Black Magic ni nini uchawi upi haswa?

Damaso

JF-Expert Member
Jul 18, 2018
1,576
2,071
Habarini za mchana.
Ninaleta uzi kidogo kuhusu ishu ya black magic, kwani katika soma soma ya vitabu nimepata vitu kidogo vya kuwashirikisha, karibuni.
Tuanze nini maana ya Black Magic: huu ni Uchawi ambao unatumika katika mila nyingi pamoja na tamaduni kadhaa katika jaribio la ushawishi wa kimwili kupitia njia zisizo za kawaida. Hii ni tofauti na White Magic ambao inalenga katika nyanja ya ushawishi ulio mwema katika imani hasa hasa katika kuponya magonjwa pamoja na kutengeneza dawa. Black Magic inahusika hasa katika kuumiza nafsi ya mtu au mnyama.
Black magic au uchawi mweusi unafanyika kupitia vitendo kama vile; kutengeneza mwanasesere kupitia imani ya Voodoo, Hirizi, alama pamoja na ishara za kichawi, laana na mikosi pamoja na ndumba mbalimbali.
Black magic inatumika ili:
1. Kumuwekea mtu laana au mikosi katika maisha yake.
2. Kumlazimisha mtu kufanya jambo bila ridhaa yake. Mfano: kulima shamba kubwa akiwa usingizini.
3. Kuita uwepo wa mashetani pamoja na mapepo.
4. Kufufua wafu.
5. Pamoja na kutafuta maisha marefu kupitia nguvu za kishetani.

Je ni kina nani haswa wanajihusisha na uchawi huu:
1. Jamii ya Wicca nchini Uingereza wapo watu wanaofanya uchawi wa namna hii. Kuanzia karne ya 20 inaaminika kuwa wanajamii hawa walikuwa wanafanya kazi zinazohusiana na uchawi wa namna hii. Ijapokuwa imani juu ya jamii ya Wicca inasimamia katika kuponya na sio kudhuru nafsi ila asilimia kubwa ya wanajamii wanafanya vitendo vinavyoendana na Black magic.

2. Jamii nyingine ni Santeria, hawa wanapatatikana katika maeneo machache ya Carribean pamoja na Afrika ya Magharibi. Ingawa imani yao inajumuisha baadhi ya vitu kutoka Katika imani ya Wakatoliki, ambayo imewapelekea kuwa sheria kuu moja "Do unto others as you would have done unto you." ambayo imetolewa katika maneno ya Biblia katika kitabu cha Luka mtakatifu 6:31. Hivyo kuidhoofisha imani ya Black magic. Lakini bado kuna wanajamii wanaokiuka sheria hiyo kwa kushiriki katika kufanya matendo ya black magic. Wanafanana kidogo na jamii ya Voodoo (nitawaeleza mbele kidogo).

3. Imani ya Voodoo, hii ni kati ya jamii yenye kusifika kwa kutumia uchawi mweusi katika asilimia zaidi ya 90. Kwani hawa jamaa wana uwezo wa kutengeneza ndumba ya kumdhuru mtu kwa kiasi kidogo sana mpaka kufikia dollar 5 za kimarekani. Ijapokuwa waganga wengi wa Voodoo wanatibu pamoja na kutengeneza tiba Kw kutumia uchawi mweupe bado wana ujuzi mwingi sana wa kutumia black magic. Yaani hata akikupa tiba kwa White magic bado anaweza kutumia black magic kukupa tena hali dhoofu ili urudi apige pesa.
4. Dini za Shetani, kumbuka sio wote waliopo katika dini hizi ni wachawi bali kuna watu ambao wao wanashikilia imani ya kupata maisha au uzima wa milele kupitia njia ya shetani, hivyo kupelekea kutumia black magic katika kuwaita majini, mashetani pamoja na mapepo. Hii ni kupitia kuweka sala za kuabudu shetani na kuweka dawa za kichawi.

Je utajuaje kama umerushiwa uchawi mweusi?
Kwanza inapelekea kuchoka kwa ghafla, ikifuatana na kichwa kuuma na kuwa kizito. Pia kwa wale ambao wapo sensitive sana utaanza kuhisi kitu kisicho cha kawaida mfano, kuhisi haupo peke yako kuzunguka mazingira yako, nywele kusimama ghafla pamoja na kuigiwa na uoga hofu ghafla.
Asante Niishie Hapo kwa sasa

Sent using Infinix hot 4
 
Nimeandika kwa ufupi maana hii kitu ni deep sana View attachment 1049176
blackmagic-1.jpg


Sent using Infinix hot 4
 
Hiyo point #4, ya kufufua wafu inahitaji ufafanuzi zaidi ili nikuelewe au tukuelewe.

Ni wafu wa kimwili au kiroho/kiimani??
Mi nadhani hakuna kufufua aliyekufa kibaiologia labda tofauti na hapo, bali kunawezekana kufufua mwili (yani mfano spirit za kishetani zinavaa mwili wa aliyekufa). So unaweza kutana mtu udhani kafufuka lkn ni mwili tu unaongozwa na usichokiona.
Just opinion.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nadhani hakuna kufufua aliyekufa kibaiologia labda tofauti na hapo, bali kunawezekana kufufua mwili (yani mfano spirit za kishetani zinavaa mwili wa aliyekufa). So unaweza kutana mtu udhani kafufuka lkn ni mwili tu unaongozwa na usichokiona.
Just opinion.

Sent using Jamii Forums mobile app


Aje Damaso afafanue hapa ufufuo alioutaja ulikuwa na maana gani?.
 
Ufufuo wa black magic ni ule wa kuita mfano wa mwili wa mtu katika roho sio katika mwili halisi. Yaani kupitia spells zao wanaweza kufanya ufufuko wa kiroho wa mfu aliyekwisha kufufuka.

Sent using Infinix hot 4
 
Kuhusu ishu ya namna au njia za kufanya uchawi huu Kiukweli siwezi kuelekeza maana wenyewe wana msemo wao kuwa "To suppress one within The group you need to have same knowledge" yaani kama ukitaka kupambana na black magic basi lazima uwe na ujuzi wa kiruu hii hakuna sehemu yoyote ambayo White magic inaweza kuzuia athari za black magic.

Sent using Infinix hot 4
 
kwenye castle wrd yani krne za zamani huko watu walikuwa wanaamini sana magic ,inasemekana kuna watu waliozaliwana vipawa hvyo ni gift kutoka wa sir god na hii ni kama karama ambayo hata ssa watu wanazo mnawaita wachungaji hii ndio white magic mtu hachagui kuwa nayo inamchagua na kuitumia kwa manufaa yake na y wengine
lakini black magic inaweza kuwa missuse of white magic yan blessed/gifted person akatumia karama yake in evil way pia inaweza ikawa kwa kununua kupewa au kuiba majic
simulizi za zamani za cameloth na king Urthur and the round table zipo kinaga ubaga juu y haya mambo ukushindwa kusoma vitabu angalia hata series ya merlin
utaelewa
 
kwenye castle wrd yani krne za zamani huko watu walikuwa wanaamini sana magic ,inasemekana kuna watu waliozaliwana vipawa hvyo ni gift kutoka wa sir god na hii ni kama karama ambayo hata ssa watu wanazo mnawaita wachungaji hii ndio white magic mtu hachagui kuwa nayo inamchagua na kuitumia kwa manufaa yake na y wengine
lakini black magic inaweza kuwa missuse of white magic yan blessed/gifted person akatumia karama yake in evil way pia inaweza ikawa kwa kununua kupewa au kuiba majic
simulizi za zamani za cameloth na king Urthur and the round table zipo kinaga ubaga juu y haya mambo ukushindwa kusoma vitabu angalia hata series ya merlin
utaelewa
Nimewahi kusoma kitabu kimoja cha mwandishi fulani anadai kuwa king arthur aliwahi kufanya mahojiano na baadhi ya jamaa wanaofanya black magic na kudai kuwa ilitumwa spell lazma inakuwa effective sana. Na wengi walikuwa wanapewa ushawishi wa kufanya missue ya gifts au karama zao za magic (White magic). Mfano mzuri ni wale watabiri kwa kutumia tarrots card pamoja na fortune tellers hawa ndo wanaofanya White magic.

Sent using Infinix hot 4
 
Uchawi ndio ule ule tu inategemea unautumiaje.
Haujakosea ila kutokana na dhumuni la matumizi ndo panapotokea uchawi mweusi pamoja na mweupe.
Mfano mzuri unakumbuka kipindi wale wachawi wa Taifa la Urusi waliokwenda kumuombea dua rais pamoja na dunia. Sasa wale na baadhi ya fortune tellers ni White magicians ila kama kuna mtu anayedhuru kiumbe chochote au binadamu yoyote huyo hawekwi kwenye kundi hili la White magic bali huyo ni black magicians.
I hope umenielewa kidogo mkuu.

Sent using Infinix hot 4 lite
 
Haujakosea ila kutokana na dhumuni la matumizi ndo panapotokea uchawi mweusi pamoja na mweupe.
Mfano mzuri unakumbuka kipindi wale wachawi wa Taifa la Urusi waliokwenda kumuombea dua rais pamoja na dunia. Sasa wale na baadhi ya fortune tellers ni White magicians ila kama kuna mtu anayedhuru kiumbe chochote au binadamu yoyote huyo hawekwi kwenye kundi hili la White magic bali huyo ni black magicians.
I hope umenielewa kidogo mkuu.

Sent using Infinix hot 4 lite
Sawa ila vp uliposema kwamba uchawi mweupe hauwezi kuzuia athari za uchawi mweusi? Maana kama tunakubaliana kuwa haya majina ya Black na white ni tofauti za matumizi tu ila uchawi ni uleule iweje useme uchawi mweupe hauwezi kuzuia athari za uchawi mweusi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom