Big Brother Africa 2014 (Hot Shots) - Special thread

Big Brother Africa 2014 (Hot Shots) - Special thread

Je mshindi akiwa ni Mtanzania pongezi watapewa wazazi wake au nchi anayotoka?
 
Mh! Na bendera walizonazo?? Maana naona amebeba utaifa pale
Bendera kubeba sio kigezo. Inategemea amebebaje,kama kajibebea tu alipewa na mjomba wake atajibeba.
Ili tuseme mtu amebeba bendera ya taifa ni lazima akabidhiwe na mamlaka halali mf.balozi,waziri nakadharika.
 
Subili huyo mtanzania ashinde ndio mtajua katumwa na selikali au na wazazi wake
Hapo ndipo mawazili watajitokeza na kuanza kumpamba sifa za kijinga.
 
Sitashangaa akishinda viongozi wa serikali wakijitokeza kumpongeza kuwa kaliwakilisha taifa vizuri, maana ilishatokea kwa Mwisho na Richard. Kifupi ni kwamba Tanzania ina upungufu na ukame wa mafanikio katika kila jambo kiasi kwamba hata kama leo yangeanzishwa mashindano ya (ashakum si matusi) ng.on.o mtanzania akishinda viongozi watajitokeza kumpongeza.

Kwa kifupi hayo mashindano sidhani kama Tanzania imetuma mwakilishi na kama wanapeperusha bendera za tanzania ni matumizi mabaya ya bendera ya taifa. Ila sioni ajabu, ndiyo Tanzania yetu hii tunaishi kwa mzaha tu.
 
Sitashangaa akishinda viongozi wa serikali wakijitokeza kumpongeza kuwa kaliwakilisha taifa vizuri, maana ilishatokea kwa Mwisho na Richard. Kifupi ni kwamba Tanzania ina upungufu na ukame wa mafanikio katika kila jambo kiasi kwamba hata kama leo yangeanzishwa mashindano ya (ashakum si matusi) ng.on.o mtanzania akishinda viongozi watajitokeza kumpongeza.

Kwa kifupi hayo mashindano sidhani kama Tanzania imetuma mwakilishi na kama wanapeperusha bendera za tanzania ni matumizi mabaya ya bendera ya taifa. Ila sioni ajabu, ndiyo Tanzania yetu hii tunaishi kwa mzaha tu.
Tena utashangaa zaidi mkulu wa nchi atamwita Ikulu kupata dinner pamoja nae chezea magamba weye
 
Tena utashangaa zaidi mkulu wa nchi atamwita Ikulu kupata dinner pamoja nae chezea magamba weye

Candymumie yaani ataitwa shujaa, na itasemwa kuwa ameliletea taifa heshima kubwa. Niliposikia kiongozi wa nchi anatoa pongezi kwa Richard baada ya kushinda BBA miaka kadhaa iliyopita nilijisikia aibu sana. Mambo kama yale wanayofanya yanawezaje kuliwakilisha taifa? Mtu kaenda kwa jitihada zake mwenyewe na familia yake, nina hakika wapo wengine hasa wa kike ambao inawezekana hata familia zao hazikukubaliana, leo eti analiwakilisha taifa. Kwa sababu tu kashinda?

Yaani nchi hii hata wachawi wakianzisha mashindano yao na mshindi akawa anapatikana kwa kuua watu wengi kwa mwaka nchini kwake, bado wanasiasa wa Tanzania watashangilia tu ushindi. Absolute nonsense!
 
Last edited by a moderator:
Nilivyoona last post ni wewe nikaamue nifungue huu uzi nione comment yako na nilichokikuta ndicho hicho nilichokihisi.

ROBERT MICHAEL, Matola yuko sahihi, acheni kupotosha. Hao si wawakilishi wa Tanzania. Wameenda wao kama wao na wamewakilisha familia na marafiki zao. Full stop!
 
Last edited by a moderator:
Bendera kubeba sio kigezo. Inategemea amebebaje,kama kajibebea tu alipewa na mjomba wake atajibeba.
Ili tuseme mtu amebeba bendera ya taifa ni lazima akabidhiwe na mamlaka halali mf.balozi,waziri nakadharika.

Umeniwai kumjibu mkuu
 
Haya.......leo ndio mtoano unaanza rasmi.......sijui nani ni out......
 
Back
Top Bottom