Bila maamuzi magumu kutoboa kupitia kuajiriwa nitakusikia tu kwenye bomba Ajira za afya michosho tu sifa mtaani tu ila hela hamna

Bila maamuzi magumu kutoboa kupitia kuajiriwa nitakusikia tu kwenye bomba Ajira za afya michosho tu sifa mtaani tu ila hela hamna

aya maisha bwana yana kejeli zake ambazo zinatafakarisha sana.

Kila mtu ana maana yake kwenye haya maisha na ana aina ya picha ambayo anayokichwani kwamba nikipata kike na kile basi nimetoboa,ni hudhuni sana.

pole kwa masikitiko mkuu

kwa upande wangu nikiweza kuhudumia familia yangu,kuwa na usafiri wangu na ka hidden roof ka vyumba 5 kanatosha sana.

uku nikiwa naangalia kuku na mbuzi wangu wakizaliana uku watoto wangu wakicheza pembeni ya bustani ya mboga mboga.
 
Kwanza mtu anae tegemea hizi ajira za serikali na za wabongo tayari kwa 50% ni masikini wa akili, wengi wanajipa matumaini ya kupiga pesa za Rushwa perdium na ubadlifu au wizi, Jomba huwezi kutoboa na pesa ya rushwa au perdium labda uwe mkurungezi wa wizara au katibu mkuu, eti mualimu nesi famasia, police, mtendaji wa mtaa, teller nk. utakufa masikini subiri ufikishe umri wa kustaafu ndo utajua kwamba ulichezea mda wako.
😂😂😂😂
 
Ni umasikini mkuu tu kweli wewe ulipwe 450k kwa maisha ya Dar es salaam una familia unapanga unaishi je, kama sio umasikini wengine tungekua na wazazi wenye uwezo bora urudishe majeshi kwa wazazi yuishi kama hao waarabu koko wa kariakoo baba mama shangazi watoto mke wote sehemu moja
Mbavu zangu mie, 😂😂😂
Ila waja.
 
Anzisha Biashara ukiwa humo humo kwenye ajira hadi hiyo biashara ianze kukupa return mara 5 au zaidi ya unachopata kwenye ajira usithubutu kuacha kazi akakimbilia kujiajiri.
Kujiajiri hakutaki watu legelege utaishia kuongea mwenyewe barabarani.
Hata ukiona mtu anachoma mahindi barabarani ujue yupo smart masna siikila mtu anaweza kufanya hivyo
Ila watu, 😂😂😂
 
Tuseme unalipwa 800k kila mwezi.
Kodi 100k kwa mwezi
Kula 300k kwa mwezi
Nauli 100k kwa mwezi

Jumla 500k kwa mwezi kwa matumizi binafsi

Imebaki 300k, hii unaweza kuiwekea bajeti ya mambo ingine kama akiba, mavazi, uwekezaji, kujiendeleza kielimu, nk.

Hii pesa ukitulia kwenye ajira kwa miaka 10 una uwezo wa kuestablish financial stability kubwa sana.

Epuka matumizi yasiyokuwa ya lazima.
1. Starehe
2. Kuhonga ndugu, jamaa, na marafiki
3. Kama unataka kuanzisha familia hakikisha unaeanzisha nae familia ana uwezo wa kujitegemea kiuchumi.
4. Epuka kuzaa bila malengo.

Mshahara wa mtu mwenye diploma au degree aliyeajiriwa serikalini unatosha sana kuanzia maisha na Kutengeneza financial stability.
Mbona hesabu zinagoma kabisaa hapa, kuna dharura za magonjwa, vifo, etc.
 
MAISHA YA KUAJIRIWA NI UTUMWA
ndio maana unaitwa CIVIL SERVANT
au mtumishi wa UMA kama vile house girl au house boy ..anavyoitwa mtumishi wa ndani ndivyo wanavyoitwa watumishi wa uma

kama wanavyoitwa wafanyakazi za ndani ndivyo wanavyoitwa watumishi wa serikali..

hasa maskini wanyonge madaktari na walimu...ambao hawana marupu rupu na posho..

tofauti na baadhi ya watumishi wenye posho nyingi allowances nyingi nyingi ambao hawategemei mshahara kivile..

MBAYA ZAIDI
1.unatumia masaa mengi kushinda kazini kuliko nyumbani kama madokta ambao wanalala kabisa mahosoitali..hawaoni familia zao
Kazi tembo mshaahara sisismizi.

2.SIfa za kijinga KUITWA CHIFU CHIFU...na wakati mwingine ..bora hata upate hizo sifa za kijinga..Badala ya shukrani..unabebeshwa lawama na wanasiasa wanakutumia kama punching box kujichukulia ujiko...kujionyesha kuwa wanafanya kazi kwa kudhalilisha watumishi wa umma wanyonge kama madokita..


3.ukistaafu mara mafao yako wakudhulumu..wanakupa kikokotoo unapewa kiduchu..kwa bindi..
bora hata ukifika kustaafu..ukipata majanga kati kati unasahaulika fasata..mbaya zaidi kwa wale ambao huko kazini kwao wanajiona miungu watu yeye ndiye yeye ..yeye akisema ..kana kwamba bila yeye kazi za umma hazifanyiki...you are replacable usipokuwepo kazi za umma zitaendelea ..ila usipokuwepo kwenye familia yako ndio utaacha pengo ila usijipe umuhimu kwenye taasisi za uma pengo lako linazibika.
 

Attachments

  • images - 2026-03-13T000234.285.jpeg
    images - 2026-03-13T000234.285.jpeg
    12.7 KB · Views: 5
Mimi nimejiajiri, Miongoni mwa vitu huwa vinaniwia vigumu sana kumshauri mtu, ni kumwambia aache kazi akajiajiri. Sitoagi ushauri huo, sababu ni rahisi tuu.
Kila jambo lina faida na hasara, kujiajiri kuna changamoto zake kibao, kuajiriwa kuna changamoto zake kibao. kujiajiri sio kwa kila mtu.

Kuna mtu kwa nature yake tuu ni mfanyakazi, hawezi kujiajiri. Kunamtu kwa nature yake tuu ni Mfanyabiashara kwa asili. Kuna watu kibao walitaka kujiajiri, wakasanda wakarudi ofisini. 😊

Hivyo basi, Kila mtu afanye analoona ni sawa kwake na analimudu. Yupo mtu ataweza kujiajiri na yupo mtu hawezi kujiajiri na kinyume chake. Yupo mtu hawezi kuajiriwa, akiajiriwa tuu anafukuzwa kazi au asifanye kazi za watu kwa ufanisi sababu anaona sio nafasi yake. Yupo mtu akiajiriwa na kitambi kinatoka, anaenda kutoa shukrani kanisani. Anavimba na kuipenda sana kazi yake. Yupo mtu ataajiriwa atawaza amwibie mwajiri, akafanye biashara zake. Ishu ni mindset.

Nje ya mada: Mimi siwezi kuajiriwa sio sababu nabeza kazi za watu au naona walioajiriwa hawana mafanikio, hapana. Wapo watu wengi wameajiriwa wameniacha mbali sana kiuchumi na kimafanikio, ila mimi kwa nature, sipendi "shuruti".
Huwezi niambia nifanye hivi, fanya vile, nikafanya bila ridhaa. Sitawaliki kiufupi. ukiniajiri utanifukuza tuu au nitaharibu kazi maana kazi zinataka utii, jambo ambao kiukweli mimi sinao. Nina nidhamu lakini sina hali ya utii yaani shuruti.

Mimi Baba yangu aliniona nina traits za kujifanyia mambo yangu mapema sana, bila amri wala shuruti wala kupangiwa, napenda kujituma zaidi kuliko kutumwa. akanambia mapema sana maliza chuo, ujifanyie biashara zako ambazo hutaingiliwa na mtu yeyote, hutapangiwa wala kuwa chini ya mtu ambae unawajibika kwake.
Mwaka wa 12 sasa nipo kwenye biashara zangu. Nimeshapoteza pesa mara nyingi sana, nimeshafanya biashara kibao zikabuma. Nimeshafanikiwa mara kadhaa kuzijenga biashara flani na badae nikafanya makosa na zikafa, lakini kwa kuwa mimi ni wa huku, naishi biashara, bado nipo. Na pia ninazo biashara za muda wote, zinakua kila uchao pamoja na changamoto zake. Kwa hiyo hakuna kitu rahisi, jipime wewe ni wa wapi.
Usikurupuke tuu kuacha kazi, kisa umeona Joni ana biashara na hujui, anapambana na kipi.

Ushauri: Kama wewe ni mfanyakazi na unataka kweli kufanya biashara, tengeneza kwanza "side hustles" ukiwa hapo hapo kazini, ujipime kwa muda mwingi kabla ya kuingia mazima kwenye biashara. Watu kibao ni wajasiliamali na ni wafanyakazi, baadae akiimarika ndo anarusha taulo. 😁
Usikurupuke, biashara zinazaliwa, zinakua na zinaweza kufa.
 
Siku baada ya siku sioni dalili ya kutoboa kupitia haya maisha ya kuajiriwa mambo yanazidi kuwa tough familia inaanza kukua kwa mshahara huu wa single digit sina hakika kama kuna kutoboa bila kuchukua action sasa

Kinachouma zaidi kuna watu huo mshahara wako ni per diem ya siku mbili tu aisee haki iko wapi? Kusema ukweli huku kuajiriwa ni hatari sana sijasema kuajiriwa ni kubaya ila shida je unalipwa kiasi gani? Yaani kuna sehemu ukiajiriwa au kuna halmashauri ukiajiriwa unajichimbia kaburi tu kutoboa hapo sahau kabisa aisee bila maamuzi magumu kutoboa nitakusikia tu kwenye bomba yaani huku Afya mnafanya kazi kubwa ila Mshahara wenyewe kuduchuu yaani unakuta hamna semina, hamna extra duty wala pesa nje ya mshahara wewe ni kutegemea mshahara tu full stop hii haikubaliki kabisa
Nini maana ya mafanikio Kwanza?
 
Kwanza mtu anae tegemea hizi ajira za serikali na za wabongo tayari kwa 50% ni masikini wa akili, wengi wanajipa matumaini ya kupiga pesa za Rushwa perdium na ubadlifu au wizi, Jomba huwezi kutoboa na pesa ya rushwa au perdium labda uwe mkurungezi wa wizara au katibu mkuu, eti mualimu nesi famasia, police, mtendaji wa mtaa, teller nk. utakufa masikini subiri ufikishe umri wa kustaafu ndo utajua kwamba ulichezea mda wako.
Jwtz wana hela kuanzia cheo cha luten usu
 
Pole sana kwa yaliyokukuta,ila usikate tamaa, kopa angalau milioni kumi tu anza biashara ya vifaa vya electronic na simu ndani ya miaka miwili utakuwa na kama milioni 30 hivi wekeza wekeza kisha acha kazi usimamie biashara yako. Utakuja unishukuru baadae.
😂😂
 
Pesa ipo kwenye kujiajiri Tu asikudanganye mtu , kama umeajiriwa ni Bora uweke interval ya kukusanya mtaji let say miaka miwili au mitatu then Acha kazi nenda kajiajiri, angalizo ni kwamba usije ukakimbilia kujiajiri Tu kisa umeona mtu au Kwa tamaa Tu ya kutaka pesa haraka haraka bila kujipanga.

Kumbuka kwenye kujiajiri itachukua muda zaidi kujipata pengine zaidi ya ulivyotarajia lakini ukikomaa unatoboa ukiwa kijana mdogo kabisa Hadi unajilaumu kuwa siku zote ulikuwa wapi, pia kumbuka zaidi ya asilimia tisini ya waliojiajiri biashara zao hufa Kati ya mwaka mmoja Hadi mitatu, unapochukua maamuzi ya kujiajiri Ingia jumla jumla Kwa miguu yote kinyume na hapo hutoboi may be Kwa kazi zisizohitaji uwepo wako sana tena may be.

Asilimia kubwa au tuseme 97% ya waajiriwa TZ watakufa maskini, mishahara inayolipwa ni kama ya vibarua, ni watu wachache Sana wanaokula maisha...

Cha msingi usikimbilie kuacha kazi ghafla, lazima ujipange Kwanza, ujipange kimtaji (X2), ujipange kiroho na kimwili, ujipange kimaarifa....ukishajipanga sasa unachomoka bila kuangalia nyuma....

No risk no rewards, No discipline no results...kama ikikufaa zaidi tumia filosofi ya kijapani inaitwa IKIGAI (nenda Google au youtube ukaitafute).

NB: Usiombe ushauri wa kujiajiri Kwa mtu ambaye hajawahi kujiajiri...zingatia Sana Hili.
Hata kujiajiri haikuhakikishii kufanikiwa kimaisha. Hii nchi aslimia kubwa ya watu ni masikini au wanaishi maisha ya kawaida ya kupata basic needs.
 
Ni umasikini mkuu tu kweli wewe ulipwe 450k kwa maisha ya Dar es salaam una familia unapanga unaishi je, kama sio umasikini wengine tungekua na wazazi wenye uwezo bora urudishe majeshi kwa wazazi yuishi kama hao waarabu koko wa kariakoo baba mama shangazi watoto mke wote sehemu moja
Wewe wafanyakazi wako unawalipa sh ngapi?
 
Umeshagundua tatizo, Anza kutafuta namna ya kujikwamua sasa mkuu.
 
Watu wanatajirika kwa kuendeleza walipoacha wazazi wao, wewe umezaliwa Juzi tu unataka utoboe ndani ya miaka 3.

Baba na Babu yako hawajaacha kitu. Huna kipaji chochote wala bahati.
😄😄😄 Eti huna kipaji chochote Wala bahati
 
Back
Top Bottom