Bloggers waendeleza kejeli kwa Rais Kikwete

Habarindiyohiyo

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
263
13
Kumezuka tabia ya bloggers wa kitanzania kuendeleza kejeli kwa Rais Kikwete kwa kutumia lugha kali kali ambazo pia zinaleta uchochezi. Kati ya Bloggers washabikia tabia hii yupo Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua, yupo pia huyu JJ. Watu hawa wanashindwa kutofautisha kati ya ukosoaji na udhalilishaji wa hadhi ya Rais aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya watanzania wote. Mamlaka zinazohusika lazima zichukue hatua kukemea hali hii. Kama kuna blogger mwingine mwenye tabia hii atajwe pia hapa ili aweze kufahamika.Bloggers watambue kwamba wanaweza kuhukumiwa kwa maneno yao wanayoandika andika. Kama tunaweza kuikemea theutamu kwanini tuache kuwakemea hawa?

............ndiyohiyo
 
Please he deserves all the ridicule people can throw at him. he is beyond receiving any logical advice now.
 
Kumezuka tabia ya bloggers wa kitanzania kuendeleza kejeli kwa Rais Kikwete kwa kutumia lugha kali kali ambazo pia zinaleta uchochezi. Kati ya Bloggers washabikia tabia hii yupo Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua, yupo pia huyu JJ. Watu hawa wanashindwa kutofautisha kati ya ukosoaji na udhalilishaji wa hadhi ya Rais aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya watanzania wote. Mamlaka zinazohusika lazima zichukue hatua kukemea hali hii. Kama kuna blogger mwingine mwenye tabia hii atajwe pia hapa ili aweze kufahamika.Bloggers watambue kwamba wanaweza kuhukumiwa kwa maneno yao wanayoandika andika. Kama tunaweza kuikemea theutamu kwanini tuache kuwakemea hawa?

............ndiyohiyo

ni yupo anayekejeli wenzie? anayesema au anayetenda bila kusema?

Na Kikwete hakuchaguliwa kwa asilimia "80 ya Watanzania wote"; ingekuwa hivyo angetamba.
 
Yeye KIKWETE ndo anaukejeli URAIS. the person is a big let down and an embarassment to our country.

Sijui alisoma nini? Umewahi kuona wapi Rais anakuwa WAKILI wa WEZI? The EPA fraudsters are happy that this guy is the president. I can believe this country.
 
Last edited by a moderator:
Imean, ICANT BELIEVE THIS COUNTRY kwa kweli. Kuna Rais ambaye anatetea wahujumu nchi. Yeye ndo msemaji na mtetezi wao namba moja, na anafanya hivyo bila soni mtoto wa kiume wa Kikwere!!
 
Last edited by a moderator:
Kumezuka tabia ya bloggers wa kitanzania kuendeleza kejeli kwa Rais Kikwete kwa kutumia lugha kali kali ambazo pia zinaleta uchochezi. Kati ya Bloggers washabikia tabia hii yupo Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua, yupo pia huyu JJ. Watu hawa wanashindwa kutofautisha kati ya ukosoaji na udhalilishaji wa hadhi ya Rais aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya watanzania wote. Mamlaka zinazohusika lazima zichukue hatua kukemea hali hii. Kama kuna blogger mwingine mwenye tabia hii atajwe pia hapa ili aweze kufahamika.Bloggers watambue kwamba wanaweza kuhukumiwa kwa maneno yao wanayoandika andika. Kama tunaweza kuikemea theutamu kwanini tuache kuwakemea hawa?

............ndiyohiyo

...watu huwa hawalazimishiwi kumuheshimu mtu.....wala huwezi kutumia ushindi wa kishindo wa asilimia 80% wa mwaka 2005..kuhalalisha heshima..heshima ya rais ni ile ile hata kama alipata asilimia 51%..that is the office...kinachofuata baada ya ushindi ni kazi.....na kwa hali ilivyo perfomance ya rais kwa sisi is A RECORD LOW....then do you expect watu waliomuamini to come low beggin.........waache wamrushie mayai viza ...hiyo ndio due anayostahili.....na kwa sisi watanzania hatuna hiyana akijirekebisha na kutuongoza vema na maendeleo yakaonekana ,,..tutakuwa wa kwanza kumsifu......kwanza kwa rais huyu ana bahati watu wamemvumilia sana..wakitegemea mabadiliko..ni MR.POLITICIAN...!
 
ni yupo anayekejeli wenzie? Anayesema au anayetenda bila kusema?

Na kikwete hakuchaguliwa kwa asilimia "80 ya watanzania wote"; ingekuwa hivyo angetamba.


true mmj ..i am really irked by people who still refer to 80% landslide victory as an excuse to challange this poor looser....wakati inajulikana ushindi huo ulitokana na rushwa kuanzia kwenye media hadi kwa wananchi ...na zawadi zawadi...kwa kutumia yale mabilioni ya epa ..hata angeshinda kwa asilimia 90% tusingeshangaa....kwani ni kielelezo cha umaskini wetu!!
 
Kumezuka tabia ya bloggers wa kitanzania kuendeleza kejeli kwa Rais Kikwete kwa kutumia lugha kali kali ambazo pia zinaleta uchochezi. Kati ya Bloggers washabikia tabia hii yupo Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua, yupo pia huyu JJ. Watu hawa wanashindwa kutofautisha kati ya ukosoaji na udhalilishaji wa hadhi ya Rais aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya watanzania wote. Mamlaka zinazohusika lazima zichukue hatua kukemea hali hii. Kama kuna blogger mwingine mwenye tabia hii atajwe pia hapa ili aweze kufahamika.Bloggers watambue kwamba wanaweza kuhukumiwa kwa maneno yao wanayoandika andika. Kama tunaweza kuikemea theutamu kwanini tuache kuwakemea hawa?

............ndiyohiyo

Ebu kawasemee kwa Mkuchika awafungie
 
Kumezuka tabia ya bloggers wa kitanzania kuendeleza kejeli kwa Rais Kikwete kwa kutumia lugha kali kali ambazo pia zinaleta uchochezi. Kati ya Bloggers washabikia tabia hii yupo Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua, yupo pia huyu JJ. Watu hawa wanashindwa kutofautisha kati ya ukosoaji na udhalilishaji wa hadhi ya Rais aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya watanzania wote. Mamlaka zinazohusika lazima zichukue hatua kukemea hali hii. Kama kuna blogger mwingine mwenye tabia hii atajwe pia hapa ili aweze kufahamika.Bloggers watambue kwamba wanaweza kuhukumiwa kwa maneno yao wanayoandika andika. Kama tunaweza kuikemea theutamu kwanini tuache kuwakemea hawa?

............ndiyohiyo

Hebu tuonyeshe wapi wamevunja sheria watu hawa, nilichosoma kwenye blogu ya Ansbert Ngurumo ni:
NILIWAHI kuandika habari za kiongozi mmoja wa juu wa CCM ambaye alikifananisha chama chake na puto lililojaa pumzi; kwamba sasa linakaribia kupasuka.

Alikifananisha pia na himaya ya Kirumi iliyodumu na kutamba kwa karne kadhaa, lakini hatimaye ikaangushwa na wapambe wa Kaizari.

Wiki hii, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Shariff Hamad, amesema nchi imevimba, inakaribia kupasuka. Ana ujumbe ule ule, mzito kwa watawala.

Nina hakika kwamba watawala wanayaona na kuyasikia yanayotokea sasa nchini; na wanajua chanzo chake – kiburi na jeuri yao! Naamini hakuna kiongozi yeyote wa serikali atakayesimama na kutamka hadharani, walau kwa sasa, kwamba Tanzania ni nchi ya amani. Amani haipo tena!

Sina shaka pia kwamba viongozi hawa watakiri, walau kwa mara ya kwanza, kwamba ‘upendo’ wa wananchi kwa serikali ya awamu ya nne umekwisha.

Kama hawataki kukiri ukweli huu (kwamba amani imetoweka na kwamba wananchi wameichoka serikali), basi wakubali kuendelea kupigwa mawe na wananchi kwa visingizio mbalimbali.

Naamini pia kwamba wakati mapambano ya walimu yanaendelea, zamu ya polisi na wauguzi inakaribia, maana wote hawa wamo katika kundi la watumishi wa umma wanaonyonywa, wanaodharauliwa na kupuuzwa na serikali ile ile kwa muda mrefu.

Kwa bahati mbaya, makundi haya, hasa walimu na polisi wamekuwa wakitumiwa na serikali (na CCM) kuendekeza na kupalilia unyonyaji huu – hasa wakati wa uchaguzi.

Matokeo ya ushabiki wa polisi na walimu kwa CCM – kwa visingizio vya nidhamu ya utumishi na posho za kuwadhalilisha – ni sehemu ya tatizo lililowafikisha hapo walipo; wao na jamii nzima.

Kwa sababu serikali imezoea kuwatumia wakatumika, imewafanya wao kuwa sehemu ya vyombo vyao vya kunyanyasia wananchi. Serikali inasahu kwamba polisi na walimu ni dada, kaka, baba, mama, wajomba na shangazi zetu. Wana mahitaji yale yale kama wananchi wengine; na wanastahili heshima na haki zile zile wanazopewa watumishi wengine wanaolipwa manono.

Imewachukua muda mrefu sana walimu kutambua nafasi yao katika jamii na kutetea haki zao. Kwa taaluma yao, walimu ndio walipaswa kuisaidia jamii kujitambua, kujitetea na kujikwamua.

Walimu wanapaswa kuwa werevu, na wana jukumu la kuendelea kutufundisha kuhusu misingi na mbinu za kujinasua katika manyanyaso ya serikali. Wao ni wanyanyasika kama sisi. Wanachofanya sasa, ni sehemu ndogo ya elimu ya uraia kwa vitendo.

Naamini kwamba baada ya mapambano haya ya walimu na serikali, kama walimu hawatanywea na kujikomba tena kwa mwajiri asiyejali maslahi yao, heshima ya walimu itapanda, na maslahi yao yataongezeka; na hawatakubai tena kuwa vibaraka wa mafisadi.

Kwa jinsi tunavyojua uvumilivu na uungwana nwa walimu wetu, kama wamefikia mahali pa kumshambuliwa rais wao kwa mawe, viti na chupa za maji (kwa kauli yake ya kuahirisha mgomo wao) ni ishara kwamba serikali imewamefikisha pabaya.

Watanzania hawatawalaumu walimu, bali serikali iliyowafikisha hapo. Na sasa ujasiri wa walimu hao umeigwa na wazee wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyovunjika 1977, ambao kama ilivyo kwa walimu, nao wamechoshwa na unyanyasaji wa serikali.

Wiki hii wamekusanyika mbele ya Wizara ya Fedha kudai haki zao, wakazuia magari kuingia na kutoka wizarani; serikali ikawaitia polisi ambao waliamua kutumia nguvu kuingiza magari hayo. Lakini wazee wakaamua kuyadhibiti kwa kupasua kioo cha gari mojawapo.

Polisi walikosea. Harakati za wazee hawa si fujo kwa mtu yeyote. Wanatafuta haki yao, na wanawatetea hata polisi wenyewe; maana yawezekana baadhi yao wana watoto ambao ni askari.

Na adha ya askari wa Tanzania inafahamika. Leo ni wazee hawa, kesho ni wao. Na hao wanaowatuma polisi kupiga wazee, ndio watakaokuwa wanawatumia polisi wengine kesho kuwapiga polisi wastaafu.

Na kama polisi nao wangejitambua mapema, wangeibana serikali vilivyo iboreshe maslahi yao sasa kabla vuguvugu la walimu, wanafunzi, wastaafu na watumishi wengine wa umma halijapoa.

Polisi wetu wasiishie kutii amri za kutembeza vipigo kwa wazazi wao; wanapaswa wawe sehemu ya harakati za kuikomboa jamii. Serikali imezoea kutumia polisi kupambana na nguvu za vijana; na mara kadhaa wamefanikiwa kuwaumiza kaka na dada zao kwa ajili ya kulinda utii wao kwa mafisadi.

Lakini funzo walilolipata Tarime linapaswa kuwaamsha na kuwajenga upya polisi wetu. Wajue kuwa wananchi sasa wameamka. Wako tayari kupambana na nguvu zozote za giza zinazotumiwa na serikali.

Kwamba mamia ya askari waliopelekwa Tarime kudhibiti wapinzani kwa kisingizo cha kulinda amani wameshindwa kufurukuta, ni ishara kwamba umma ukiamua, jiwe la haki linaweza kuwa na nguvu kuliko risasi ya dhuluma.

Katika wiki hii hii, tumesikia pia habari za msafara za Rais Jakaya Kikwete kushambuliwa kwa mawe mkoani Mbeya. Ni habari za kusikitisha. Binafsi, sina kumbukumbu ya msafara wa rais kushambuliwa na wananchi. Lakini naamini serikali itatumia akili katika kulichunguza tukio hili, na kudhibiti mengine kama hayo siku zijazo.

Wananchi hawa si vichaa. Hata sababu zilizotolewa na serikali kwamba wananchi walishambulia msafara wa rais kwa kuwa walikuwa na kiu ya kumuona lakini hakusimama kijijini kwao kwa sababu ya giza, hazieleweki kwa watu wenye kupenda kufikiri na kutafakati kidogo.

Wananchi wanaompenda kiongozi wao hawamrushii mawe kumdhuru yeye au watu walioambatana naye. Najua serikali yenyewe haiamini kauli yake, ndiyo maana imemwaga mashushushu mahali hapo kuchunguza sababu za kitendo hicho.

Hata hivyo, tunapaswa kujiuliza. Kwanini sasa wananchi wanaonekana kushabikia urushaji mawe? Huu ndio ukomo wa uvumilivu wao wa siku nyingi? Ndiyo njia mpya ya kujieleza kwamba wamechoka kupuuzwa?

Ndiyo njia ya kuwafanya wakubwa wawasikilize? Je, baada ya mawe watatumia silaha gani? Je, wakubwa wapo tayari kujifunza kutokana na mawe wanayorushiwa na wananchi? Au wataendelea kuwatuma polisi warushe risasi kudhibiti mawe hayo? Je, watafanikiwa?

Baada ya matukio ya Tarime, mgomo wa walimu, wastaafu wa Afrika mashariki na fujo za wananchi Mbeya dhidi ya msafara wa rais, serikali imepata ujumbe?

Maana inawezekana wakubwa wanaendelea kujidanganya kwa kauli kama zilizotolewa wiki iliyopita na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu, alipokuwa akilishutumu gazeti la MwanaHALISI kwa habari za kundi la wana-CCM wanaotaka kumwondoa Rais Jakaya Kikwete mwaka 2010.

Alisema: “Unamng’oa vipi rais ambaye utendaji wake wa kazi umeleta mafanikio makubwa kwa wananchi na umekuwa mfano wa kuigwa mbele ya mataifa mengine? ‘Hakuna tishio lolote, hakuna njama zozote za kumng’oa rais madarakani, iwe ni leo au mwaka 2010, kama gazeti hilo lilivyodai... kama kungekuwa na njama hizo mtu wa kwanza kujua angekuwa ni rais mwenyewe, kwani rais ana vyombo vya ulinzi na usalama.”

Ndiyo! Vyombo hivyo vya ulinzi na usalama (wa rais) vinaweza kugeuka leo na kuwa vyombo vya ulinzi na usalama wa wananchi. Havitalinda uozo wa watawala, bali vitawasaidia wananchi kuondokana na tatizo. Na hata kama vyombo hivyo vinahakikisha kwamba rais yuko salama - kama Rweyemamu alivyosema - haina maana kwamba usalama wake ni kukaa madarakani.

Ukweli ni kwamba wanaotaka kumwondolea rais mzigo wa uongozi wanampenda, na wanaijali nchi yao. Lakini ukweli ni kwamba kauli ya serikali kupitia kwa Rweyemamu inaonyesha upofu wa watawala; au ni mkakati wa makusudi wa kupotosha ukweli katika mazingira magumu.

Tuulizane. Ni kweli kwamba uongozi wa Rais Kikwete umeleta mafanikio makubwa kwa wananchi?

Mwaka jana mwishoni, ripoti ya Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia (REDET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilisema kwamba imani ya Watanzania kwa serikali ya awamu ya nne imeshuka mno.

Umaarufu wa Rais Kikwete ulikuwa ameshuka kwa asilimia 23. Hiyo ni baada ya miaka miwili tu ya utawala wake. Kati ya Desemba mwaka jana na sasa, hakuna la maana ambalo serikali yake imelifanya kurejesha imani ya wananchi.

Kwa mtazamo wa jumla, serikali imekwama; uchumi umedorora; maisha ya wananchi yamezidi kuwa magumu kutokana na kupanda kwa gharama za maisha; na ufisadi umekuwa sifa mpya ya serikali ya Kikwete, na umekuwa kichocheo cha harakati mpya za wananchi dhidi ya serikali.

Nguvu kubwa iliyokuwa imewekezwa kwenye magazeti na vyombo vingine vya habari ili kuijenga serikali (hasa Kikwete binafsi) mbele ya umma, imepwaya kwa sababu maisha halisi ni magumu kuliko makala tamu tamu za wapenzi wa serikali na chama tawala.

Nguvu ya mashushu wanaojipendekeza kwa serikali imepwaya kwa sababu nao ni binadamu; wanafika mahali wanaona ukweli. Maisha magumu yanawaathiri wao na ndugu zao vile vile.

Pesa za wizi na halali zilizo mikononi mwa vyombo vya dola na chama tawala zina kikomo. Haziwezi kununua kila kitu. Walau hadi sasa, zimeshindwa kununua mapenzi ya wananchi kwa serikali.

Haziondoi chuki yao dhidi ya watawala walioahidi maisha bora ambayo hayajapatikana, na dalili hazionyeshi kama yatapatikana wakiwa madarakani.

Vitisho dhidi ya wakosoaji wa serikali havifajua dafu kwa sababu serikali haina nidhamu; mambo ya kukosoa yanaongezeka. Woga wa wananchi kwa watawala umepungua kwa kiasi kikubwa, na uelewa wao wa masuala ya kisiasa umeongezeka.

Propaganda za CCM na wapambe wake zimeshindwa kufanya kazi kwa sababu wananchi wa kizazi hiki ni waelewa kuliko wale waliokabidhiwa jukumu la kueneza propaganda za CCM. Matokeo yake, serikali haikubaliki kwa wananchi, na kizazi hiki kimeanza kujitambulisha zaidi na siasa zinazoitaka CCM ipumzike.

Ni kizazi kinachotaka, na kimedhamiria, kuona CCM ikiachia madaraka katika ngazi za halmshauri, bunge na serikali kuu. Na wanaoyaona haya si wapinzani tu. Hata ndani ya CCM wamo watu wenye akili nzuri, waliochoka siasa za maigizo, wanaotaka kuendana na siasa zinazoakisi hisia na matarajio ya wananchi.

Ushindani na kuchimbana miongoni mwao, vikichanganyika na kushindwa kwa serikali kuwapa wananchi matumaini, ndivyo vimechochea harakati za baadhi ya wana-CCM kuamua kuipindua serikali yao wenyewe.

Baadhi yao wanaona aibu kwamba chama kikubwa chenye mizizi mirefu, wanachama wengi na rasilimali nyingi; kinaongozwa na kikundi kidogo cha watu wachache walafi, na wenye uwezo mdogo sana wa kuelewa, kupembua, kuandaa na kusimamia mikakati makini ya kukikwamua chama na taifa.

Wanakerwa na mbwembwe na usanii unaotangulizwa katika uongozi wa chama na serikali. Wamefikia mahali hawaogopi tena kushindana na viongozi walio madarakani sasa.

Lakini si wao tu. Wapo pia wale waliokuwa na Rais Kikwete tangu awali, waliomwandalia kila kitu na kumsindikiza hadi Ikulu; waliotarajia kuvuna kwa ari, nguvu na kasi mpya na kuwekeza katika kipindi cha utawala wake.

Nao wanaona kwamba mwenzao amekwama, na ndiyo sababu hata wao wamekwama. Na wako tayari kujikwamua kwa gharama zote, hata ikibidi wamtose yeye.

Haya yote yanaonekana, yanasikika. Yanatokana na ukweli kwamba serikali imekwama, wadau wanatapatapa.

Yanaakisi kauli ya wananchi katika ripoti ya utafiti wa REDET kwamba sababu za wasioridhishwa na utendaji wa Rais Kikwete na asilimia zao zikiwa kwenye mabano, ni pamoja na kushindwa kwake kuboresha maisha kama alivyoahidi (asilimia 30.4), huku wengine wakidai kuwa ameshindwa kutimiza ahadi (asilimia 21.6), kutokufuatilia utekelezaji (asilimia 11.6), kuchagua viongozi wabovu (asilimia 9.1) na kushindwa kupambana na rushwa (asilimia 5.6).

Wananchi wanaona, wanasema; na hata watumishi serikalini wanaona; wanasema hivyo, na wanalaumiana. Kama wana-CCM wangekuwa na ujasiri kama tulioshuhudia mwezi uliopita nchini Afrika Kusini, wangekuwa wamepiga kura ya kutokuwa na imani na uongozi wao.

Lakini ukweli wa mambo ni kwamba, katika makundi yao mbalimbali, wana CCM wameshakubaliana kimya kimya kwamba wanahitaji uongozi mpya. Naamini na Watanzania wengine wanahitaji uongozi mpya kitaifa hata kabla ya 2010.

Labda hii ndiyo tafsiri ya harakati kurusha mawe zinazojionyesha sasa katika makundi mbalimbali ya jamii. Wananchi wamechoka; watawala wanaendelea kudhani wanapendwa. Hawana habari; wamekwisha.

ansbertn@yahoo.com +447885850425 Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua



Na nilishokisoma kwenye Blogu ya John Mnyika ni:

Rais Kikwete: mene mene na tekel; taifa linagawanyika

Ni saa sita na ushee usiku. Siku mpya imeanza, ni Novemba Mosi; ni siku ya vijana Afrika. Najaribu kutafakari maudhui ya siku hii ya pekee kwa vijana Afrika kama ilivyopitishwa na umoja wa Afrika. Natafakari ujumbe wa mwaka huu “Maadili chanya ya kiafrika, amani na mshikamano”. Tafakari yangu inanirudisha nyuma katika hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa umoja wa Afrika aliyoitoa usiku wa Oktoba 31 mwaka 2008. Mwangi wa maneno ya Rais wa nchi yangu unarindima katika kichwa changu na kunikosesha usingizi. Si kwa uzito wa maneno bali kwa hofu yangu juu ya madhara ya wepesi wa maneno yenyewe kwa mwelekeo wa taifa.

Nagutuka; nagundua natafakari ubatili, najihisi kama afukuzaye upepo. Haraka nachukua moja ya vitabu vitakatifu, najaribu kutafuta maneno ya kupoza hisia zinazoniandama. Napekua pekua bila kujua nini hasa natafuta kusoma, nakutana na kisa cha Mfalme Nebukadneza. Napata shauku ya kurudia kisa chake nilichokikariri nilipokuwa mtoto, nakutana na maneno ‘mene mene na tekel’. Najikumbusha maana yake; ‘ufalme wake umepimwa na umeonekana haufai’!

Natabasamu kwa uchungu. Ni kama nimeona kidole kikiandika maandishi hayo katika ukuta wa taifa letu. Naukumbuka mjadala ulioibuliwa na Katibu wa Itikadi wa CCM, John Chiligati, ambaye pia ni Waziri katika serikali ya Rais Kikwete wa kubeza na kutweza wenye kuhoji uwezo wa Rais Kikwete. Nakumbuka kauli ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kwamba nchi imekwama Rais Kikwete ameelemewa. Nakumbuka maneno ya Mbowe akitangaza kwamba Rais Kikwete ameshindwa kuliongoza taifa na hivyo kuna haja ya watanzania kutompa kura yeye na chama chake katika uchaguzi wa mwaka 2010. Nakumbuka maneno ya Waziri Mkuu na Jaji mstaafu Joseph Warioba kwamba nchi si shwari. Mene mene na tekel!

Napata nguvu ya kuamka na kuandika; Rais Kikwete amenidhihirishia mimi niliye mdogo, ambaye sistahili hata kufungua kidamu za viatu vyake kwamba anaipeleka nchi harijojo. Katiba ya nchi yetu inatamka kwamba kila mtu anastahili heshima lakini katika medani ya uongozi; heshima ya mtawala inalindwa kwa maneno na matendo yake. Namheshimu Rais Kikwete lakini maneno na matendo yake, yanastahili kukosolewa. Hakika hotuba ya Rais wetu imenidhihirishia pia kuwa hata wale washauri na wasaidizi wake waliopo pale Ikulu na serikalini wanapaswa kutuambia watanzania kwanini kodi zetu zitumike kuendelea kuwalipa mishahara kama wanashindwa kutimiza wajibu wa kulinda heshima ya taasisi ya Urais. Nakabiliwa na mtanziko bado, kati ya kuandika vile ninavyoamini na kuonekana kwamba sinaheshima kwa Amiri Jeshi mkuu. Ama kusema ukweli, nikiamini kwamba Rais aliye kioo cha taifa letu atachukua hatua za haraka kujirekebisha na kurekebisha hali ya mambo inavyokwenda katika taifa letu. Rais Kikwete aliwahi kusema kwamba alikuwa mwanafunzi mzuri wa Mwalimu Nyerere; hivyo naamini amesoma waraka wake wa ‘tujisahihishe’. Kutenda kosa si kosa, kosa kurudia kosa.

Kadiri hotuba ya Rais ilivyokuwa ikicheleweshwa ndipo matumaini yalipozidi kwamba pengine kulikuwa na mambo mazito ambayo mkuu wa nchi alikuwa akiyaandaa. Shauku ya kukosa hotuba za Rais kwa mwezi wa Septemba tofauti ya utaratibu ambao Rais amejiwekea ikazimwa kwa hotuba ambayo kimaudhui inafafana na hotuba ambayo tayari Rais alishaitoa Bungeni mwezi Agosti na kauli zake zilizofuatia katika ziara zake. Nikajiuliza; yamfaa nini mwanadamu kusema kama hana cha kusema?.

Rais wangu alionekana kuelemewa na mambo moyoni, haiba yake imegubikwa na uchovu pengine kutokana na ziara nyingi ama ni msongo wa mawazo au ni tatizo la macho yangu la kuona yasiyopaswa kuonekana. Rais alikuwa akihutubia kwa kutazama huko na kule kama vile palikuwa na nguvu za giza pembeni zikimzinga asitoe mwanga kwa taifa letu analoliongoza. Wanasaikolojia wanajua, jinsi ujumbe unavyotolewa unaweza kusema mengi kuliko hata ujumbe wenyewe.

Rais akaanza kwa kugusa suala tete la Tanzania kujiunga na OIC. Moja kwa moja akawaasa watanzania wasiuendeleze mjadala huo. Mjadala ambao umeendelezwa na serikali yake yenyewe, mjadala ambao yeye mwenyewe katika hotuba yake ameweka bayana kwamba serikali inauendeleza. Nikashangaa! Lakini nikashangaa zaidi kwa Rais Kikwete kutofautina wazi wazi na Waziri wake wa Mambo ya Nje, Benard Membe ambaye Rais Kikwete amemuita kuwa ndio ana dhamana ya suala hilo. Wakati Rais anasema kwamba utafiti wa suala hilo bado haujakamilishwa na Waziri Membe, waziri mwenyewe wakati anahutubia bunge Agosti 22 mwaka huu huu alitangaza kwamba wizara yake imeshakamilisha utafiti. Nani mkweli kati yao Mungu ndio ajuaye. Lakini Mwalimu Nyerere, katika kitabu cha Uongozi wetu na hatma ya Tanzania, alizungumza vizuri kuhusu serikali. Mwalimu aliweka wazi, mkusanyiko wa mawaziri wasiokuwa na dira ya pamoja na uwajibikaji wa pamoja, wanabaki kuwa serikali kwa mujibu wa sheria tu. Lakini kimaadili na kimantiki; hakuna serikali! Rais anataka kila mtu akae kimya aiachie Wizara imalize kazi yake, kama vile wizara ni chombo kisikokuwepo Tanzania kisichowajibika kufanya kazi kwa kuzingatia hisia na matakwa ya watanzania. Kwa mtindo huu wa funika kombe, Rais Kikwete anazidi kuligawa taifa chini kwa chini; ni kama kujaribu kufunika moshi na kujifariji kuwa hakuna moto.

Liliamshwa la mpasuko Zanzibar; likajadiliwa, likakwamishwa. Liliibuliwa na mahakama ya kadhi; likakolezwa, likafunikwa. Likaibuliwa la mafisadi; likavumishwa, likatulizwa. Limeibuka la OIC; likachochewa, limefutikwa. Uongozi wa kuahirisha matatizo badala ya kuyatatua! Haya na mengine ni mabomu ya wakati.

Zoezi la kutumia visingizio kuahirisha matatizo likaendelea katika suala la walimu pia. Nilitaraji walau kwa mara hii Rais awaombe radhi walimu kwa ahadi yake aliyoitoa awali ambayo haikutimizwa katika tarehe ambayo aliitaja mwenyewe. Kwa kuwa sakata hili liko mahakamani; niishie hapa, nivute subira. Walimu waendelee tu kusota kwa sababu ya udhaifu wa serikali wa kutoweka kumbukumbu vizuri za waliofariki na zile za kutambua stahiki za kila Mwalimu. Serikali isiyoweza kuwatambua wafanyakazi wake inaweza kweli kuwakumbuka wananchi wa kawaida?

Ndipo Rais alipohamia kwenye changamoto ya hali ya uchumi ya dunia na hasa wa mfumo wa fedha unaozikabili nchi zilizoendelea. Kilichonishangaza ni Rais kutumia muda mrefu kuhutubia yale yale ambayo aliyasema kwa taifa Katika hotuba yake ya Tanga wakati wa sherehe za kuzima Mwenge na maadhimisho ya miaka tisa ya kifo cha, hayati Mwalimu Julius Nyerere. Halafu Rais katika kutafuta suluhisho la suala hilo, hoja kuu aliyoitoa ni kukaribisha wazo la Rais George Bush wa Marekani la kuitisha mkutano maalum wa kimataifa wa kuzungumzia tatizo la kifedha la kimataifa!. Utegemezi wa mawazo toka Washington ndio unaotufanya tusahau kulinda mihimili ya kiuchumi ambayo awamu zilizopita za utawala wa nchi yetu zilijaribu kuiweka. Kubwa zaidi, nilitarajia Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kuwaeleza watanzania ni jinsi gani anakusudia kuziunganisha nchi zingine za Afrika kuhakisha nafasi ya Afrika inahakikishwa. Badala yake Rais Kikwete ameishia kulalamika tu kwamba “kwa bahati mbaya afrika imesahaulika katika mkutano huo”. Rais Kikwete walau angetumia nafasi hiyo kueleza mikakati ya bara la Afrika hususani ile ya kuunganisha jumuia mbalimbali za kiuchumi iliyojadiliwa nchini Uganda ambapo yeye alishiriki kama sehemu ya ujenzi wa nguvu ya kiuchumi ya bara letu. Uthabiti na ueledi kama huo ungekuwa ni zawadi nzuri kwa vijana wa Tanzania wakati wanaungana na wenzao kuadhimisha siku ya vijana Afrika.

Kama ilivyotarajiwa na wengi Rais Kikwete akagusia suala la mauji ya Maalbino, ikiwa ni siku chache toka alizungumze suala hilo kwa kina Oktoba 19, 2008. Mara hii Rais akiwataka wananchi watoe kwa siri taarifa za watu wanaojihusisha na vitendo hivyo. Binafsi nilitarajia badala ya kutaka orodha mpya, Rais Kikwete kama alitaka kuzungumzia tena suala hili, angeueleza umma wa watanzania orodha za mwanzo za watuhumiwa wa mauaji ya maalbino ambazo ziliwasilishwa kwa vyombo vya dola ikiwemo kwa kufuatilia mtandao ulioanikwa na mwandishi wa habari wa BBC, Vicky Ntetema. Lakini haya mambo ya Rais Kikwete kutaka orodha za siri hayakuanza leo, aliwahi kutaka orodha ya watuhumiwa wa biashara ya madawa ya kulevya, akapatiwa; kimyaaa. Zikafuata orodha nyingine mbalimbali; hakuna hatua zinazoeleweka. Ndipo ikafuata ile orodha ambayo kwa ushujaa wa Dr Wilbroad Slaa(Mb) na viongozi wenzake wa upinzani waliamua kuitoa orodha hiyo hadharani kabisa pale Uwanja wa Temeke Mwembe Yanga. Orodha ya Mafisadi(list of shame) ikawekwa hadharani; hasara ya ufisadi uliotajwa inasababisha vifo vya watanzania wengi zaidi kila siku mpaka leo.

Kama kila siku wakina mama wajawazito wanakufa kwa kukosa huduma bora za kujifungua. Kama kila siku watanzania masikini wanakufa kwa kushindwa kuweza kununua dawa za kutibu malaria. Kama helikopta mbovu zinanunuliwa na kuua. Kama watoto wanakufa kwenye kumbi za disco kwa kukoseshwa hewa. Basi mafisadi ni sawa wauaji! Taifa linazidi kugawanyika, kati ya tabaka lenye kufa taratibu kwa kunyonywa kwa ufisadi na tabaka lililojifungia kwenye pepo ya akaunti za vijisenti mpaka nje ya nchi.

Rais Kikwete akaendelea kuikwepa Orodha ya Mafisadi kwa ukamilifu wake, akaendelea kuzungumzia suala la EPA tu. Akaendelea kukwepa kusema chochote kuhusu Meremeta, Tangold, Deep Green na ufisadi mwingine ambao kwa ujumla wake ni mara kumi ya bilioni 133 za EPA.

Lakini hata kwenye EPA kwenyewe, Rais Kikwete katika hotuba yake ameendelea kukwepa kuchukua uamuzi; amepalilia mche wa mbegu ya ubaguzi katika utawala wa sheria ambayo aliipanda Agosti 21 mwaka 2008 kupitia hotuba yake bungeni.

Rais Kikwete ameendelea kuliganya taifa kwa kuwalinda mafisadi na kugeuza suala lao kuwa la madai badala ya jinai.

Katika hotuba yake Rais Kikwete anatoa pongezi kwa Kamati ya Mwanasheria Mkuu “kwa kazi nzuri iliyofanya ambayo mbali na kubaini namna ya tuhuma za uhalifu zilivyofanywa, pia ilibaini wahusika na kuwabana kiasi cha kufanikiwa kurejeshwa kwa fedha ambazo vinginevyo zingepotea kabisa. “

Kama Rais Kikwete mwenyewe anakiri kwa maneno yake mwenyewe kwamba kamati yake imebaini uhalifu na wahalifu sasa ni vipi Rais huyu huyu anawapa msamaha wahalifu kabla ya kufikishwa mahakamani? Anawapa msamaha huu kwa sheria ya nchi gani? Maana Katiba ya nchi na sheria ambazo Rais ameapa kuvilinda vinampa mamlaka chini ya utaratibu maalum wa kusamehe watu kwa sababu Fulani Fulani baada ya kushtakiwa na kuhukumiwa(clemance/parole). Hakika Rais Kikwete amekiuka katiba kwa kuendesha nchi kwa ubaguzi na kuvunja sheria za nchi kwa kulinda wahalifu. Kwa mantiki hii, na vijana wezi nao wakirudisha mali za wizi nao waachiwe huru tu ili tujenge taifa la misamaha ili wajumuike na hao mafisadi walioghushi nyaraka na kuhujumu uchumi wa taifa. Milango ya magereza na ifunguliwe ili majambazi waachiwe huru, na milango ya mahakama ifungwe ili wezi wasishitakiwe tena; ili tujenge taifa lisilo na utawala wa sheria, linaoendeshwa kwa kanuni za mwituni. Mene mene na tekel!

Namsikiliza Rais wangu kwa mara nyingine akitaja kiwango cha fedha kilichorudishwa bila kuwa na hakika. Kwa mara nyingine akitoa maagizo ya kufungua mashtaka kwa watu ambao hawajarudisha fedha; maagizo ambayo aliyayatoa siku nyingi. Kwa yale makampuni mengine tisa yaliyofisadi bilioni 40 Rais ndio kwanza ‘anakusudia’ kuwataka polisi waendelee na uchunguzi. Na kati ya hayo ipo ile kampuni ya Kagoda Agricultural Limited iliyochota takribani bilioni 30 ambazo nyingine zimeelezwa na vyanzo mbalimbali kuwa zilitumika kwenye kampeni za uchaguzi zilizomweka yeye na chama chake cha CCM madarakani. Rais Kikwete amekosa uthubutu na uthabiti wa kuwataja hadharani maswahiba wake na kuwachukulia hatua. Mene mene na tekel.
Rais Kikwete amemalizia hotuba yake kwa kutusihi watanzania tujiepushe na mambo yanayoweza kutugawa na kupandikiza mbegu za chuki miongoni mwetu na badala yake tuimarishe maelewano, mshikamano na umoja wa kitaifa. Misingi ambayo yeye mwenyewe ameibomoa kwa maneno na matendo yake. Ukiona wananchi wanazomea viongozi, wanarusha mawe, wanalala barabarani ujue migawanyiko imeshapandikiza mbegu ya chuki na kukata tamaa. Vitabu vitakatifu vinaeleza kwamba amani ni tunda la haki. Maelewano tunayopaswa kuyaimarisha ni yale ya kutambua asili na matitizo yanayolikabili taifa letu na kuelewana suluhu tunayohitaji. Mshikamano tunapaswa kuuimarisha ni wa kuunganisha nguvu ya umma katika kuleta mabadiliko tunayoyahitaji. Umoja wa kuimarisha ni unaojengwa kwa misingi ya uadilifu na fikra mbadala zenye kupinga aina zote za ufisadi na kutetea rasilimali za taifa.

Daima tukumbuke; mabadiliko ya kweli katika taifa letu hayawezi kuletwa na mafisadi wale wale, wa chama kile kile, chenye uoza ule ule, wakiendeleza yale yale kwa ari, nguvu na kasi mpya. Kwa falsafa ya chukua chako mapema(ccm), Tanzania yenye neema haiwezekani. Ni wakati wa kusimama na kujitambulisha; ama upande wa kuliunganisha taifa ama kuligawa, historia itakuhumu kwa kadiri ya maamuzi yako ya leo. Mene mene na tekel. Tuombe ulinzi wa Mungu tuvuke salama!

John Mnyika
Novemba Mosi, 2008-Mwanza, Tanzania


Na ameandika pia haya kuhusu Rais Kikwete:

TAARIFA KWA UMMA

SALAMU ZA MSHIKAMANO KATIKA SIKU YA VIJANA AFRIKA

“VIJANA TUFIKIRI NA KUUNGANA KUKOMBOA AFRIKA”

Novemba Mosi ni siku ya Vijana Afrika. Siku hii imepitishwa na Umoja wa Afrika kama siku maalum ya kuadhimisha na kutafakari mchango wa vijana katika maendeleo ya bara letu kiuchumi, kisiasa na katika nyanja mbalimbali za jamii. Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA(BAVICHA), napenda kuungana na vijana wote barani Afrika katika kuadhimisha siku hii.

Kama sehemu ya maadhimisho hayo, vijana wa CHADEMA wamepanga kufanya mkutano na waandishi wa habari katika makao makuu ya chama Novemba Mosi ili kuzungumzia hali ya siasa, uchumi na kijamii katika bara la Afrika katika muktadha wa changamoto zinazowakabili vijana na fursa ambazo zinaweza kutumika.

Nachukua fursa hii kutoa salamu za mshikamano kwa vijana wote kuungana kuitumia siku hii kutafakari nafasi na wajibu wa vijana katika kuleta demokrasia na maendeleo katika bara la Afrika.

“Vijana wa zamani kama Mwalimu Nyerere, Nkurumah Mandela na wengineo walitumia ujana wao kupambana na ukoloni, na kuleta uhuru katika mataifa yao. Ni wajibu wa vijana wa sasa kuwa mstari wa mbele katika kukabiliana na ushindani wa kibeberu unaoliathiri bara la Afrika nyuma ya kivuli cha utandawazi. Vijana wanaweza kutekeleza wajibu huu vizuri kama watathubutu kufikiri na kufikiri kuthubutu kuunganisha nguvu bila kujali mipaka ya nchi, hali au itikadi”

Bara la Afrika ni bara ambalo limejaliwa rasilimali, lakini rasilimali hizi zimegeuzwa na watawala kuwa laana(resource curse) yenye kuchochea vita na kuongezeka masikini kwa wananchi walio wengi hususani vijana.

Tunachukua fursa hii kuwataka vijana wa Afrika badala ya kuelekeza nguvu zao kutumika katika vita na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe watumie nguvu hizo kupambana na ufisadi, kutetea rasilimali na kuleta mabadiliko katika mataifa yao kupitia fikra mbadala.

Nafasi ya vijana kuleta ukombozi katika bara ni kubwa kama vijana watatumbua kwamba bara la Afrika lina uwingi mkubwa wa vijana kuliko makundi rika mengine; na kwamba vijana wakijitazama na kutazamwa kama suluhisho badala ya tatizo wanaweza kutoa mchango mkubwa zaidi katika maendeleo ya bara letu.

Ni vyema, waunda sera na watoa maamuzi barani Afrika wakatambua uwepo wa ongezeko kubwa la idadi ya vijana(youth population bulge) na kwamba wachukulie hali hii kuwa ni fursa badala ya tatizo. Bila hali hii kutambuliwa rasmi na kuundiwa sera na mikakati, matatizo yanayowakabili vijana mathalani ongezeko la ukosefu wa ajira, upungufu wa fursa za kielimu, mmomonyoko wa maadili, ongezeko la matumizi ya madawa ya kulevya na kusambaa kwa ugonjwa wa VVU/UKIMWI miongoni mwa vijana yatazidi kushamiri.

Changamoto ya ongezeko la vijana Afrika inaathiri zaidi miji mikubwa katika Afrika kutokana na kasi ya vijana kutoka vijijini kukimbilia mijini kutafuta fursa za maisha. Hivyo, katika kuadhimisha siku ya vijana Afrika kwa mwaka huu, mkazo uwekwe katika kuhamasisha uwepo wa mazingira ya kuboresha sekta zinazogusa vijana wengi Afrika hususani kwa kuboresha kilimo. Pia, sekta za rasilimali Afrika mathalani uchimbaji madini na mafuta ziwekewe mazingira ya kutoa ajira kwa vijana walio wengi badala za sekta hizo kutawaliwa na makampuni makubwa ya kigeni. Hata pale sekta hizo zinapotawaliwa na uchimbaji mkubwa mkazo uwekwe kuhakikisha muunganiko wa mbele na nyuma(forward and backward linkage) na sekta nyingine za kiuchumi.

Ili kuhakisha kwamba nguvu ya umma ndio inakuwa msingi wa uongozi katika Afrika, vijana wachukue hatua za kulinda demokrasia Afrika ambayo imeanza kutetereshwa na utadamuni ambao unaoendelea katika bara hili wa kung’ang’ania madaraka. Utamaduni huu unachukua sura ya baadhi ya nchi kutawaliwa kijeshi lakini pia unachukua sura ya ung’ang’anizi wa madaraka hata baada ya chaguzi kutaka vingenevyo kwa kutumia mwanya wa uundaji wa serikali za mseto ama za umoja wa kitaifa kama njia ya kuepusha migogoro.

Mwisho, ili kuwa na muongozo wa pamoja katika kuwezesha vijana kutimiza wajibu wao katika bara la Afrika, tunatoa rai kwa serikali za Afrika ambazo hazijaridhia bado Mkataba ya Vijana wa Afrika(African Youth Charter) ulipitishwa na viongozi wa umoja wa Afrika mwaka 2006 mjini Banjul nchini Gambia kufanya hivyo mara moja. “Na katika hili, namtaka Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika aonyesha mfano mzuri kwa wenzake kama kweli wamedhamiria kuweka mstari wa mbele kushughulikia masuala ya vijana. Inashangaza kwamba mpaka pamoja na Rais Kikwete kusaini mkataba huo mwaka 2006 akiwa mjini Banjul, mpaka sasa mkataba huo haujaridhiwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kila mwaka, kuanzia wakati huo mpaka sasa, Wizara inayohusika na masuala ya vijana imekuwa ikitoa kauli kwamba mkataba huo utaridhiwa ‘kikao kijacho cha bunge’. Hata hivyo vikao vingi vimepita bila mkataba huo kuridhiwa; wakati sasa umefika wa Rais Kikwete kama Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri kuiwajibisha hadharani wizara inayohusika kwa kuchelewa kutimiza wajibu huu muhimu wa maendeleo ya vijana wa Tanzania na Afrika kwa ujumla”

Ujumbe huu umetolewa Mwanza-Tanzania 31 Oktoba 2008 na:

John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa
Posted by John Mnyika at 5:05 AM 0 comments Links to this post
Monday, October 27, 2008
Salamu za Mshikamano kuunga mkono Maandamano ya Wadau wa Habari
Salamu za Mshikamano kuunga mkono Maandamano ya Wadau wa Habari

Ndugu Wahariri

Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) tukiwa ni sehemu ya wadau wa sekta ya habari nchini, tunaunga mkono maandamano ya amani mliyoitisha ya kupinga hatua ya serikali kulifungia gazeti la MwahaHALISI.

Tunawapongeza wahariri kwa mshikamano wenu katika kipindi hiki cha majaribu; endeleeni kusimama pamoja, ni umoja wenu ndio utakaokuwa kinga ya pamoja dhidi mtu au chombo chombo chochote kinachoingilia uhuru wenu. Mshikamano wenu ni ishara ya kushindwa kwa mkakati wa ‘wagawe uwatawale’ na imani kwamba umoja ni nguvu. Wahariri wote hawapaswi kukaa kimya kuhusu kufungiwa kwa MwanaHALISI kwa kuwa leo ni kwa gazeti hilo, kesho itakuwa kwa gazeti lingine; hivyo ni vyema kuungana pamoja kulinda uhuru, taaluma na sekta ya habari nchini.

Kwetu sisi hatua hiyo ya serikali tunaitafsiri zaidi ya kufungia gazeti la MwanaHALISI; ni hatua ya kufungia uhuru wa kusambaza habari na uhuru wa kupokea habari. Hivyo hatua hiyo ni kinyume cha haki za binadamu, kinyume cha utawala bora na ni kikwazo kwa demokrasia na maendeleo. Hakika serikali na viongozi wake wamevuka mstari wa kukubali kukosolewa na sasa wameamua kuanza kufungia uhuru wa fikra mbadala.

Hatua ya Waziri mwenye dhamana na sekta ya habari kugeuka mlalamikaji, mwendesha mashtaka na mfungaji ni mwelekeo mbovu wa kupuuza taasisi za kusimamia uwajibikaji na haki. Uamuzi uliofanywa na serikali hauna tofauti na unaofanywa na raia wanaojichukulia sheria mikononi(mob justice). Kwa serikali inayoheshimu misingi ya asili ya haki, tulitarajia chombo chochote cha habari, kikivunja sheria ama kukiuka maadili dhidi ya serikali, viongozi wake ama watu binafsi mashtaka ama malalamiko yangepelekwa kwa taasisi zinazohusika mathalani Baraza la Habari(MCT) ama Mahakama.

Hatua ya serikali kufungia gazeti la MwanaHALISI pamoja na kuwa imechukuliwa kwa mujibu wa sheria iliyopo, imekiuka misingi ya asili ya utawala wa sheria. Kwani kulikuwa na sheria nyingine nzuri ambazo serikali ingeweza kutumia kupitia mahakama lakini ikaamua kuchagua kutumia sheria mbaya kwa kutumia mamlaka ya Waziri. Itakumbukwa kwamba wadau wa sekta ya habari na hata serikali yenyewe imekuwa ikikiri kwamba Sheria hiyo iliyotumiwa ni sheria mbovu inayohitaji kufutwa ama kufanyiwa marekebisho makubwa ikiwemo kupunguza mamlaka makubwa ya viongozi wa serikali dhidi ya vyombo vya habari. Sheria yoyote inayotambulika kuwa mbovu katika jamii yoyote, inapoteza uhalali wa kihaki(legitimacy) miongoni mwa umma na hivyo kuendelea kuitumia ni kuteteresha misingi ya utawala wa sheria na kutoa mfano mbaya kwa vijana nchini na wananchi kwa ujumla. Hivyo, tunachukua fursa hii kuitaka serikali kuharakisha mchakato wa kupitisha sheria ya vyombo habari na sheria ya uhuru wa taarifa.

Aidha tumeshangazwa na uamuzi wa serikali kufanya maamuzi yake kwa ubaguzi kwa kulichukulia hatua gazeti la MwanaHALISI na kukwepa kuyachukulia hatua magazeti mengine ambayo yameandika habari inayoshabihiana na maudhui ya habari iliyoandikwa na gazeti hilo. Kwa muda mrefu sasa, habari za uwepo wa viongozi ama makundi ndani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) yenye kupanga ‘kumng’oa’ Rais Jakaya Kikwete miongoni mwa wanaotarajiwa kugombea urais kupitia chama hicho mwaka 2010 zimeandikwa na magazeti mbalimbali. Hatua hii ya kibaguzi inaibua maswali kuhusu dhamira ya serikali kulifungia gazeti hilo wakati huu ambapo mchango wa gazeti hilo na mengine yaliyo mstari wa mbele kupinga ufisadi na kutetea rasilimali za taifa unahitajika kwa kiasi kikubwa. Hata baada ya kulifungia gazeti la MwanaHALISI, habari za aina hiyo zimeendelea kuandikwa ikiwemo na vyombo vya habari vya nje; mathalani tarehe 24 Oktoba, 2008 kutoka Ufaransa gazeti la Africa Intelligence inayomtaja Rostam Aziz kukusanya fedha kwa ajili ya kufadhili kundi lake katika uchaguzi huo. Katika muktadha huo, serikali inapaswa kulifungia gazeti la MwanaHALISI mara moja, kama imeonyesha wazi kushindwa kuyachukulia hatua magazeti mengine.

Kadhalika kwa mtiririko wa matukio katika taifa letu, kuna mwelekeo wa Serikali na CCM kuminya maoni yenye kumkosoa au kumgusa Rais Kikwete. Mjadala wa Rais Kikwete ‘kung’olewa’ katika uchaguzi mwaka 2010 unaelekea kuichukiza kwa kiasi kikubwa Serikali na CCM. Gazeti la MwanaHALISI liliandika habari ya namna hiyo, likafungiwa na Serikali. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akiwa katika ‘Operesheni Sangara’, alitoa hoja hiyo na matokeo yake CCM ikaibuka na kujibu kwa vitisho na vioja. Vijana wa Tanzania wangependa kupata mfano uongozi bora wenye kukubali kukosolewa na kukubali mabadiliko badala ya uongozi legelege wenye kuendeleza udikitekta wa kimawazo na hivyo kuminya fikra huru. Si dhambi kwa CHADEMA ama mtu yoyote kutaka kuiondoa CCM ama kiongozi wake yoyote madarakani mwaka 2010 kupitia njia za kidemokrasia.

Mwisho, tunatoa mwito kwa watanzania wote kusoma alama za nyakati na kuunga mkono harakati hizi za wahariri na wadau wa sekta ya habari kutetea uhuru wa kweli katika taifa letu. Jamii itambue kwamba kitisho cha uhuru na haki kwa mtu Fulani au mahali Fulani ni tishio kwa watu wote na mahali pote. Yanayofanywa kwa vyombo vya habari, yanaweza pia kufanywa kwa watetezi wengine kwani hivi karibuni taifa limeshuhudia Asasi ya HAKIELIMU ikitishiwa kutokana na jitihada zake za kuhamasisha mabadiliko ya fikra katika sekta ya elimu na kupiga vita ufisadi unaoathiri sekta hiyo. Tuko katika kipindi cha majaribu; kuibuka kwa mijadala yenye kuchochea mgawanyiko/ubaguzi, kuongezeka kwa matabaka na malalamiko juu ya hali za maisha. Katika wakati huu ambapo misingi ya nchi yetu iliyopo katika Ngao ya Taifa ya Uhuru na Umoja inapotikiswa ni wakati wa kuunganisha “Nguvu ya Umma” kupinga aina zote za ufisadi na kutetea rasilimali za taifa kwa kuhamasisha maadili, fikra mbadala na mabadiliko ya kweli. Kuunga mkono maandamano ya wadau wa sekta ya habari ni sehemu ya azma hiyo. Mshikamano, daima; pamoja, tutashinda!

Wasalaam,

John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa
Mwanza, Tanzania-28/10/2008


Wewe ndio unafanya uchochezi na kejeli sio Ansbert Ngurumo wala John Mnyika
 
Juzi huko Tabora kazomewa na wananchi akawauliza 'mnanizomea mimi au huyu hapa',hakukuwa na haja hata ya kuuliza wanamzomea nani kwa mila zetu za kiafrika unapiga fimbo chini karibu na mtu kama onyo fimbo ya pili unampiga mwilini.
 
The presidency is an institution lead by the president. Urais ni taasisi inayoongozwa na rais. Uraisi na rais ni vitu viwili tofauti. Urais ni taasisi ya heshima ambayo haistahili kejeli za aina yoyote. JK kama rais, bado anastahili heshima zake kwa kuiongoza taasisi ya urais. Rais ni binadamu kama walivyo binadamu wengine hivyo na yeye ana mapungufu yake. Pamoja na mapungufa hayo yanaweza kuishusha heshima yake mbele ya jamii anayoingoza lakini isiwe ndio tiketi ya kumdharau au kumkebehi. Hii sio heshima. Tutake tusitake, yeye bado ndiye raisi aliyemadarakani hivyo heshima inabaki pole pale na ubinadamu ndio unafuatia ukiandamana na constructive criticism.
Baba mzazi anabaki kuwa baba regardless amefanya vitendo vya aina gani na kushusha heshima yake kwa jamii. Wewe kama mtoto heshima kwa baba lazima ibaki pale pale.

Jamani JK aheshimiwe tuu, mbona 2010 sio mbali?.
 
Juzi huko Tabora kazomewa na wananchi akawauliza 'mnanizomea mimi au huyu hapa',hakukuwa na haja hata ya kuuliza wanamzomea nani kwa mila zetu za kiafrika unapiga fimbo chini karibu na mtu kama onyo fimbo ya pili unampiga mwilini.


..kitendo cha kuzomea mbele ya mfalme[rais].....ni sawa na kumzomea yeye moja kwa moja......na kitendo cha rais kuanza kuhoji..nani anayezomewa ..ni cha kutokujiamini............aliiingiwa na hofu///
 
Ndugu kuna tofauti kubwa sana kati ya theutamu na hao unaowaandika wewe katika the utamu yale sio mawazo na misimamo yake yeye analetewa picha wengine wanajadili -- hao kama ngurumo yeye anaandika vyake alivyofanyia kazi yeye , yeye anaweza kuja kutoa ushahidi wa kile alichoandika muda wowote atakapohitajika

nafikiri umenipata
 
Nani kakwambia unaweza kufananisha baba mzazi na Rais?

Sijaona baba wa kuchaguliwa bado!

Rais ana nguvu kubwa serikalini, kwa nini anawakumbatia hao mafisadi? UOZO ulishafanyika, hiyo tunakubali serikali iliyopita ya UKAPA ILIUZA NCHI. JK ameshika madaraka, kwa nini asisafishe huo uozo uliopo?

Mtu yeyote mwenye akili angefanya hivyo. Hata mtoto wa FORM II anajua nini cha kufanya.

Acheni kuilea hii CANCER ambayo inaweza kutibika kwa namna moja au nyingine.
 
..kitendo cha kuzomea mbele ya mfalme[rais].....ni sawa na kumzomea yeye moja kwa moja......na kitendo cha rais kuanza kuhoji..nani anayezomewa ..ni cha kutokujiamini............aliiingiwa na hofu///

na ninaamini anaielewa mantiki hii nyepesi... na ninaamini ameshajua wananchi wanamuonaje.... kama hajajua akasome kwa Ngurumo kuhusu kujua
 
Please provide specific evidence to substantiate your accusations.

While I am against ridiculing the office of the president, there is a thin line between the office and the person of the president as well as what you described to be criminal conduct against the dignity of the president and the domain of that right called freedom of expression.

You would do well to argue your case in a presentation that clearly demonstrate the following.

1. The ridicule is unwarranted and unnecessary
2. The ridicule is on the office and not the person of the president
3. The ridicule is far and beyond the provisions of freedom of expression
4. The ridicule is criminal

Then, and only then, will your case have any merit to warrant discussion by serious minds. Otherwise you may be branded as an appeaser, an office seeker or indeed a Salva Rweyemamu type infiltrating ideas to unnecessarily cushion the president.

The people of this forum are a fair and observant lot, and everything you provided will be justly considered. As they say, the ball is now in your court.
 
Last edited:
Kumezuka tabia ya bloggers wa kitanzania kuendeleza kejeli kwa Rais Kikwete kwa kutumia lugha kali kali ambazo pia zinaleta uchochezi. Kati ya Bloggers washabikia tabia hii yupo Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua, yupo pia huyu JJ. Watu hawa wanashindwa kutofautisha kati ya ukosoaji na udhalilishaji wa hadhi ya Rais aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya watanzania wote. Mamlaka zinazohusika lazima zichukue hatua kukemea hali hii. Kama kuna blogger mwingine mwenye tabia hii atajwe pia hapa ili aweze kufahamika.Bloggers watambue kwamba wanaweza kuhukumiwa kwa maneno yao wanayoandika andika. Kama tunaweza kuikemea theutamu kwanini tuache kuwakemea hawa?

............ndiyohiyo

Kwahiyo hata akiwasaliti hao asilimia 80 ya waliomchagua bado aendelee kupigiwa makofi?Huu sio unafiki bali kujikomba kwa watawala.Bad news to your my fellow mlalahoi,huyo JK unayejikomba kwake is too busy kuwalinda mafisadi than to care about what you're trying to do.Shame on you!
 
Kwahiyo hata akiwasaliti hao asilimia 80 ya waliomchagua bado aendelee kupigiwa makofi?Huu sio unafiki bali kujikomba kwa watawala.Bad news to your my fellow mlalahoi,huyo JK unayejikomba kwake is too busy kuwalinda mafisadi than to care about what you're trying to do.Shame on you!

Shame upon you to for note defending your president at this hour when he needs you against the mafisadi tide. Just press these links Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua and JJ you read how these guys are discrediting our president. Jk needs our support otherwise if we all bomber him he will enventually side with mafisadi

.......ndiyohiyo
 
Kumezuka tabia ya bloggers wa kitanzania kuendeleza kejeli kwa Rais Kikwete kwa kutumia lugha kali kali ambazo pia zinaleta uchochezi. Kati ya Bloggers washabikia tabia hii yupo Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua, yupo pia huyu JJ. Watu hawa wanashindwa kutofautisha kati ya ukosoaji na udhalilishaji wa hadhi ya Rais aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya watanzania wote. Mamlaka zinazohusika lazima zichukue hatua kukemea hali hii. Kama kuna blogger mwingine mwenye tabia hii atajwe pia hapa ili aweze kufahamika.Bloggers watambue kwamba wanaweza kuhukumiwa kwa maneno yao wanayoandika andika. Kama tunaweza kuikemea theutamu kwanini tuache kuwakemea hawa?

............ndiyohiyo

Mi nadhani mtu wa kwanza wa KUKEMEWA na Mamlaka zinazohusika ni WEWE! Unachokileta hapa ni KUJARIBU kuwatia HOFU watu na kuleta uchochezi! Hivi wewe ni nani hadi uzikumbushe Mamlaka zinazohusika KUKEMEA watu? Wewe huna tofauti na wale waliomdanganya MFALME kwamba wamemshonea VAZI la ajabu halafu Mfalme naye akaingia Mtaani, watu walipokuwa wakimshangaa yeye akaona WANAMSHANGILIA. Acha kumdanganya Mfalme (tamka Rais) wako wewe! Rais wetu aache USANII! Tumemuweka pale kwa gharama kubwa sana ili alinde UTU wetu sasa kama anaendekeza USANII hatutanyamaza na wala HATUTATISHIKA! UPO WEWE! Baba mwenye familia, familia yake itaendelea kumuheshimu iwapo tu na yeye atajiheshimu, akigeuka akawa BONGE la Mlevi na kupita mitaani akipiga kelele, 'nivue shati nisivue, nivue suruali nisivue, nivue nanihii nisivue' ni nani atakayemuheshimu tena miongoni mwa wana familia wake! Kwa kadiri mambo yanavyokwenda sie wengine inatuuma sana ukizingatia tulisafiri Mamia ya Maili kwenda kumchagua huyu Muungwana na kabla ya hapo hatukuwahi kuchagua ingawa tulikuwa mita tano tu kutoka kituo cha uchaguzi! Acha Bwana!
 
Back
Top Bottom