Bloga Michuzi aalikwa kuzungumza Uingereza

Lukwangule

Senior Member
May 25, 2009
157
2
MFANYAKAZI wa Shirika la Magazeti ya Serikali (TSN) Muhidin Issa Michuzi ameondoka jana kuelekea London, Uingereza, kuhudhuria kongamano la pili la Watanzania wanaoishi nchi za nje (Diaspora 2 conference) akiwa kama bloga.

Michuzi, ambaye ametoa mchango mkubwa katika kupromoti habari za jamii mtandaoni kupitia blogu yake ya issamichuzi.blogspot.com, amealikwa na ubalozi wetu Uingereza.

Akiwa katika mkutano huo atatoa mada inayohusu umuhimu wa habari za jamii mtandaoni katika kujenga daraja kwa walio ndani na nje ya nchi.

Akizungumza jana amesema amefarijika sana kuona kuna wanaotambua mchango mkubwa unaoletwa na vyombo vya habari za jamii mtandaoni, hasa blogu.

Alisema anajisikia mwenye furaha sana kuona azma yake ya kuifanya tasnia hii ya kupashana habari kwa njia ya intaneti unatambulika na kukubalika na kupewa heshima stahili nyumbani kama ilivyo kwa vyombo vya kawaida kama vile magazeti, redio na luninga.

Michuzi, anayeweka rekodi ya kuwa bloga wa kwanza nchini kualikwa kama bloga kwenye mkutano muhimu kama huo, aliushukuru ubalozi nchini Uingereza kwa kuutambua hadharani mchango wa wanahabari za jamii mtandaoni kwa kutoa mwaliko huo.

"Dunia imezidi kuwa kijiji kimoja kidogo kwa teknohama hii ambayo hata Rais Jakaya kikwete yuko mstari wa mbele kutaka iendelezwe mijini na vijijini ili kuwezesha wananchi wawe na habari za uhakika, za haraka na zenye kutoa fursa ya wasomaji kuchangia maoni" alisema Michuzi.

Blogu ya issamichuzi.blogspot.com ilianza rasmi Septemba 8,2005 katika jiji la Helsinki, Finland, ambako alikwenda kuhudhuria mkutano wa Helsinki Conference akiwa kama mwandishi na mpiga picha wa gazeti la Daily News.

Alikuwa ni bloga wa siku nyingi aliyekuwa anaishi Marekani wakati huo,Ndesanjo Macha, aliyemshawishi Michuzi kufungua blogu yake na kuwa bloga wa kwanza wa Tanzania kuupasha ulimwengu ya kila linalojiri nchini.

Blogu hiyo kwa sasa imefikisha wasomaji milioni 8, kati ya hao asilimia 30 wakiwa ni wasomaji wa Tanzania.
 
Hizi ni propaganda za kikomunisti.

Ubalozi wa Tanzania/CCM London kama tujuavyo lazima umpe Michuzi ulaji kwa kuwa amekuwa mstari wa mbele kuitangaza SISIEM hasa London kwenye mtandao wake.

Tukumbuke juzi juzi tu,kulikuwa na issue ya kumtetea Balozi Maajar kwa tuhuma ya kuwa mwanaCCM mbele UK badala ya kuwa balozi wa watanzania wote.

Atamfundisha nani kuhusu blogu/internet nchini UK?

Come on let be serious!T U ME DA NGANYIKWA vya kutosha.

MICHUZI ale per diem yake kwa huu uwendawazimu tulionao
 
Hizi ni propaganda za kikomunisti.

Ubalozi wa Tanzania/CCM London kama tujuavyo lazima umpe Michuzi ulaji kwa kuwa amekuwa mstari wa mbele kuitangaza SISIEM hasa London kwenye mtandao wake.

Tukumbuke juzi juzi tu,kulikuwa na issue ya kumtetea Balozi Maajar kwa tuhuma ya kuwa mwanaCCM mbele UK badala ya kuwa balozi wa watanzania wote.

Atamfundisha nani kuhusu blogu/internet nchini UK?

Come on let be serious!T U ME DA NGANYIKWA vya kutosha.

MICHUZI ale per diem yake kwa huu uwendawazimu tulionao

Thanks mmakonde kwa kuliona hili HII NI DANGANYA TOTO
 
Hizi ni propaganda za kikomunisti.

Atamfundisha nani kuhusu blogu/internet nchini UK?
Come on let be serious!T U ME DA NGANYIKWA vya kutosha.

MICHUZI ale per diem yake kwa huu uwendawazimu tulionao

Ishu si kwamba anaenda kufundisha, this is two way benefiting, atatoa uzoefu wake kuhusiana na responce ya jamii kwa mitandao na habari kwa ujumla, while yeye vilevile atapata uzoefu na pia kukusanya info za kuwabandikia wapenzi wa blogu yake na waTZ kwa ujumla!
 
Of course ni mtu wa Chama, what else will you expect of him???
 
Big news, hongera Michuzi,

Blog yako ni chanzo cha habari muhimu na jamii ya watanzania inaitegemea sana. Wewe ni mfano wa kuigwa na wengi, natumaini kwenye mada yako utatoa shule kubwa kwa bloggers wa Tanzania...!

Hivi umefikisha hits milioni 8 tu? Sikutarajia... Kama JF inapata over 45mil kwa mwezi mmoja nilitarajia kwako itakuwa over 50 mkuu wangu, so far safi sana mkuu!

:)
 
Hivi umefikisha hits milioni 8 tu? Sikutarajia... Kama JF inapata over 45mil kwa mwezi mmoja nilitarajia kwako itakuwa over 50 mkuu wangu, so far safi sana mkuu!

:)
hii mkuu umeiweka kisanii zaidi!
 
Big news, hongera Michuzi,

Blog yako ni chanzo cha habari muhimu na jamii ya watanzania inaitegemea sana. Wewe ni mfano wa kuigwa na wengi, natumaini kwenye mada yako utatoa shule kubwa kwa bloggers wa Tanzania...!

Hivi umefikisha hits milioni 8 tu? Sikutarajia... Kama JF inapata over 45mil kwa mwezi mmoja nilitarajia kwako itakuwa over 50 mkuu wangu, so far safi sana mkuu!

:)

so jf inaoongoza kwa kiasi kikumbwa mno yani kama ni ushindi ni ule wa sunami wa ccm uchaguzi ulopita na kama kigezo ni anayeongoza kwa kufikisha ujumbe kupitia mtandao basi jf ndio walipaswa kuchaguliwa kama haki ingefwatwa
 
Big news, hongera Michuzi,

Blog yako ni chanzo cha habari muhimu na jamii ya watanzania inaitegemea sana. Wewe ni mfano wa kuigwa na wengi, natumaini kwenye mada yako utatoa shule kubwa kwa bloggers wa Tanzania...!

Hivi umefikisha hits milioni 8 tu? Sikutarajia... Kama JF inapata over 45mil kwa mwezi mmoja nilitarajia kwako itakuwa over 50 mkuu wangu, so far safi sana mkuu!

:)

Mkubwa umenigusa, huku kwetu mods wanaelemewa na tunafikiria kuajiri zaidi na tunapo launch itakuwa balaa kabisa!!! Yaani tangu 2005 ni 8,000,000 tu? Na new JF yetu ni over and over na ni 2006 ukiachilia wale wa zamani?? Lo JF inaongoza, tukishindanishwa kidunia tumo kabisa.

Hata hivyo, mkuu wa Wilaya ya Nanihiii hongera sana, japo.
 
kwa criteria ya blog ya tanzania yenye hits nyingi/ most visited per day nadhani blog yake imo kwenye top three. Kwa kigezo kingine cha loyalt kwa serikali hil halina ubishi.

If it was fair evaluation basing on the above criteria then Michuzi should come out as a winner.

Hongera michuzi,
 
Mwenye macho haambiwi tazama! Aliye na sikio na asikie! Over! Kama vipi muulize Invisible atakufafanulia!


nimekupata over
invisible nilimwelewa ila sikuelewa uliposema imekaa kisanii zaidi kanakwamba kadanganya
 
nimekupata over
invisible nilimwelewa ila sikuelewa uliposema imekaa kisanii zaidi kanakwamba kadanganya
wewe ndiyo hukuelewa! kisanii sio kudanganya! ila kama wewe unabeba box basi nitaelewa!
 
Back
Top Bottom