Mimi utafiti wangu usio rasmi ni kuwa pale kuna "system" ya ulaji ambayo ni ya hatari. Wapo tayari kupokea hata sumu wakidai kuwa ni madawa ili tu wapate pesa. Hivyo akija mtu ambaye anataka kuondoa genge hilo basi wanajiunga kumfanyia cha kumfanyia. Mambo ambayo huyo mama anatuhumiwa nayo yawezekana kabisa ni ya kuchonga ili tu kumpaka matope. mfano hivi sasa ulizia kitu chochote kipya kizuri ni cha nani jibu utalipata haraka sana RITZ1. Hivyo bila uchunguzi na kuwa na system ambayo ni transparent tutaendelea kukupiga ramli tu.
Kuna miungu watu pale ukigusa maslahi yao wanakula nawe sahani moja
Blandina Nyoni alipigwa vita kwasababu alikuwa anapangua system ya ulaji iliyojijengea mizizi ya siku nyingi na ndio maana mara tu baada ya yeye kuondoka na Hussein Mwinyi kurudi ,wale wote ambao Blandina Nyoni aliwaondoa huyu kilaza na genege lake alilokuwa nalo toka enzi akiwa naibu waziri akawarudisha pale wizarani!!! Sasa pale siku hizi kazi hazifanyiki ni uswahili swahili tu na watu kuzurula hovyo na ndio maana hata wafadhili wanasita kuleta misaada yao kwenye hiyo wizara kwasababu ya lack of accontability!!!