Blandina Nyoni aula TRA!

Blandina Nyoni aula TRA!

Kuwatetea viongozi wa Tanzania hata kama unawaamini namna gani ni sawa na kuvaa mabomu. Mapungufu aliyoyaonesha akiwa wizara ya afya ni Mengi sana, haki yake ataipata kwa Mungu tuu, sababu ndio anaweza kusaheme na kuanza kukuhesabia haki hapo hapo, kwa sisi wanaadamu, Brandina is another rotten government official.

Mkuu acha majungu. Ni Blandina aliyefanya hiyo Wizara ijulikane kama Wizara ya Afya ya wananchi wote, kabla ya Blandina ilikuwa Wizara ya watu wateule wachache sana, ata wengi wa madaktari walikuwa hawatii mguu Wizarani, Wizara ilikuwa inatawaliwa na AMO ambao walikuwa na inferiority complex ya hali ya juu. Hawakutaka mtu yeyote aingie kwenye anga zao, walikuwa wamejiundia mirija na safari nyingi ambazo zilikuwa hazina tija wa impact kwa jamii. Ni Blandina Nyoni aliyefanya mabadiriko makubwa mpaka ata wewe sasa unajua kuna kitu kinaitwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Nitakupa mfano amabao utakuwa umekugusa kwa namna moja au nyingine, ni Blandina Nyoni aliyeanzisha utaratibu wa raia yeyote wa nchi hii ata kama akiwa maskini aende nje ya nchi akapatiwe matibabu hapo zamani ilikuwa ndoto leo hii watoto maskini makundi kwa makundi wamepelekwa nje ya nchi kwa matibabu hii ushuuda ninao. Ni Blandina alileta mabadiriko mpaka Muhimbili National Hospital ikawa kama ilivyo sasa (Emergency medicine dept ni mfano mmoja wapo).

Ni blandina aliyethubutu kuwatawanya Madaktari Bingwa waliomaliza masomo yao kwenda Mikoani ili wakatoe huduma za kibingwa katika hospitali za Rufaa Mikoani ili watanzania maskini walioko huko nao wapate huduma. Alidiriki ata kuwachimba mkwara kwamba atayekaidi atamtimua. Hii ndo chanzo na kisa hasa cha matatizo yote yalipoanzia (Migomo), sababu ata Viongozi wa MAT walikubwa na kimbunga hiki cha Blandina.

Mengi yaliosemwa kuhusu Blandina ni majungu tu na yameshajulikana kama ni majungu ya kupikwa tu. Waliopika majungu yale hawana tofauti yeyote na wale walioneza uvumi wa dawa ya Babu wa Loliondo na kudakwa na watu wavivu wa kufikiri hadi kupelekea maelfu ya watu kupoteza maisha. Ata Mhe. Rais alishawahi kusema kuwa "watanzania wana viwanda vya uongo"
 
Tunapoamua kuwa waadilifu basi tuwe wote, isijekuwa unajifanya mwadilifu kumbe nyuma ya pazia ni mwovu. Naona nyote mnamzungumzia Blandina Nyoni kwa kusikia watu wanavyosema, shukuruni Mungu hamjawahi kuwa surboninate wake ni hatari
 
Pole Tanzania ona Tanganyika inavyokucheka

hapo ndo napoamin ccm inatudharau sana watanzania kwani wanajua hatuna la kufanya. ivi ana uadilifu gani uyu mama wakati ni juzi tu tumebaini ameshiriki kuiba mashina ya kusafisha figo toka muhimbili na kuipeleka aghakan. badala ya kuwa mahakani anaongezewa ulaji. dah nchi yangu tanzania....
 
Aliyekuwa katibu mkuu wizara ya afya dada yetu blandina nyoni amerudishwa kazini kwa mwajiri wake wa zamani(tra)
Kila la heri dada...
 
Hii habari mbona ilishatupiwa zamani sana au wewe ndo unaipata leo?Ila si mbaya mwache arudishwe mbona Kikwete na sofia Simba wamerudishwa kuwa viongozi!
 
long time kitaambo ! Tunasubiri sare za wafanyakazi kutoka mariedo boutique !
 
Sasa unashangaa nini kutokea Tanzania? Labda ingekuwa nchi nyingine labda tungeshtuka.
 
Samahanini wana JF, Hivi huyu si alishawahi kuwa Katibu mkuu wizara ya Ardhi pia, ama?
 
Mkuu acha majungu. Ni Blandina aliyefanya hiyo Wizara ijulikane kama Wizara ya Afya ya wananchi wote, kabla ya Blandina ilikuwa Wizara ya watu wateule wachache sana, ata wengi wa madaktari walikuwa hawatii mguu Wizarani, Wizara ilikuwa inatawaliwa na AMO ambao walikuwa na inferiority complex ya hali ya juu. Hawakutaka mtu yeyote aingie kwenye anga zao, walikuwa wamejiundia mirija na safari nyingi ambazo zilikuwa hazina tija wa impact kwa jamii. Ni Blandina Nyoni aliyefanya mabadiriko makubwa mpaka ata wewe sasa unajua kuna kitu kinaitwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Nitakupa mfano amabao utakuwa umekugusa kwa namna moja au nyingine, ni Blandina Nyoni aliyeanzisha utaratibu wa raia yeyote wa nchi hii ata kama akiwa maskini aende nje ya nchi akapatiwe matibabu hapo zamani ilikuwa ndoto leo hii watoto maskini makundi kwa makundi wamepelekwa nje ya nchi kwa matibabu hii ushuuda ninao. Ni Blandina alileta mabadiriko mpaka Muhimbili National Hospital ikawa kama ilivyo sasa (Emergency medicine dept ni mfano mmoja wapo).

Ni blandina aliyethubutu kuwatawanya Madaktari Bingwa waliomaliza masomo yao kwenda Mikoani ili wakatoe huduma za kibingwa katika hospitali za Rufaa Mikoani ili watanzania maskini walioko huko nao wapate huduma. Alidiriki ata kuwachimba mkwara kwamba atayekaidi atamtimua. Hii ndo chanzo na kisa hasa cha matatizo yote yalipoanzia (Migomo), sababu ata Viongozi wa MAT walikubwa na kimbunga hiki cha Blandina.

Mengi yaliosemwa kuhusu Blandina ni majungu tu na yameshajulikana kama ni majungu ya kupikwa tu. Waliopika majungu yale hawana tofauti yeyote na wale walioneza uvumi wa dawa ya Babu wa Loliondo na kudakwa na watu wavivu wa kufikiri hadi kupelekea maelfu ya watu kupoteza maisha. Ata Mhe. Rais alishawahi kusema kuwa "watanzania wana viwanda vya uongo"

Mkuu ebu fikiri kabla ya kupost, hayo uliyoyaandika hapo ni kinyume tupu, mimi niko muhimbili hapa more than 5 years hayo uliyoyaandika sijayaona. Blandina Nyoni alikua ni mkandamizaji ni hakuna na alikua na jeuri ya kujibu kwa madaktari kama ile kazi kazaliwa nayo.
 
Sina maelezo marefu katika suala hadi pale nitakapopata gazeti la DIRA ambalo limekuja na habari kwamba Blandina Nyoni ambae alitimuliwa Wizara ya Afya hivi sasa ni mmoja wa Makamishina wa Mamlaka ya Mapato Tanzania huku mshahara wake kwa mwezi ni zaidi ya sh. milioni kumi!

Source: Gazeti la DIRA!
Alikuwa huko TRA kabla ya kuja serikalini hata hivyo wakati yuko serikalini alikuwa analipwa mshahara wa TRA.Ukumbuke kuwa nchi hii inaendeshwa na mashushushu.kwa heri
 
Hongera Mama Weledi, Uzoefu na Elimu yako ndo vinakupa heshima ya kutumikia taifa letu hili Changa katika kutimiza Dira ya Taifa 2025.
 
They said 12M sir not 10M, si you know she was not fired? she still enjoys a Governement Car, a Driver, and all that goes with such callings am not sure if she is alone... Someone said 'dhaifu'

dhaifu kwa maana kuwa kuna mkubwa ana kaa maana huyu mwanamama mashalaah
 
Back
Top Bottom