Biashara ya vipuri vya pikipiki: Ushauri, michango, mawazo

marandu2010

JF-Expert Member
Aug 7, 2010
1,199
435
Boda-Boda-Riders-In-Juba2.jpg

Wakuu kwa mara nyingine tena:

Pikipiki zimeenea sana sasa hasa katika jiji letu la Dar es salaam.Hii inanifanya nione biashara ya spea za pikipiki itakuwa inalipa sana?

Sijajua upande mwingine wa shillingi. Hebu nipate mawazo yenu wakubwa.

Mna maoni gani katika hili?

Asanteni sana wakuu.

===
2.
Natumaini hamjambo wanajamii wa JF especially jukwaa hili,

Mimi ni kijana niliyeajiriwa sekta ya umma..nimeamu nijitose kwenye ujasiriamali...hasakwenye sekta ya usafirishaji hususani spea za pikipiki kama nilivyoainisha.

Kwa kuanzia nimefanya uchunguzi wa kutosha sehemu ninyaoishi ina pikipiki nyingi ila spea ndio hamna...sehemuitapatikana ila nahitaji kama kuna yeyote anaefahamu zaidi jins ya kuplan business hii anaipe some inputs.

Kama starting capital,vifaa vizur vya kuanzia kununua,bei na mengineyo.

Ninachukua mkope hivi karibuni nimeonelea bora nitimize iyo ndoto ya ujasiriamali maana uthubutu tayari ninao.

Pia niatanunua pikipiki kama 2.

Nimetenga nusu ya mkopo wangu wa 8mil ndio nianzie busness is it enough?

Asanteni.

=> Maoni na Ushauri

Pikipiki na spea zake zina soko,ila lazima ununue spea feki za china,siyo feki ila ni spea zisizo madhubuti,inalipa sana kwa mtazamo wangu hasa ktk miji midogo ,siyo Dar, kwa Dar itakulazimu uuze bei ya jumla.

100% nakuunga mkono kabisa ulichoandika....ukitaka kuendelea ku-survive kwenye soko lazima uweke bidhaa feki za kichina, na sababu ni:
  1. Watanzania walio wengi ni wako sensitive kwenye price....ukiweka kifaa genuine automatically bei yake lazima iwe juu ...sasa basi waliowengi wana opt kununua za bei ya chini...ambazo ni brand za kichina ( Nimejifunza haya kutokana na biashara ninayoifanya ya vifaa vya ujenzi)
  2. Pikipiki zilizo nyingi nchini ni za kichina ( affordable kwa kila mtu) - hivo tumia simple formula Pikipiki za kichina= spea za kichina......hapa unakuwa uwewapa wateja kitu wanachokipata
  3. Suppliers wa spea za Pikipiki hasa za kichina ni wengi........ila kaka inatakiwa uwe makini sana kwenye manunuzi ......hiki ndo kitu nilichojifunza. Unaweza ukakwea pipa mwenyewe ukaingia China au Ukanunua kwa whole salers walioko kariakooo. Si kila muuza spea kariakoo anasafiri...wengine ni misheni town tu af maduka yao wame-display kama wholesalers

Wakuu heshima kwenu,

Baada ya kupita pilikapilika za uchaguzi, sasa tuachane nazo, maana watanzania hawataki mabadiliko, kila mmoja atakura kwa ulefu wa akiri zake.

Wakuu naomba mwenyeuzoefu wa hii biashara ya kuuza vifaa vya pikipiki, naomba anisaidie.

Je, mtaji wa milioni moja utafaa?

Vifaa gani muhimu kwenye duka?

Je, faida yake inakuaje, na hasara zake inakuaje na changamoto zake pia?

Mimi naishi Kimanzichana mkoa wa Pwani.

Asante

=====
Sidhani kama Mtaji wa milioni moja utatosha,labda nikuulize hapo ume include kodi ya pango,kumlipa muuzaji etc.Nikupe mfano tairi ya pikipiki size ya san lg kubwa moja ni 50000 jiulize na spea zingine itakua bei gani?

Kaa chini survey uone vifaa gani vinahitajika sana kwa watumiaji ambapo unaenda kufungua duka,andika list yake na bei za manunuzi.

tazama faida ya kila kifaa angalia makadirio ya mauzo ghafi na baadae faida halisi utakayopata ukikamilisha hayo angalia kamtaji kako kama kanatosha.Ili uweze kufanikiwa ni lazima ujenge network na bodaboda owners ili waje kwako na ikiwezekana walete wenzao..

Unaweza kuwa unawapa motisha wakileta wateja hata kuwapunguzia kidogo bei ilimradi isiathiri profit margin yako!

Wengine ongezeeni.


Mkuu hongera sana kwa hili na mungu akusaidie. But huja sema uko wapi. Eneway ushauri wangu.

Kama utakuwa umepata eneo la kuuzia hizo spea fanya yafuatayo.

1. Nenda kule Kariakoo, pale utakutana na waagizaji nje wa spea za piki piki wale wamespecialize kama ni toyo utakuta waagizaji wa toyo, kama ni sunlg utakuta waagizaji wa vifaa vya sunlg na kazalika kila aina ya pikipiki ina waagizaji wake wakuu wa spea nje na hawa sanasana ni wahindi

2. Ongea nao na chukua bei za kila spea za pikipiki zinazo patikana mtaani kwenu

3. Waambie unataka kufungua duka la kuuza spea na kama hutaweza kuspecialize unaweza chukua spea za kila aina ya pikipiki

4. Patana nao, hawa jamaa wanaweza kuwa wanakuletea yaani unawatumia hela benk then unawatumia sumary ya spea unazo taka wao watazichua na watazifunga kwenye box then watakutumia either kwa njia ya basi mpaka mahali unafanyia biashara means mji, haina haja ya kufuata mwenyewe bongo.

Yangu ni hayo tu

Dimma,

Kwanza kabisa hongera kwa uthubutu, pili biashara ya spear usiifanye kama hujui hata kutofautisha bearings na matumizi yake wapi inafungwa na vifaa vingine kama hivyo.

Pia biashara hyo inahitaji uwepo wako ili kuweza kutambua mzunguko mzima wa biashara yako unaendaje, hiyo ikiwa ni pamoja na kujua vifaa gani vinakuwa rahisi kutoka ili visikosekane. Hapo ndio inaweza kuwa starting point yako. Spear sio kama ubwabwa kuwa umkabidhi jungu muuzaji huku ukiamini utamuhesabia plates.

Kingine ni location; hii Ina matter zaidi hasa mwanzoni unapo fikiria kufungua. MWISHO ni aina ya spear unayonunua ni kampuni gani,kuna spear ukinunua baada ya wiki ishasagika, kufanya return hutaruhusiwa Wala kuweza, hivyo umakini unahitajika.

Fuatilia hayo kwa muhtasari ukiwa tayari karibu kkoo tukuhudumie kwa Bei ya jumla nawe ukauze kwa rejareja.

Wasalaam
 
Muzee una mawazo mengi sana ya biashara! vp uko konfyuzd? nina wasiwasi hautafanikisha! (kidding!).

Kwani wewe una ujuzi gani, kama ni mstaafu, ulikkuwa unafanya kazi gani?

Jaribu kuangalia biashara ambayo unaaidia nayo kidogo (Kama haujui hata plagi itakuwa ngumu kufanya biashara ya spea za auto-japo inawezekana).

Kama ulikuwa mwalimu ni heri ufungue twisheni senta, au duka la vitabu!
Vinginevyo karibu shambani!
 
Hello amoeba,,hilo ndio tatizo tulilo nalo sisi binadamu,,ni wepesi wa kuhukumu wengine,,na wenye macho yaliyopewa uwezo kuona ubaya wa wengine na si uzuri wao,,kuna shinda gani ikiwa mimi nitakuwa nina business ideas nyingi?

Je, mtu mtu anayetaka informations kuhusu biashara mbalimbali ambazo ni halali yuko confused?

Siku zote ni vyema kufikiri kabla ya kutenda,,lakini hii haimaanishi tuzungumze bila kufikiri,,kuzungumza pia ni mojawapo ya matendo kwa hiyo tufikirie pia kabla hatuja zungumza.

By the way nakushukuru kwa vipengele vichache vyenye tija katika meseji,but accept to change in the others.

Asante sana.
 
Mimi kwa upande wangu nafurahi kuona idea mbalimbali za biashara kwani hiyo inasaidia hata wengine na
kupata changamoto katika kuanzisha biashara.
 
hello amoeba,,hilo ndio tatizo tulilo nalo sisi binadamu,,ni wepesi wa kuhukumu wengine,,na wenye macho yaliyopewa uwezo kuona ubaya wa wengine na si uzuri wao,,kuna shinda gani ikiwa mimi nitakuwa nina business ideas nyingi??? je mtu mtu anayetaka informations kuhusu biashara mbalimbali ambazo ni halali yuko confused???? si kuzote ni vyema kufikiri kabla ya kutenda,,lakini hii haimaanishi tuzungumze bila kufikiri,,kuzungumza pia ni mojawapo ya matendo kwa hiyo tufikirie pia kabla hatuja zungumza..

by the way nakushukuru kwa vingele vichache vyenye tija katika meseji,,but accept to change in the others..asante sana.

Dont quote me wrong mkuu!,
soma tena msj yangu, kwenye mabano nimeweka "natania", hata hivyo nisamehe if you cant take a joke!
1Love!
 
Tunahitaji mawazo mbalimbali kuhusu biashara najua humu kuna wataalamu wa kila aina na wenye uzoefu
wa muda mrefu kwenye biashara
 
Ni kweli hii biashara itazidi kukua everyday, naamini pikipiki bongo zitakuwa kama India au china maana watu wengi ndo wataweza kuafford.
 
Tunahitaji mawazo mbalimbali kuhusu biashara najua humu kuna wataalamu wa kila aina na wenye uzoefu
wa muda mrefu kwenye biashara
Exactly,,unajua nilikuwa nafikiri akili hiyo ninayo mimi tu,,kumbe hata mwenzangu unaliona hilo,asante sana tuendelea kuweka wazi mambo watu tufanye biashara vizuri zaidi,,nadhani hilo ndio lengo la kuwa hapa katika forum hii ya biashara,itusaidie kimawazo wote kwa pamoja..

asante sana mkuu enny.
 
Ni kweli hii biashara itazidi kukua everyday, naamini pikipiki bongo zitakuwa kama India au china maana watu wengi ndo wataweza kuafford.
Asante sana kang kwa kuweka wazi hili,,tuko pamoja mkuu.
 
Pikipiki,na spea zake zina soko,ila lazima ununue spea feki za china,siyo feki ila ni spea zisizo madhubuti,inalipa sana kwa mtazamo wangu,hasa ktk miji midogo ,siyo dar,in dar itakulzzimu uuze bei ya jumla.
 
piki piki,na spea zake zina soko,ila lazima ununue spea feki za china,siyo feki ila ni spea zisizo madhubuti,inalipa sana kwa mtazamo wangu,hasa ktk miji midogo ,siyo dar,in dar itakulzzimu uuze bei ya jumla
Asante sana mzalendo
 
piki piki,na spea zake zina soko,ila lazima ununue spea feki za china,siyo feki ila ni spea zisizo madhubuti,inalipa sana kwa mtazamo wangu,hasa ktk miji midogo ,siyo dar,in dar itakulzzimu uuze bei ya jumla

100% nakuunga mkono kabisa ulichoandika....ukitaka kuendelea ku-survive kwenye soko lazima uweke bidhaa feki za kichina, na sababu ni:
  1. Watanzania walio wengi ni wako sensitive kwenye price....ukiweka kifaa genuine automatically bei yake lazima iwe juu ...sasa basi waliowengi wana opt kununua za bei ya chini...ambazo ni brand za kichina ( Nimejifunza haya kutokana na biashara ninayoifanya ya vifaa vya ujenzi)
  2. Pikipiki zilizo nyingi nchini ni za kichina ( affordable kwa kila mtu) - hivo tumia simple formula Pikipiki za kichina= spea za kichina......hapa unakuwa uwewapa wateja kitu wanachokipata
  3. Suppliers wa spea za Pikipiki hasa za kichina ni wengi........ila kaka inatakiwa uwe makini sana kwenye manunuzi ......hiki ndo kitu nilichojifunza. Unaweza ukakwea pipa mwenyewe ukaingia China au Ukanunua kwa whole salers walioko kariakooo. Si kila muuza spea kariakoo anasafiri...wengine ni misheni town tu af maduka yao wame-display kama wholesalers
 
Payuka ,umeshafanikiwa kufika china kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa za biashara yako,if yes,labda utupe dira jinsi ya kwnenda na kupata suppliers wa ukweli ili marandu2010 afungue duka lake la spea za pikipiki,
marandu mimi ntakufungulia e-shop ya spea za pikipiki ili wenye viduka mikoani waweze kuorder online.
it will be a win-win situation,unanunua bidhaa ,mimi nakupa infrastrakcha ya kuweza kuuza online
100% nakuunga mkono kabisa ulichoandika....ukitaka kuendelea ku-survive kwenye soko lazima uweke bidhaa feki za kichina, na sababu ni:
  1. Watanzania walio wengi ni wako sensitive kwenye price....ukiweka kifaa genuine automatically bei yake lazima iwe juu ...sasa basi waliowengi wana opt kununua za bei ya chini...ambazo ni brand za kichina ( Nimejifunza haya kutokana na biashara ninayoifanya ya vifaa vya ujenzi)
  2. Pikipiki zilizo nyingi nchini ni za kichina ( affordable kwa kila mtu) - hivo tumia simple formula Pikipiki za kichina= spea za kichina......hapa unakuwa uwewapa wateja kitu wanachokipata
  3. Suppliers wa spea za Pikipiki hasa za kichina ni wengi........ila kaka inatakiwa uwe makini sana kwenye manunuzi ......hiki ndo kitu nilichojifunza. Unaweza ukakwea pipa mwenyewe ukaingia China au Ukanunua kwa whole salers walioko kariakooo. Si kila muuza spea kariakoo anasafiri...wengine ni misheni town tu af maduka yao wame-display kama wholesalers
 
Natumaini hamjambo wanajamii wa JF especially jukwaa hili,

Mimi ni kijana niliyeajiriwa sekta ya umma..nimeamu nijitose kwenye ujasiriamali...hasakwenye sekta ya usafirishaji hususani spea za pikipiki kama nilivyoainisha.

Kwa kuanzia nimefanya uchunguzi wa kutosha sehemu ninyaoishi ina pikipiki nyingi ila spea ndio hamna...sehemuitapatikana ila nahitaji kama kuna yeyote anaefahamu zaidi jins ya kuplan business hii anaipe some inputs.

Kama starting capital,vifaa vizur vya kuanzia kununua,bei na mengineyo.

Ninachukua mkope hivi karibuni nimeonelea bora nitimize iyo ndoto ya ujasiriamali maana uthubutu tayari ninao.

Pia niatanunua pikipiki kama 2.

Nimetenga nusu ya mkopo wangu wa 8mil ndio nianzie busness is it enough?

Asanteni.
 
natumaini hamjambo wanajamii wa jf especially jukwaa hili

mimi ni kijana niliyeajiriwa sekta ya umma..nimeamu nijitose kwenye ujasiriamali...hasakwenye sekta ya usafirishaji hususani spea za pikipiki kama nilivyoainisha.......kwa kuanzia nimefanya uchunguzi wa kutosha sehemu ninyaoishi ina pikipiki nyingi ila spea ndio hamna...sehemuitapatikana ila nahitaji kama kuna yeyote anaefahamu zaidi jins ya kuplan business hii anaipe some inputs....kama starting capital,vifaa vizur vya kuanzia kununua,bei na mengineyo...........ninachukua mkope hivi karibuni nimeonelea bora nitimize iyo ndoto ya ujasiriamali maana uthubutu tayari ninao...

Pia niatanunua pikipiki kama 2....

Nimetenga nusu ya mkopo wangu wa 8mil ndio nianzie busness is it enough?

Asanteni

mkuu hongera sana kwa hili na mungu akusaidie. But huja sema uko wapi. Eneway ushauri wangu.

Kama utakuwa umepata eneo la kuuzia hizo spea fanya yafuatayo.

1. Nenda kule kariakoo, pale utakutana na waagizaji nje wa spea za piki piki wale wamespecialize kama ni toyo utakuta waagizaji wa toyo, kama ni sunlg utakuta waagizaji wa vifaa vya sunlg na kazalika kila aina ya pikipiki ina waagizaji wake wakuu wa spea nje na hawa sanasana ni wahindi

2. Ongea nao na chukua bei za kila spea za pikipiki zinazo patikana mtaani kwenu

3. Waambie unataka kufungua duka la kuuza spea na kama hutaweza kuspecialize unaweza chukua spea za kila aina ya pikipiki

4. Patana nao, hawa jamaa wanaweza kuwa wanakuletea yaani unawatumia hela benk then unawatumia sumary ya spea unazo taka wao watazichua na watazifunga kwenye box then watakutumia either kwa njia ya basi mpaka mahali unafanyia biashara means mji, haina haja ya kufuata mwenyewe bongo.

Yangu ni hayo tu
 
KomandoO,

Asante sana ndugu yangu mi nipo dsm il anataka nifungue biashara hiyo maeneo ya ubungo...i hope ulishawahi kuifanya nawe pia..nitajitahidi mkuu unajua ten amaisha nayo yamebana inabidi kujipanga kweli kweli
 
Last edited by a moderator:
KomandoO,

Mkonowapaka, watamkwamisha au kumgonga bei. Kwa achunguze ni pikipiki za aina gani ndiyo nyingi kwenye soko. Angie kwenye website ya hawa wazalishaji na awombe uwakala wa kuuza spea watampa!

Pia awe anatengeza pia vijana wapo amuajiri moja au wawili. Asimamie mwenyewe! Akimwachia mtu amekwisha!

Nawasilisha.
 
Last edited by a moderator:
ImageUploadedByJamiiForums1387767815.738142.jpg ImageUploadedByJamiiForums1387767840.424193.jpg ImageUploadedByJamiiForums1387767873.808937.jpg
Wadau hongereni kwa kazi.
napenda kutambulisha duka langu la spare parts za pikpiki lililoko kariakoo mtaa wa Sikukuu/Amani. tuna vifaa vingi vizuri sana kwa bei nzuri.
tafaadhali wasiliana nami kwa no. 0658131333, email ni gkileo@gmail.com. pia no. yangu imesajiliwa kwa whatsapp ,we chat nk.
ndugu mdau utakaesoma hapa yawezekana ukawa huna duka wala pikipiki ,lakini mtaani kwako lipo. tafadhali mfahamishe kuhusu duka letu na mpe namba yangu pia waweza kunitumia namba ya simu ya mmiliki wa duka
 
Back
Top Bottom