Binti yako akipata ujauzito nyumbani utafanyaje?

Binti yako akipata ujauzito nyumbani utafanyaje?

shalet

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2013
Posts
3,441
Reaction score
3,613
Habari zenu

Kuna binti ni ndugu yetu tulimchukua baada ya wazazi wake wote kufariki, shule alikuwa hataki ada ya mtihani alikula so matokeo hayakutoka tukaona isiwe shida tumsaidie kwenda baraza kucheki ana zero so hawezi endelea tukasema atulie home then next year arudie tena manake muda ushaenda.

Kumbe ni mjazito na alikaa kimya bila kutuambia mpaka siku ya kujifungua na kwa vile home tulikuwa hatushindi naye mara nyingi ilikuwa vigumu kugundua sasa shida inakuja kuwa kashazaa tayari na tulipanga tusimuulize chochote kuhusu huyo mzazi mwenzie na yeye kakausha tu huku kila siku wakitumiana picha na hicho ki looser chake.

Sasa wasiwasi wetu huyu binti atatujazia timu ya mpira nyumbani kwani haonyeshi ku regret hata kidogo wala mpango wa kumtambulisha huyo mpenzi wake.

Naombeni ushauri tumchukulie hatua gani huyu binti.

NB: Tulifikiria tumrudishe kwenye nyumba ya wazazi wake na tumpe mtaji mdogo wa kupika vitafunwa ajitegemee hii imekaaje.
 
Mkuu habar? Hebu iandike thread yako kwa kuzingatia kanuni na taratibu za uandishi..nnamaanisha, weka vituo kweny sentence zako.
 
Mlifanya makosa kutomuuliza mzaz mwenzie ana plan nae gan
 
Mwacheni afundishwe na ulimwengu...
 
Mfungieni kwenye gunia mkamtupe mtoni.

Mkiendekeza huo ujinga wake wengine kwenye hiyo familia wataiga kwa kuona ni sawa alichokifanya.

Kama ameshindwa kujiwajibisha, awajibishwe.
 
Mlifanya makosa kutomuuliza mzaz mwenzie ana plan nae gan



haya sasa wafanye nini ? nadhani ndicho mtoa mada anahitaji,kuainisha kosa lake hakutamsaidia.
 
Mlikosea kuchukulia poa toka mwanzo.

tulijua ataomba msamaha sasa yupo kimya na vile tulimpa na vizawadi basi anaona alichofanya ni kizuri.
 
Mkuu habar? Hebu iandike thread yako kwa kuzingatia kanuni na taratibu za uandishi..nnamaanisha, weka vituo kweny sentence zako.

So katika thread nzima we umeona vtuo tu.... acha ujivuni na ligi zisizo na maana mkuu
 
Sumu

kwa kweli tunafikiria kumtia adabu huyo mtu wake hajaleta hata sabuni afu bado naona wanawasiliana tu!
ila hapo kwenye blue ni kinyume na ubinadamu.
 
Last edited by a moderator:
Sumu

Samahani Sumu ila ushauri wako kila uzi unaocomment unanipa mashaka...wewe mkurya??😕
 
Last edited by a moderator:
Muulizen tena muwe wakali sana... mchape mpka amtaje muhusika... muhusika aje na aseme ana Mpango gani na mdogo wenu, ikibid mlazimishen amuoe kinguvu ndo dawa yao
 
So katika thread nzima we umeona vtuo tu.... acha ujivuni na ligi zisizo na maana mkuu

Kamwe hutoweza kujifunza usipokubali makosa..Leo kafanya hvyo hapa, kesho ataandika application letter kwa mtindo huu., je hajakosa kazi hapo??..ww ndio uache ligi zisizo na maana...fikiri kabla ya kutenda mkuu.
 
...kosa la kwanza kapata mimba na kuzalia nyumbani.
..then hataki kufanya chochote, si shule wala kazi..aaah!
..huyo keshakua mzigo tayari..!
 
Kamwe hutoweza kujifunza usipokubali makosa..Leo kafanya hvyo hapa, kesho ataandika application letter kwa mtindo huu., je hajakosa kazi hapo??..ww ndio uache ligi zisizo na maana...fikiri kabla ya kutenda mkuu.

Acha uzembe mtoa uzi he is in need, anahitaji ushauri wako sio kumsahihisha kiswahili... amini mm ni mpuuzi tu aneweza chunguza makosa ya uandishi katika stuation hiyo ya mleta maada
 
Hako kajamaa kake naona kameokota dodo kwenye mpera, yani kamezalisha mtoto wa watu na hakajapata usumbufu wowote na bado kanachat nae!! kanasubiri akaze kaze mgongo kakampe mimba nyingine!


Acheni kuchukulia poa hilo jambo ndugu mbaneni huyo binti awaoneshe huyo muhuni, ili mjue ana malengo gani na huyo mwanenu Ohooo!!!
 
Muulizen tena muwe wakali sana... mchape mpka amtaje muhusika... muhusika aje na aseme ana Mpango gani na mdogo wenu, ikibid mlazimishen amuoe kinguvu ndo dawa yao

tulifikiria hivyo shida inakuja tutatakiwa kusimamia kila kitu na kuhakikisha wanaishi sawa tukaghairi.
 
Back
Top Bottom