Bilioni 8.75 zatengwa kukamilisha Vituo vya Afya 20 nchini

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,032
Serikali kupitia Ofisi ya Rais-TAMISEMI imeeleza kuwa katika mwaka wa fedha 2023/24 imetenga jumla ya Shilingi Bilioni 8.75b kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya 20 katika Halmaashauri nchini

Akizungumza Bungeni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais–TAMISEMI, Festo J. Dugange amesema fedha hizo zitatumika kwa ajili ya ujenzi, upanuzi na ukamilishaji wa vituo vya afya ambapo vituo vya Afya vya Rukaragata, Kalenge na Nyabusozi ni miongoni mwa vituo vya muda mrefu na miundombinu yake inahitaji maboresho kulingana na mahitaji ya sasa.

Nduganga emesema Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo imetengewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya upanuzi wa vituo vya afya viwili kati ya vitatu vyenye mahitaji.

Aidha, Dkt. Dugange amesema Utaratibu wa kutenge bajeti kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa vituo vya afya chakavu ni endelevu.
 
Kwa kasi ya ujenzi wa Taifa chini ya SSH, akiamua azindue Kila kitu yeye mwenyewe, anahitaji miaka mitano bila kukaa ofisini akipita mradi mmoja baada ya mwingine.

Nimefuatilia TV hivi karibuni, Kila mahala, Kila siku, panazinduliwa miradi ya maji, Kila Kona ya nchi.
 
Kwa kasi ya ujenzi wa Taifa chini ya SSH, akiamua azindue Kila kitu yeye mwenyewe, anahitaji miaka mitano bila kukaa ofisini akipita mradi mmoja baada ya mwingine.

Nimefuatilia TV hivi karibuni, Kila mahala, Kila siku, panazinduliwa miradi ya maji, Kila Kona ya nchi.
NI jambo jema anapaswa kuwa mkali na kuwachukulia hatua kali wale wote wanaofuja na kuhujumu miradi hii
 
Back
Top Bottom