Benjamini William Mkapa iliyochini ya Wizara ya elimu pamoja na usaidizi wa Wizara ya Fedha lenye jukumu la kutoa mikopo Kwa wanafunzi wa elimu ya juu yaani kuanzia shahada ya kwanza/digrii Kwa vigezo maalumu vilivyowekwa ,Mkopo inatolewa katika sehemu ya hela ya ada, hela ya kujikimu, hela ya mafunzo Kwa vitendo, hela ya viandikwa na ela ya programu maalumu.

Mambo haya yakifanyika katika bodi ya mikopo basi italeta utawala bora nchini Tanzania;

Kutoa mkopo Kwa kuzingatia vigezo walivyoviweka. Bodi ina vigezo mbalimbali ili Mwanafunzi apate mkopo kama vile kiwango cha ufaulu,Uhitaji mfano mwanafunzi aliyesomeshwa kwa udhamini wa shule,taasisi, yatima , aliye katik mfuko wa TASAF,mlemavu ambapo vigezo hivi mda mwingine havifwati bali kunakuwa na udanganyifu unaopelekea upendeleo Kwa baadhi ya wanafunzi wasio na vigezo hii ni kutokana na ukilitimba unaifanywa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu katika bodi ya mikopo. Hivyobasi ,teknolojia inatakiwa itumike katika uchakataji wa upataji wa mikopo.

Uwepo wa ofisi zote Mahali pamoja zinazosaidia taratibu zote za uombaji wa mikopo . Taasisi kama RITA, Mahakama( mawakili /mahakimu), Posta ,NIDA, ,hii itasaidia uokoaji wa muda na ukamilishwaji wa nyaraka Kwa ufanisi Kwa waombaji. Hivyo kuwepo na ofisi inayounganisha taasisi zote sehemu moja Kwa Kila wilaya au mkoa, tofauti na sasa ambapo hupatikana katika ngazi ya mkoa tu.Pia hata makao Makuu bado yapo Dar es salaam na Makao Makuu madogo Dodoma ambapo ikitokea shida kubwa mwombaji huitajika kwenda makao Makuu.

Kuondoa vipaumbele vya Utoaji wa mikopo katika baadhi ya program/taaluma hasahasa za kisayansi. Bodi iondoe kigezo hichi cha kutoa kipaumbele Kwa wanafunzi Waliosoma masomo ya Sayansi tu kama udaktari ,utabibu ,ufamasia, uhandisi,kama vile."Samia scholarship" ilivyofanya bali iwafikirie na wanaochukua masomo ya sanaa kama vile uandishi wa habari, ualimu wa sanaa,utawala, utalii,tafsiri na ukalimami, maendeleo ya jamii kwasababu wengi wameachwa majumbani bila ya kupata mkopo ambao ndio masikini..Hii italeta usawa Kwa wote na hivo kuleta maendeleo katika nchi yetu.

Samia scholarship ya Mwaka 2022/2023 iboreshwe mwaka huu wa masomo 2023/2024. Miongoni mwa vigezo ni kutoa ufadhili Kwa tahasusi za Sayansi tu, Kama vile (PCB, PCM, PGM, CBG, PMCs) Kwa wavulana wenye daraja la kwanza alama 3-5 na wasichana kuanzia alama 3-6 ambapo waliopata hizo alama wengi Kwa matokeo ya Advanced 2022 ni wanafunzi toka shule za watu binafsi na wachache Sana shule za serikali. Ambamo wengi wao ni watoto toka katika familia tajiri amabo mkopo kwao sio kipaumbele chao Kwa sababu wanaweza kukidhi gharama za vyuo vikuu,hivyo basi serikali ione wajibu na Kwa tahasusi za sanaa waliofanya vizuri hii italeta usawa Kwa wote.

Kutoa Fedha za mafunzo Kwa vitendo (Field practice) Kwa wanafunzi wote .Zipo baadhi ya programun wanapata Fedha za mafunzo kwa vitendo ma baadhi kuachwa wakati mwaka wa kwanza wa masomo wanahitaji waende kufanya mafunzo Kwa vitndeo mfano programu ya shahada ya sanaa katika elimu (Bachelor of Arts with Education BA-ed, au Bachelor of Arts in Education BEd) ,Kutopewa Kwa hela kwao kunawafanya kupata ugumu wakati ukifika wa kwenda kufanaya mafunzo Kwa vitendo katika shule za msingi, Sekondari na vyuo vya kati na taasisi mbalimbali na hivo kutofanya vizuri.

Kuimarisha mifumo ya TEHEMA na Kanzi data .Mifumo ya bodi mfano TEHAMA iboreshwe ili kuongeza ufanisi na ubora katika Utoaji wa mikopo mfano Kanzi data iunganishe Mifumo ya Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) na la Ufundi (NACTEVET), Tume ya Vyuo vikuu Tanzania(TCU),Posta, RITA, NIDA ili iokoe muda wa umalizikaji wa nyaraka Kwa Kipindi kifupi,Pia Mifumo mdanmwingi imekua inasumbua Kwa ku-sheki/kutikisika hivyo taarifa kuvurugika mfano wanufaika wa mikopo kutokupata fedha Kwa wakati , kupata fedha zaidi au pungufu ya kiwango alichopangiwa.Hii itasaidia kupunguza upotevu wa fedha wakati wa kutoa mikopo na kupokea madeni toka Kwa wanufaika.

Kutoa elimu Kwa wanafunzi na Jamii .Elimu inatakiwa itolewe Kwa wanafunzi Kipindi wakiwa shuleni (Kwa kidato Cha Sita) kabla hawajamaliza au Kwa wanafunzi wa diploma wakiwa vyuo vya kati ili kuweza kujua nini anatakiwa kufanya Baada ya dirisha la mikopo kufunguliwa mfano kuandaa nyaraka mbalimbali kama cheti Cha kuzaliwa, namba ya nida, uthibitisho wa cheti cha kuzaliwa ,cheti cha vifo vya wazazi au walezi Toka RITA, barua ya udhamini wa masomo toka shuleni au chuo cha kati.Uthibitisho wa daktari kutokana na ulemavi.Pia Kwa upande mwingine kujua gharama za ada kwenda bodi, mhuri wa wakili, gharama za steshenari hii itasaidia wanafunzi na Jamii/wazazi kujiandaa mapema tofauti na sasa ambapo elimu inatolewa kidogo mfano katika makambi ya JKT Kipindi cha wahitimu wa kidato cha Sita wakiwa makambini Kwa mujibu wa Sheria ambapo si wote wanahudhuria .Hii ikifanyika italeta uwajibikaji na Kuongezeka kwa utawala bora.

Yote hayo yakifanyika Kwa weredi wa hali ya juu basi itafanya bodi ya mikopo (HESLB)) kuwa na uwezo wa kutoa mikopo Kwa wanafunzi Kwa usawa na kuepuka lawama za hapa na pale katika Jamii. Pia itawafanya wanafunzi wengi kusoma Kwa bidii bila ya kuwaza kwamba atapata wapi fedha ya kumalizia ada, fedha ya mafunzo kwa vitendo, fedha ya viandikwa na hivo kuapatikana Kwa wataalamu wenye tija katika jamii ya Tanzania.
 
Yeah , Nimekuelewa vizuri sana , Kaka Hongera kwa Kuweza toa mchango wa kimawazo Juu ya Umma , Nina amini kama serikal Italichukua swala hili katika hali ya uzito Kwa sababu wapo wananfunzi wanasitisha masomo kwa kukosa mkopo kwa sababu ya Hali ya kimaisha , Na hivyo upelekea Wanaweza nufaika asilimia kubwa ni wale wasio na uhitaji ambao ni matajiri , hivyobasi serikal ichunguze jambo hili kwa kina zaidi , ili kupunguza wimbi la Vijana walio na malengo kufikia ndoto zao na baadaye kukwamishwa kwa sababu ya kukosa hela ya kujikim chuoni(boom)na Ada (school fees).
 
Suala lina wezekana Kikubwa Ni utekelezaji Wahali ya juu ili kufikia malengo Ya kila Mweny Uhitaji kupata hitaji lake na kuendelea mbele kufikia malengo yake katika Elimu
 
  • Thanks
Reactions: Yvo
Bodi ya mikopo ya elimu ya juu (Higher Education Students' Loans Board) Tanzania ilianzishwa mwaka 2005 na Rais wa tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt.Benjamini William Mkapa chini ya Wizara ya elimu yenye jukumu la kutoa mikopo Kwa wanafunzi wa elimu ya juu kuanzia shahada ya kwanza Kwa vigezo maalumu vilivyowekwa ,Mkopo inatolewa katika sehemu ya hela ya ada, kujikimu, mafunzo Kwa vitendo, viandikwa na programu maalumu.
View attachment 2617815
Chanzo ;(Bodi ya Mikopo)

Njia za kuimarisha utawala bora katika bodi ya mikopo.

Kutoa mkopo Kwa kuzingatia vigezo walivyoviweka. Bodi ina vigezo maalum ili Mwanafunzi apate mkopo mfano kiwango cha ufaulu,Uhitaji wa mkopo(Yatima, TASAF,Ulemavu ).Vigezo hivi mda mwingine havifwati bali kunakuwa na udanganyifu unaopelekea upendeleo Kwa baadhi ya wanafunzi wasio na vigezo hii ni kutokana na ukilitimba unaofanywa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu.Hivyo teknolojia itumike katika uchakataji wa upataji wa mikopo.

Uwepo wa ofisi zote Mahali pamoja zinazohusika na Mikopo.Taasisi kama RITA, Mahakama,Posta,NIDA.Hii itasaidia kuokoa muda na ukamilishwaji wa nyaraka Kwa ufanisi Kwa waombaji. Mfano kuongeza ofisi katika wilaya zote tofauti na sasa ambapo zipo katika ngazi ya mkoa tu.Hii itaongeza uwajibikaji na ufanisi na kupelekea utawala bora.

Kuondoa vipaumbele vya Utoaji wa mikopo katika baadhi ya taaluma. Bodi iondoe kigezo hichi cha kutoa kipaumbele Cha mkopo kwa wanafunzi Waliosoma masomo ya Sayansi tu mfano udaktari, uhandisi,mfano katika"SAMIA SCHOLARSHIPS" ilivyofanya bali ifikirie na masomo ya sanaa mfano,habari,ualimu wa sanaa,utawala,utalii, tafsiri na ukalimami,kwa sababu wengi waliokosa mkopo ni masikini.Hii italeta usawa Kwa wote.

"SAMIA SCHOLARSHIP" ya Mwaka 2022/2023 iboreshwe mwaka huu wa masomo 2023/2024. Miongoni mwa vigezo ni kutoa ufadhili Kwa tahasusi za Sayansi tu, Kama vile (PCB, PCM, PGM, CBG, PMC's) Kwa wavulana wenye daraja la kwanza alama 3-5 na wasichana alama 3-6 ambapo waliopata hizo alama hizo mwaka 2022 matokeo ya kidato Cha Sita ni wanafunzi toka shule za watu binafsi wenye uwezo wa kumudu gharama za chuo na mkopo kwao sio kipaumbele. wachache Sana ni Toka shule za serikali.Hivyo basi serikali ione wajibu na Kwa tahasusi za sanaa waliofanya vizuri ili kuleta usawa Kwa wote.
View attachment 2617867
Chanzo:(Wizara ya elimu ,Sayansi na teknolojia)

Kutoa Fedha za mafunzo Kwa vitendo Kwa wanafunzi wote.Baadhi ya taaluma taaluma wanapata fedha za mafunzo kwa vitendo na wengine kuachwa wakati mwaka wa kwanza wa masomo wanahitajika kwenda kufanya mafunzo Kwa vitndeo mfano wa taaluma ni shahada ya sanaa katika elimu. Hivyo hupata ugumu wakati ukifika wa kwenda kufanya mafunzo Kwa vitendo katika shule za msingi na Sekondari hivyo bodi iwajibike Kwa hilo.

Kuimarisha mifumo ya TEHEMA na Kanzi data.Ili kuongeza ufanisi na ubora katika Utoaji wa mikopo mfano Kanzi data iunganishe Mifumo ya Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) na la Ufundi, Tume ya Vyuo vikuu Tanzania(T.C.U),Posta, RITA, NIDA ili iokoe muda wa umalizikaji wa nyaraka Kwa Kipindi kifupi,Pia Mifumo mda mwingi imekua inasumbua Kwa kutikisika hivyo taarifa kuvurugika, mfano wanufaika wa mikopo kutokupata fedha Kwa wakati , kupata fedha zaidi au pungufu ya kiwango alichopangiwa.Hii itasaidia kupunguza upotevu wa Kwa bodi fedha wakati wa kutoa mikopo.

Kutoa elimu Kwa wanafunzi na Jamii .Elimu inatakiwa itolewe Kwa wanafunzi Kipindi wakiwa shuleni (Kwa kidato Cha Sita) na vyuo vya kati kabla hawajamaliza ili kuandaa mapema mahitaji na nyaraka kabla ya dirisha la mikopo kufunguliwa, mfano cheti cha kuzaliwa, vifo ,namba ya nida,barua ya udhamini wa masomo,uthibitisho wa daktari kutokana na ulemavu,gharama za ada kwenda bodi,muhuri wa wakili,steshenari hii itasaidia kujiandaa mapema tofauti na sasa ambapo elimu inatolewa kidogo mfano katika makambi ya J.K.T Kipindi cha wahitimu wa kidato cha Sita na ualimu wakiwa makambini Kwa mujibu wa Sheria ambapo si wote wanahudhuria .Hii ikifanyika italeta uwajibikaji na Kuongezeka kwa utawala bora.

Kiujumla haya yakifanyika Kwa weredi wa hali ya juu basi itafanya bodi ya mikopo kuwa na uwezo wa kutoa mikopo Kwa wanafunzi Kwa usawa,haki na kuondoa sintofahamu katika jamii.Pia italeta chachu ya wanafunzi kusoma na kuondoa mzigo Kwa wazazi au walezi juu ya gharama na hivo kuongeza kiwango cha elimu na wataalamu wenye tija katika jamii ya Tanzania.
Bodi ya mikopo ya elimu ya juu inabidi kuhakikisha usawa kwa wote ili malengo ya watu yatimie
 
  • Thanks
Reactions: Yvo
Back
Top Bottom