Bileku mpasi

Bileku mpasi

kilimasera

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
3,068
Reaction score
277
KWA wapenzi wa muziki watakumbuka kuwa bendi ya Empire Bakuba ilianzishwa na watu watatu, marehemu Joseph Kabasele Yampanya 'Pepe Kalle', Papy Tex na Dilu Dilumona miaka ya 1970.
Lakini, pamoja na bendi hiyo kuasisiwa na watatu hao na baadaye kupewa nguvu na Jojo Ikoma, ni vigumu kutaja mafanikio yake bila kumhusisha Djouna Mumbafu ‘Bikelu Mpasi’ a.k.a Big One.
Bileku, aliyezaliwa na kupewa majina ya wazazi wake, Bileku Jean-Pierre Matonet, aliweza kuifanya Bakuba ije juu ‘kinoma’.
Pamoja na ukweli kuwa alichukuliwa na Pepe Kalle kama dansa na rapa wa bendi hiyo, Bileku Mpasi aliweza kupanda haraka na kuwa maarufu, pengine hata zaidi ya waasisi wenyewe.
Kupanda kwake kwa mafanikio kulitokana na umahiri wake wa kucheza, kurapu na baadaye kuimba, kiasi kwamba, Pepe Kalle alifikiria kumpa nafasi ya hisa zake katika bendi hiyo.
Pepe Kalle, alitokea kumpenda na kumuamini Bileku Mpasi, kama alivyofanya marehemu Franco kwa marehemu Madilu Systems, enzi za uhai wao walipokuwa pamoja T.P OK Jazz.
Jitu hilo la miraba minne, hakumpenda bure kijana huyo, bali ni kutokana na kujituma na kuifanya Empire Bakuba iliyoanzishwa kutokana na jina la moja ya makabila ya nchini Zaire (DR Congo ya sasa), ‘kufunika’ sana enzi za uhai wake.
Kasi yake ya kucheza na kurapu kwa wakati mmoja, ndiyo kwa sasa imekuwa ikiigwa na marapa mbalimbali wa makundi ya muziki wa Lingala, kuanzia DR Congo, Congo Brazaville hadi Bongo.
Enzi zake, mkali huyo alikuwa akichuana na nyota kama Robert Ekokota Wenda wa Wenge Musica BCBG kabla ya kuibuka wengine kadhaa waliofuata nyayo zao.
Wapo wengine wanaodai kuwa, Bileku Mpasi ndiye muasisi wa ‘Ma-Atalaku’ waliouibua nchini Congo na kufanya muziki wa Lingala ama Bolingo kuchangamka mno.
Ukali wake na ushirikiano aliokuwa nao na mbilikimo Emorro na baadaye Djuma Fatembo na Jolly Bebe, kulimfanya Bileku kuzidi kuwa juu na hasa kwa rapu zake matata katika albamu mbalimbali.
Ingawa hakuna taarifa kamili juu ya historia ya mkali huyo, ambaye kwa sasa ana kundi lake binafsi la Orchestra Big One, akitamba na albamu ya Tonnerre de Brest yenye kibao cha ‘6600 Volts’, inadaiwa alizaliwa miaka zaidi ya 40 iliyopita.
Shughuli zake za muziki, alizianza mji wa Kalemi kabla ya kuibukia Kishansa miaka ya 1970 mwishoni.
Mwanzoni mwa miaka ya 1980, alikuwa akifanya shughuli zake katika bendi ndogondogo kama mnenguaji, kabla ya kuchukuliwa na Pepe Kalle na kuwa dansa na rapa wao.
Hata hivyo, kutokana na kuonesha kipaji kikubwa katika uimbaji, Pepe Kalle akishirikiana na mtunzi mahiri wa Empire Bakuba enzi za uhai wake, Papy Tex walimpika kuwa muimbaji mkali.
Hata hivyo, ukali wake na kuwafunika wawili kati ya waasisi wa kundi hilo, inaelezwa kuwa, kulimsababishia rapa huyo 'kuunda' bifu kali na Papy Tex.
Ndiyo maana, mara baada ya kifo cha marehemu Pepe Kalle Novemba mwaka 1998, kulitokea mtafaruku kama ule wa TP OK Jazz baada ya kifo cha Franco juu ya mustakabali wa bendi hiyo na Madilu.
Ilidaiwa kuwa wanamuziki waliosalia katika bendi hiyo walikuwa na nia ya kuiendeleza Empire Bakuba, ila waasisi na waliokuwa wamiliki wake, Dilumona na Papy, walianzisha zengwe baada ya kufahamika Bileku amepewa usimamizi wa hisa za Pepe Kalle.
Yeye na Gode Lufombo, waliamua kujiondoa na kuiacha Bakuba mikononi mwa mwenye nayo na kwenda kujiunga na kundi la Delta Force, ambalo lilikuwepo hata kabla ya kifo cha Pepe Kalle.
Delta Force, alikaa nao tangu mwaka 1999 hadi 2002 kabla ya kuamua kujiondoa na kuwa msanii wa kujitegemea na kufanikiwa kufyatua albamu yake ya kwanza ya ‘Tonnerre de Brest’.
Albamu hiyo ilikuwa na kibao matata cha ‘6600 Volts’, ilitolewa mwaka 2004 na kumfikisha Bileku kwenye Fainali za Tuzo za Muziki Afrika za Kora (Kora Music Awards), ingawa hakufanikiwa kubeba tuzo yoyote.
Miongoni mwa vibao vya albamu hiyo iliyompa mafanikio makubwa kabla ya kuunda Orchestra Big One inayotamba na albamu nyingine mpya ya mwaka jana ni pamoja na ‘100% TVA’, ‘6600 Volts’ na ‘Cupidon Brisé’.
Vibao vingine ni pamoja na ‘Fin Du Match’, ‘Karachiga’, ‘Nez a Nez’, ‘Mihona’, ‘Onze’, ‘Respect Pepe Kalle’, ‘Tatou’ na ‘Tonnerre De Brest’.
Bileku anayekumbukwa na Watanzania kwa kuchangia kuibua vipaji vya madansa wa Kitanzania kama kina Kokoriko aliyeshabihiana naye, marehemu Maxi Prest, Mrisho Mpasi. Ndani ya bendi yake, anaimba pamoja na mdogo wa marehemu Pepe Kalle, Ally Kale, ambaye amefanana mno kisauti na marehemu kaka yake, kiasi ukisikiliza nyimbo za kundi hilo unaweza kudhani ‘Tembo wa Afrika’ amefufuka
 
Mbona huyu sio Mzizimkavu mkuu? Huyu ni kilimasera anatumia avatar ya Mzizimkavu.


Ok!Unajua kumbe wote wamefanana tabia ndiyo maana wanatumia hadi Avatar moja. Mzizimkavu na yeye ni bingwa wa kucopy na kupaste.
 
Yanga Africa, Yangaa Umoja wa Mataifa, MABINGWA WA TANZANIA na AFRIKA MASHARIKI na KATI eeeh!. Abas Gulamali rais wa Yanga, Abas Gulamali eeeh!
 
Makala safi imetulia na imeenda shule. Muendelee kutumegea stori za hao jamaa. kusema ukweli alileta mapinduzi makubwa sana hasa kwenye kuchangamsha muziki hususani kwenye Sebene. Nakumbuka alikuwa Rapper au Atalaku bora kwa miaka mitatu mfulululizo enzi hizo Zaire.

Ile atalaku yake iliyokuja kuwashika ilikuwa baada ya kisa cha ukweli cha Emorro kuwekewa sumu kwenye kinywaji walipokuwa Angola. Sasa wakati wanahaha kumwokoa marehemu Emorro alikuwa akilalamika tumbo linamuuma mgongo unauma naomba kiti nikae.

Yeye Bileku akaghani hivi samahani kama nitakuwa nitakosea baadhi ya maneno

Mama nabeleka.......
Sheri nabeleeeka
libumu pasi
likongo pasi
pesanga kiti na vyandila

aiiii.....mama.....aiiiiii....maamaa

Tokea hapo moto wake ulikuwa balaa na labda alipokuja Ekokota wa Wenge ndiye alikuwa mpinzani wa kweli. Ila kuna kipindi baada ya Ekokota kufanyiwa operesheni ya koo Atalaku mpya wa Wenge Tutu Kaludji alibadilisha mwelekeo wa Atalaku na rappings zake za kama mtu anaimba hivi hasa kwenye mtindo wa Ndombolo.Hawa huwa wanaitwa Ma-tenorist wapo wengi kama akina BRIGADE ambaye alikuwa kwa KOFFI na WERRASON au sasa hivi LOBESO mzee wa MALEWA ya WERRASON kwetu huku wapo kama akina GREYSON SEMSEKWA.

Ila toka Werrason alipomwibua "BILL CLINTON" miaka ya mwisho ya tisini alirudisha tena heshima ya Atalaku maana Atalaku anatakiwa mtu awe na koo lililoshiba na sauti ya nguvu kweli kweli. Toka zama za BILL CLINTON mwelekeo wa Atalaku haujabadilika sana hapa kwetu kuna mtu kama KITOKOLOLO au Msafiri Diof au MIRINDA NYEUSI wanajaribu kufuata mtiririko wa BILL CLINTON.

Ila tunaweza kusema mwasisi wao alikuwa si mwingine bali ni Djouna Mombafu au maarufu kama BILEKU YA MPASI. Rafiki wa Didier Drogba ambaye alimsaidia sana kumwibua tena BILEKU na ile Album yake binafsi ya kwanza.
 
Sijapata kupenda bendi zaidi ya Empire Bakuba na Super Matimila!!! Mleta uzi huu umenikumbusha mbali sana, hasa enzi hizo nikiwa napata mbege pale Mti Mpana, Shimo la Udongo (Kurasini).
 
Natakujua hivi huu wimbo sintia ameimba nani kati ya bileku mpasi na papy tex
 
Safi sana kaka umetukumbusha mbali tunaopenda muziki, hasa vijana wa zamani. Umetuongezea siku za kuishi, ubarkiwe sana mleta thread hii.
 
Bileku ndio aliyeua Empire Bakuba mara baada ya kifo cha Pepe Kale, bend ilitakiwa iwe mikononi mwa Papy Texs
 
Back
Top Bottom