ndiyoKuna sehemu kwenye biblia kumeandikwa Yesu atakuja?
Naomba tafadhalindiyo
Anazingua huyo kila uzi anacomment hivyoAsante sana mkuu!
Itakua ndio furaha yake labda..!Anazingua huyo kila uzi anacomment hivyo
Zipo nyingi sana...Karibia Agano jipya kila kitabu..lakini mfano mmoja huu hapa kutoka kwa yesu mwenyewe..(from the horses mouth)Naomba tafadhali
Shukrani mkuu nipo hapa namsubiriZipo nyingi sana...Karibia Agano jipya kila kitabu..lakini mfano mmoja huu hapa kutoka kwa yesu mwenyewe..(from the horses mouth)
(Marko 13:1-2; Luka 21:5-6)
1Yesu alitoka hekaluni, na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake walimwendea, wakamwonesha majengo ya hekalu. 2Yesu akawaambia, “Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
Taabu na mateso
3Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, “Tuambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?” 4Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa na mtu. 5Maana wengi watatokea wakisema kila mmoja kwamba yeye ndiye Kristo nao watawapotosha watu wengi. 6Mtasikia juu ya vita na fununu za vita; lakini msifadhaike, maana hayo hayana budi kutokea, lakini mwisho wenyewe ungali bado. 7Taifa moja litapigana na taifa lingine; ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine. Hapa na pale patakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi. 8Yote hayo ni kama mwanzo wa maumivu ya kujifungua mtoto.
9“Kisha watawatoeni ili mteswe na kuuawa. Mataifa yote yatawachukieni kwa sababu ya jina langu. 10Tena, wengi wataiacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana. 11Watatokea manabii wengi wa uongo watakaowapotosha watu wengi. 12Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia. 13Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa. 14Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.
Dhiki kuu
15“Basi, mtakapoona ‘Chukizo Haribifu lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake), 16hapo, walioko Yudea na wakimbilie milimani. 17Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake. 18Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake. 19Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo! 20Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato! 21Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena. 22Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.
23“Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: ‘Kristo yuko hapa’ au ‘Yuko pale,’ msimsadiki. 24Maana watatokea akina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu. 25Sikilizeni, nimekwisha waonya kabla ya wakati. 26Basi, wakiwaambieni, ‘Tazameni, yuko jangwani,’ msiende huko; au, ‘Tazameni, amejificha ndani,’ msisadiki; 27maana, kama vile umeme uangazavyo toka mashariki hadi magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu. 28Pale ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.
Kuja kwake Mwana wa Adam
29“Mara baada ya dhiki ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa. 30Kisha, ishara ya Mwana wa Mtu itaonekana angani, na hapo makabila yote duniani yatalalamika; watamwona Mwana wa Adam akija juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi. 31Naye atawatuma malaika wake wenye tarumbeta la kuvuma sana, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, toka mwisho huu wa mbingu hadi mwisho huu
Lengo la 1 la YEHOVA lilikua binadamu tuishi duniani milele..na ndio itakavyo kua baada ya utawala wa shetaniJe, ulimwengu ukishaisha watu wake watakua wapi?
Kumbe wewe ni Mshahidi wa Yehova, utawala wa shetani utaanza lini na kufika kikomo lini?Lengo la 1 la YEHOVA lilikua binadamu tuishi duniani milele..na ndio itakavyo kua baada ya utawala wa shetani
Utawala wa shetani ulianza tangu kipindi cha adamu,kaini na mpaka sasa tupo chini yake..Kumbe wewe ni Mshahidi wa Yehova, utawala wa shetani utaanza lini na kufika kikomo lini?
Nimeona umetumia neno Yehova na pia huwa wanapenda kuzungumzia zaidi habari ya nyakati za mwishoUtawala wa shetani ulianza tangu kipindi cha adamu,kaini na mpaka sasa tupo chini yake..
utawala huo utakomeshwa pindi yesu atakapo kuja duniani.. na hizo ndio ishara za kuja kwake..
nb. kwanini umesema mimi ni shahidi wa yehova mkuu!
Kwenye biblia nyingi neno YEHOVA limetolewa kisha wakapandikiza BWANA,MUNGU jaribu kufuatilia.. sijajua maana yakutoa ilo jina ila watakua na maana yao! ila mimi natumia kwa sababu yeye mwenyewe alisema tumwite jina ilo.. na biblia inasema ilo ndio jina lake..Nimeona umetumia neno Yehova na pia huwa wanapenda kuzungumzia zaidi habari ya nyakati za mwisho
Nawe pia`Ahsante
Mbona sodoma na gomora walinyukana na dunia bado ipo.!?Kweli vyote vilitabiriwa
Kwani nani alikwambia dunia itaharibiwa? Biblia inasema Yehova hata iharibu dunia kwa moto au maji tena! napia hakuna kitu chochote kitacho iharibu dunia..Mbona sodoma na gomora walinyukana na dunia bado ipo.!?
Sasa YEHOVA anahaja gani ya kuimaliza dunia wakati tutabakia hapa hapa baada ya utawala wa shetani?Lengo la 1 la YEHOVA lilikua binadamu tuishi duniani milele..na ndio itakavyo kua baada ya utawala wa shetani
Kijana naona huelewi ,ni hivi wanavyodai,,yehova atatuma masiha kuja kuwakomboa watu wake wanaoteseka utumwani(dhambini),atapokuja masiha,atapigana,hapa lazima vita uwepo,kuuteka jerusalemu ulio mkuu,kisha baada ya ushindi,itapita miaka 1000 ya amani,hakuna kuugua,hakuna njaa,vita etc yaani full amani,Sasa YEHOVA anahaja gani ya kuimaliza dunia wakati tutabakia hapa hapa baada ya utawala wa shetani?