Michael Amon
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 8,775
- 3,610
KIKONGWE machachari kwenye tasnia ya muziki wa Bongo fleva Bibi Cheka, amesema hakukata tamaa tangu akiwa kijana, alijipa moyo kuwa siku moja kila mtu atamjua kutokana na juhudi zake binafsi.
Cheka alisema hakuna kitu anachochukia kama kusikia mtu akisema 'siwezi.' Alisema kila anapomsikia mtu akisema hivyo, humchukia maisha yake yote hasa akiwa mwanamke.
Bibi Cheka kwa sasa anatamba na wimbo wa 'Ni wewe'ambao ameimba na Mheshimiwa Temba wa Kundi la Wanaume Family chini ya Saidi Fella na yeye akiwa mmoja wa wanamuziki wa kundi hilo.
Cheka alisema kilichomfanya ajiingize kwenye kundi la Wanaume Family ni ndoto zake za siku nyingi kuwa mtu maarufu ambaye amefikia hapo kwa juhudi zake.
"Sikukata tamaa na siku zote nilitamani kila mmoja anijue na kutambua kazi yangu nikiwa mwanamke na kupitia Wanaume Family hilo limewezekana hadi wewe umekuja kuniuliza,kabla ya hapa tungeonana wapi?"Alihoji.
Bi Cheka alimalizia kwa kuwataka wanawake wenzake wamuunge mkono badala ya kumbeza na kumuona ni muhuni kwani kazi ni kazi ili mradi ni ya halali na mkono unakwenda kinywani.
"Kazi hii ya kuimba imenifanya nisiwe mzigo kwa familia kwani natatua shida zangu ndogondogo,"alisema bila kutaja alipata kiasi gani cha fedha kutokana na wimbo huo.
E-mail: meezy@youngmaster.co.tz