Binafsi nimesikitika sana kwa tabia iliyozuka ya Waziri anakuwa na mamlaka ya kutumbua watumishi bila kufuata utaratibu

Koryo2

JF-Expert Member
Nov 28, 2016
2,056
2,515
Leo katika kipindi cha magazeti yetu asubuhi nilisikia taarifa ya kutumbuliwa watumishi sita wa Mwaruwasa- Morogoro na Mhe. Waziri wa Maji.

Binafsi nimesikitika sana kwa tabia iliyozuka ambapo Mhe. Waziri anakuwa na mamlaka ya kutumbua watumishi bila kufuata utaratibu uliowekwa katika Utumishi wa Umma.

Kusimamishwa kwa mtumishi wa umma kuna taratibu zake. (1) Kwanza kuletewa tuhuma dhidi yake (2) Mtuhumiwa kujibu tuhuma alizoplekewa (3) Kuona kama kuna kosa na hatua za kuchukua dhidi ya mtuhumiwa.(4) Kama kusimamishwa/kufukuzwa kazi basi mtuhumiwa anayo nafasi ya rufaa kwenye ngazi za juu.

Sheria zipo lakini hazifuatwi hivi tuko nchi gani hii ambayo hata sheria hazifuatwi?. Wabunge ndo wanaotunga hizi sheria akiwemo Mhe. Waziri lakini baadaye wanazikiuka.

Katibu Mkuu wa Utumishi wa Umma yupo na anajua fika taratibu na yeye yuko kimya. Acheni uonevu dhidi watumishi wa umma.
 
Waziri ni mwakilishi wa Rais, nina imani sheria inamruhusu kulingana na hasara inayoweza kusababishwa na mtuhumiwa kwa kuruhusu kufuatwa taratibu huku akiendelea kuwepo kazini.
 
Mimi nasema...tumechoshwa na ubabaishaji ! Fedha zinatolewa watendaji na wasimamizi wanasiguana hukohuko huku miradi ikikwamishwa na wao.
Kukosa maji kwa muda mrefu na changamoto mbalimbali zinakera jmn

Acha sheria zivunjwe ili haki zitafutwe lkn wababaishaji tyr wakiwa kando ya mradi.
 
Mimi nasema...tumechoshwa na ubabaishaji ! Fedha zinatolewa watendaji na wasimamizi wanasiguana hukohuko huku miradi ikikwamishwa na wao.
Kukosa maji kwa muda mrefu na changamoto mbalimbali zinakera jmn

Acha sheria zivunjwe ili haki zitafutwe lkn wababaishaji tyr wakiwa kando ya mradi.
Waziri yuko sahihi acha atumbue.
Sheria inapande mbili. Wanafukuzwa na kama wao ni wanaume waende mahakamani wakiwa nje ya mradi
Wakishindwa mahakani ndiyo wataiona joto ya jiwe.
Wakishinda hiyo ni shangwe.
Lakini sehemu kubwa ni wao kushindwa na kulipa hasara yote.
 
  • Thanks
Reactions: 1gb
Leo katika kipindi cha magazeti yetu asubuhi nilisikia taarifa ya kutumbuliwa watumishi sita wa Mwaruwasa- Morogoro na Mhe. Waziri wa Maji. Binafsi nimesikitika sana kwa tabia iliyozuka ambapo Mhe. Waziri anakuwa na mamlaka ya kutumbua watumishi bila kufuata utaratibu uliowekwa katika Utumishi wa Umma. Kusimamishwa kwa mtumishi wa umma kuna taratibu zake.(1) Kwanza kuletewa tuhuma dhidi yake (2) Mtuhumiwa kujibu tuhuma alizoplekewa (3) Kuona kama kuna kosa na hatua za kuchukua dhidi ya mtuhumiwa.(4) Kama kusimamishwa/kufukuzwa kazi basi mtuhumiwa anayo nafasi ya rufaa kwenye ngazi za juu. Sheria zipo lakini hazifuatwi hivi tuko nchi gani hii ambayo hata sheria hazifuatwi?. Wabunge ndo wanaotunga hizi sheria akiwemo Mhe. Waziri lakini baadaye wanazikiuka. Katibu Mkuu wa Utumishi wa Umma yupo na anajua fika taratibu na yeye yuko kimya. Acheni uonevu dhidi watumishi wa umma.
Hapa hakuna cha kusubiri kujitetea fukuza tu.
 

Attachments

  • VID-20210419-WA0046.mp4
    25.1 MB
Back
Top Bottom