Bibi amuita Magufuli 'Mungu' baada ya kupewa msaada

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
40,525
Reaction score
46,612
Kusema ukweli nimeona aibu kuiangali hii video, nimesoma tu heading kwenye video, maana ni aibu ilioje kuina na kusikia binadamu mwenzako akiitwa Mungu, nimeona aibu sana. Kwa wenye ujasiri wa kuangalia naomba muangali halafu mtuhadithie. Video ipo chini hapo.
 
Hapo Jiwe anavimba kichwa hasa
 
Inasikitisha sana huyu mama masikini, matatizo ya namna hii Tanzania ni mengi sana ni vyema tukatengeneza mfumo makini wa either kusaidia watu kama hawa au kuzuia matatizo kama haya yasitokee kwenye jamii... Wanaofikiwa na Mh Raisi ni wachache kuliko wengi wasiofikiwa, tunafanyaje kuwafikia na kutoa msaada kama huu..
 
Mimi nataka kujua reaction ya mkulu ilikuaje,

Na mimi nimeogopa kuiangalia
 
Kuna Siku nilimsikia mzee wa upako akielezea jinsi Huyo mfalme alivyokufa,ni kwamba mda mchache baada ya kutoa hio hotuba yake na kusifiwa hadi kufananishwa na Mungu alianza kutokwa na funza huku huku nyama zikiacha mwili anajiona mpaka kaanguka chini na kufa.
 
Mimi nataka kujua reaction ya mkulu ilikuaje,

Na mimi nimeogopa kuiangalia
Watu wanaongozwa na chuki hapa. Bibi amepiga magoti, rais akamwambia ''inuka tu bibi'' anayestahili kupigiwa magoti ni Mungu tu''. Bibi akaongezea hata wewe ni kama mungu wa pili. Kwa kifupi rais amemjibu vizuri sana ila kutokana na uelewa wa bibi ndiyo akasema hivyo lakini siyo kweli kwamba rais alifurahia.
 
Huyo bibi atakua kilaza wa kanda hiyo
 
Huyo Mbogo ni nani na hapo ni kijiji gani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…