mastersajenti
Senior Member
- Dec 4, 2015
- 165
- 24
Nimeshangazwa sana kuona eneo la Posta Mpya kutoka Hotel ya Hall day Inn mpaka New African Hotel limegeuka eneo la biashara za kimachinga.Wakati Wa utawala Wa Awamu ya kwanza maeneo hayo yalikuwa yanaheshimiwa sana kwani ndio kioo cha mji lakini Leo hii miongoni mwa maeneo machafu no pamoja Na hayo.Muda wote utakuta maandazi chapati mahindi ya kuchemsha majiko ya kuchoma viazi mitumba wapiga debe Na makelele yao huku ofisi za serikali Na makampuni zikishindwa kufanya Kazi zao .Wakati umefika Kwa viongozi wetu kuziondoa biashara za aina hiyo Na kuzipeleka maeneo rasmi pia watu kufanya biashara pembezoni mwa majengo ya ofisi za serikali kama vile Shoe shinner Wapo Mahakama Kuu, Wizara za Ardhi ,Barabara ya kwenda Ikulu hakika inashangaza sana.Bjnafsi nimechukizwa sana Na wahusika msiporekebisha hali hii Nitamwandikia Barua ya wazi Mh.TINGATINGA msinilaumu.