Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 18,655
- 20,988
Mnamo Mwaka 1991 Pepe Kalle na bendi yake ya Empire Bakuba walikuja Tanzania kufanya onesho katika jiji la Arusha. Walipowasili Arusha, walikodi taksi iliyokuwa inaendeshwa na mwanamama Hidaya Khamis Massawe.
Wakiwa kwenye taksi wakawa wanazungumza kilingala wakimsifia dereva bila kujua kuwa kumbe bi. Hidaya (dereva teksi) alikuwa anakijua kilingala kwani kutokana na mihangaiko yake ya kimaisha huko Zaire (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo).
Pepe Kalle akastaajabu sana kumsikia Hidaya anazungumza kilingala. Alipomaliza onesho lake Arusha, Pepe Kalle akajiapiza kurejea Tanzania kwa ajili ya Hidaya.
Mwaka uliofuata, 1992, Pepe Kalle akarudi kweli Tanzania Arusha na akatunga wimbo kwa ajili ya Hidaya. Mume wa Hidaya, Mzee Massawe, alipong'amua kuwa ule wimbo "Hidaya" umetungwa mahsusi kwa ajili ya mke wake, akamtaliki siku hiyo hiyo.
Hidaya Khamis Masawe alifariki mwaka 2021 Arusha, mtaa wa Kaloleni.
Wakiwa kwenye taksi wakawa wanazungumza kilingala wakimsifia dereva bila kujua kuwa kumbe bi. Hidaya (dereva teksi) alikuwa anakijua kilingala kwani kutokana na mihangaiko yake ya kimaisha huko Zaire (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo).
Pepe Kalle akastaajabu sana kumsikia Hidaya anazungumza kilingala. Alipomaliza onesho lake Arusha, Pepe Kalle akajiapiza kurejea Tanzania kwa ajili ya Hidaya.
Mwaka uliofuata, 1992, Pepe Kalle akarudi kweli Tanzania Arusha na akatunga wimbo kwa ajili ya Hidaya. Mume wa Hidaya, Mzee Massawe, alipong'amua kuwa ule wimbo "Hidaya" umetungwa mahsusi kwa ajili ya mke wake, akamtaliki siku hiyo hiyo.
Hidaya Khamis Masawe alifariki mwaka 2021 Arusha, mtaa wa Kaloleni.