Naombeni ushauri wenu kuhusu huyu binti aliyepewa ujauzito akiwa kwangu

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,702
36,143
Habari!

Mwezi wa pili alikuja mtoto wa dada yangu kutoka mkoa wa X kuja Dar kutembea.

Inavyoonyesha alikuwa na lengo la kuja kukaa kwa ndugu yetu (mama mdogo) ila maza mdogo alichomoa mkeka kwa kumwambia kuwa amesafiri na atamtafuta pindi atakaporudi.

Hajapokea tena simu mpaka leo.

Kwa scenario hiya binti akaja home kunitembelea akitokea kwa dada yake ambaye asingeweza kukaa naye kwa muda mrefu kwasabu ya kimazingira (dada yake kaolewa na wamepanga chumba kimoja).

Alikaa kwangu kama wiki hivi, kwakuwa wife alikuwa ana mwezi mmoja au miwili hivi ajifungue ikabidi nimuulize kuwa atabaki amsaidie shangazi yake kipindi cha kujifungua na baada ya kujifungua au nitafute mtu mwingine yeye anapita tu?

Akasema atakaa home asaidie kazi. Nikamwahidi kuwa wife akitengamaa nitampa mtaji asirudi mkoa kukaa tu au nitamtafutia kazi viwandani maana kwa elimu yake hakuna ofisi ya kumwajiri(std 7). OK maisha yakaendelea.

Issue iko hivi ; Binti kamaliza mwezi tu tayari kapigwa mimba na kijana wa jirani yangu. Kijana ni jobless anakula na kulala home.

Maza wake binti ambaye ni dada yangu nilipomweleza hakulipa uzito hili jambo.

Nilidhani ataungana na mimi tumpeleke binti nyumbani kwa kijana akaishi huko kama mwanzo wa ndoa lakini alitaka binti abaki kwangu mpaka ajifungue.

Hii May mimba ya binti ina miezi 2 .

Nawaza nichukue maamuzi magumu kumpeleka kwa kijana kama ndoa ya kimila au nimpe nauli arudi kwa wazazi wake.

Kijana na wazazi wake wamekubali kuwa mzigo ni wao .

Vipi wakuu nifanyeje hapo?

Asanteni
 
Mwenye jibu sahihi ni wewe kuliko mtu mwingine kwa maana unawaona. Fanya assesment uone kama huyo kijana anaweza kujiongeza in the future au ni kilaza hamna mpambanaji hapo.

Na ukiona wanapendana mchimbe mkwara kuwa mkali, ila hujasema binti ana umri gani hope ni 18+ na hata kama hajafika hata 16 anaolewa kwa makubaliano ya wazazi.

Ukimuacha mtaani na elimu yake std 7 na mjini hana hata nusu mwaka unatafuta mnyororo wa balaa kwake na mtoto wake.

Otherwise kama haiwezekani mrudishe kijijini. Unaona sasa kwanini mamdogo alikula kona? Ulikuwa mtego huo sasa umenasa wewe.
 
Mkuu muulize kwanza binti (yako)kama yupo tayari kuwa mama,jibu atakalotoa ndio litakupa mwanga kwa kuanzia, binafsi kutokana na jinsi ulivyoekezea hapa..

Kesho binti huyu angekua mlangoni mwa Maria stopes clinic, she's to young kuwa mama,then angepewa ile injection ya 6mths ,baada ya hapo shule ,ni muhimu afike 0 level
 
Habari!
Mwezi wa pili alikuja mtoto wa dada yangu kutoka mkoa wa X kuja Dar kutembea. Inavyoonyesha alikuwa na lengo la kuja kukaa kwa ndugu yetu (mama mdogo) ila maza mdogo alichomoa mkeka kwa kumwambia kuwa amesafiri na atamtafuta pindi atakaporudi. Hajapokea tena simu mpaka leo.
Kwa scenario hiya binti akaja home kunitembelea akitokea kwa dada yake ambaye asingeweza kukaa naye kwa muda mrefu kwasabu ya kimazingira (dada yake kaolewa na wamepanga chumba kimoja).
Alikaa kwangu kama wiki hivi, kwakuwa wife alikuwa ana mwezi mmoja au miwili hivi ajifungue ikabidi nimuulize kuwa atabaki amsaidie shangazi yake kipindi cha kujifungua na baada ya kujifungua au nitafute mtu mwingine yeye anapita tu?
Akasema atakaa home asaidie kazi. Nikamwahidi kuwa wife akitengamaa nitampa mtaji asirudi mkoa kukaa tu au nitamtafutia kazi viwandani maana kwa elimu yake hakuna ofisi ya kumwajiri(std 7). OK maisha yakaendelea.
Issue iko hivi ; Binti kamaliza mwezi tu tayari kapigwa mimba na kijana wa jirani yangu. Kijana ni jobless anakula na kulala home. Maza wake binti ambaye ni dada yangu nilipomweleza hakulipa uzito hili jambo.
Nilidhani ataungana na mimi tumpeleke binti nyumbani kwa kijana akaishi huko kama mwanzo wa ndoa lakini alitaka binti abaki kwangu mpaka ajifungue.
Hii May mimba ya binti ina miezi 2 .
Nawaza nichukue maamuzi magumu kumpeleka kwa kijana kama ndoa ya kimila au nimpe nauli arudi kwa wazazi wake.
Kijana na wazazi wake wamekubali kuwa mzigo ni wao . Vipi wakuu nifanyeje hapo?
Asanteni
Putin
 
Mpeleke kwa aliyempachika mimba kwasababu unapokaa nae wewe aliyempachika mimba pamoja na wazazi wake watakuwa wamekupa mzigo wao wakiendelea kuserebuka, kila mtu abebe mzigo wake
 
Huyo alobeba mimba ni mkubwa. Aende wakalee mimba na mwenzie na kujiandaa kupokea mtoto wao

Wewe kuendelea kukaa na huyo binti ni kumharibia familia yake aliyoanza kuijenga

Ila umwambie kabisa HAKUNA KUACHANA
Wala ASIWAZE KURUDI KWA ANKO 🙄
 
Mpe binti nauli arudi kwao kwanza itakua salama kwake kujifungua na kulea mtoto , huyo kijana hajawa tayari kwa majukumu (sijua umri pia) hawa watu walikulana kwa tamaa hawakujua effect ya mbeleni kitendo cha kumkabidhi huyo binti kwa huyo kijana kinaweza kuzaa unyanyasaji maana ataona kama amemwongezea ugumu wa maisha wakati walitafuta pamoja hiyo mimba.

Pia familia za kiswahili ni changamoto sana huyo kijana umeshasema ni jobless bila shaka atakua nyumbani kwao ! Haya unawaongezea mtu mwingine hapo hapo ni mjamzito.

Huenda wasimpige , wasimfukuze lakini watamwumiza sana kisaikolojia kwa kumsema sema hata pembeni.

Ukizingatia mimba pia zinakuaga na masharti mara sili hiki , harufu hizi sizitaki.

Nimezungumzia negativity tu ila kiasi kikubwa uhalisia wa maisha yetu ya kibongo ndo ulivyo

Pole sana !
 
Habari!
Mwezi wa pili alikuja mtoto wa dada yangu kutoka mkoa wa X kuja Dar kutembea. Inavyoonyesha alikuwa na lengo la kuja kukaa kwa ndugu yetu (mama mdogo) ila maza mdogo alichomoa mkeka kwa kumwambia kuwa amesafiri na atamtafuta pindi atakaporudi. Hajapokea tena simu mpaka leo.
Kwa scenario hiya binti akaja home kunitembelea akitokea kwa dada yake ambaye asingeweza kukaa naye kwa muda mrefu kwasabu ya kimazingira (dada yake kaolewa na wamepanga chumba kimoja).
Alikaa kwangu kama wiki hivi, kwakuwa wife alikuwa ana mwezi mmoja au miwili hivi ajifungue ikabidi nimuulize kuwa atabaki amsaidie shangazi yake kipindi cha kujifungua na baada ya kujifungua au nitafute mtu mwingine yeye anapita tu?
Akasema atakaa home asaidie kazi. Nikamwahidi kuwa wife akitengamaa nitampa mtaji asirudi mkoa kukaa tu au nitamtafutia kazi viwandani maana kwa elimu yake hakuna ofisi ya kumwajiri(std 7). OK maisha yakaendelea.
Issue iko hivi ; Binti kamaliza mwezi tu tayari kapigwa mimba na kijana wa jirani yangu. Kijana ni jobless anakula na kulala home. Maza wake binti ambaye ni dada yangu nilipomweleza hakulipa uzito hili
"Wazazi wa kijana wamekubali mzigo ni wao"!

Unasubiri nini!?mpeleke kwa huyo kijana na wazazi wake wewe!

Toa taarifa nyumbani kuwa amechukuliwa na kijana maana huyo si mtoto tena ndio maana kabeba mimba!

Simple logic tu!
 
Back
Top Bottom