Itakumbukwa kwamba wiki karibu mbili zilizopita, wakili mmoja kijana wa mjini Arusha alitiwa mbaroni kutokana na kukutwa na takribani shilingi bilioni 18 kwenye akaunti yake ya ndani na uchunguzi wa awali umehusisha fedha hizi na shughuli haramu na sasa wakili huyo ameshafikishwa mahakamani na kusomewa mashitaka yake.
Habari zilizopatikana hivi karibuni zinadai kwamba fedha hizi, ambazo zinahusishwa na shughuli haramu za maharamia na kikundi cha Al Shabaab, zina mkono pia wa mmoja wa wanaowania kuteuliwa kugombea urais wa nchi hii kwa tiketi ya chama kimoja kikubwa, katika uchaguzi wa mwaka 2015.
Inasemekana kwamba wakili huyu na mgombea huyu ni pete na chanda na mara nyingi amekuwa akimtumia katika masuala kadhaa yanayohitaji nguvu ya kifedha, kama vile michango ndani ya chama na hata shughuli za kiimani.
Sasa kama fedha haramu zinaruhusiwa kuingia katika utafutaji wa madaraka, mtu huyu akiingia madarakani, vitendo hivi haramu si vitahalalishwa?
Habari zilizopatikana hivi karibuni zinadai kwamba fedha hizi, ambazo zinahusishwa na shughuli haramu za maharamia na kikundi cha Al Shabaab, zina mkono pia wa mmoja wa wanaowania kuteuliwa kugombea urais wa nchi hii kwa tiketi ya chama kimoja kikubwa, katika uchaguzi wa mwaka 2015.
Inasemekana kwamba wakili huyu na mgombea huyu ni pete na chanda na mara nyingi amekuwa akimtumia katika masuala kadhaa yanayohitaji nguvu ya kifedha, kama vile michango ndani ya chama na hata shughuli za kiimani.
Sasa kama fedha haramu zinaruhusiwa kuingia katika utafutaji wa madaraka, mtu huyu akiingia madarakani, vitendo hivi haramu si vitahalalishwa?