Biashara ya Madini ya Dhahabu: Fahamu Uwekezaji Wake, Changamoto na Faida

mcrounmj

JF-Expert Member
Feb 26, 2016
380
885

Wadau poleni na swaumu mulio katika mfungo wa mwezi wa Ramadhani.

Napenda kujulishwa kwa mwenye uzoefu biashara ya dhahabu inalipa vipi kwa mtaji wa million 5, tahadhali za kuchukua dhidi ya utapeli, vibali vya biashara na maeneo ambayo yako suitable kwa hiyo biashara.

Natanguliza shukrani.

WADAU WENGINE WANAOHITAJI KUFAHAMU BIASHARA HII

MICHANGO YA WADAU MBALIMBALI


Jinsi ya Kuanzisha na Kuendesha Biashara ya Madini​

1.0 Utangulizi

Uchimbaji wa madini ni kuyatoa madini kutoka ndani ya ardhi kuja nje na kuyapa dhamani kwa kukata (vito vya dhamani) au kusafisha (metali) kwa ajili ya matumizi ya binadamu. Uchimbaji wa madini inahusisha pia uchimbuaji wa mawe ya kujengea na dhamani zingine zilizoko ndani ya ardhi. Utaratibu au ustaharabu wa kuchimbua mawe kwa matumizi ya binadamu ulianza pale mwanadamu alipobuni na kuanza kutumia mawe (enzi za ujima) na baadaye metali ya chuma na metali zingine ili kurahisisha kazi . Pia uchimbaji wa madini unajumuisha uchimbuaji wa rasilimali zingine za ardhi kama maji, gesi na mafuta kwa matumizi ya binadamu.
Shughuli za uchimbaji wa madini ndio mojawapo ya shughuli inayoongoza katika kuharibu na kuchafua mazingira na kwa hiyo tathimini ya utunzaji wa mazingira ni muhimu kufanyika kabla ya kuanza kuchimba ili kuweka mpango, mkakati na mbinu za kuhifadhi na kutunza mazingira katika maeneo ya ndani na nje ya mgodi
Kwanza kuna mambo muhimu ni lazima uyafahamu kabla ya kuingia kwenye biashara hii

1.1 Ngazi za Uwekezaji Biashara ya Madini​

  1. Makampuni madogo ya uwekezaji, (Uwekezaji wa mtaji chini ya dola za kimarekani milioni 50)
  2. Makampuni ya kati ya uwekezaji (Uwekezaji wa mtaji kati ya dola milioni 50 na milioni 500)
  3. Makampuni makubwa (Uwekezaji wa mtaji wa zaidi ya dola za kimarekani milioni 500)

a) Makampuni madogo ya uwekezaji – chini ya dola za kimarekani milioni 50​

Makampuni madogo ni yale ambazo kwa kiwango kikubwa zinawategemea wenye hisa kununua hisa ndipo zijiendeshe. Nyingi ya makampuni hizi ni za utafutaji wa madini na zinaweza kuwekeza mitaji midogo kwenye uchimbaji mdogo na hivyo kupata mapato yasiyozidi dola milioni 50 kwa mwaka

b) Makampuni ya kati ya uwekezaji dola milioni 50 hadi milioni 500​

Makampuni ya kati ni yale yenye mapato kwa mwaka kati ya dola za kimarekani milioni 50 mpaka milioni 500 na hazina uwezo wa kujenga miundo mbinu ya machimbo kama open pit au underground mining sites

c) Makampuni makubwa ya uwekezaji – zaidi ya dola milioni 500​

Makampuni yenye mapato ya mwaka ya dola Milioni 500 kwenda juu ndizo zinazohesabiwa kuwa ni makampuni makubwa. Pia ni lazima ziwe na uwezo wa kujenga miundo mbinu ya machimbo kama open pit au underground mining sites bila pesa za nje.
Tuchukulie wewe ni mchimbaji mdogo wa mtaji ulio chini ya milioni 50, sasa unatakiwa pia kujua aina za biashara za madini

1.2 Aina za Biashara za Madini​

  1. Utafutaji wa Madini (Mineral Exploration)
  2. Uchimbaji wa Madini (Mining)
  3. Kuchuuza (Brokering or Trading)
  4. Kutoa Huduma na Ushauri (Service and Consultancy)

a) Utafutaji wa madini au Mineral Exploration​

Utafutaji wa madini ni biashara nzuri kidogo kwa wale wanaoogopa vihatarishi na pia wanaridhika na faida za wastani. Uwekezaji wake ni mdogo na wa hatua mpaka upate prospect halafu unauza. Hatari yake kubwa iko kwenye kupata mkopo na prospect. Mpaka benki wakupe ni lazima uwe na track record nzuri sio tu ya kuchukua mikopo bali pia ya kuifanya hiyo biashara ya utafutaji kwa asilimia kubwa ya mafanikio.

b) Uchimbaji wa Madini au Mining​

Uchimbaji wa madini au mining ni kazi ngumu katika madini kwani kwanza uwekezaji wake ni mkubwa na pia unaweza ukakuta sivyo ndivyo au ndivyo sivyo kule ndani ya ardhi. Vifaa vyako vinaweza kukuonyesha kuna ngema ya kutosha lakini ukizama chini unakuta tofauti. Aidha unakuta ngema kubwa zaidi au unakuta kangema ambacho hata ngarama haiwezikurudisha. Na ndio maana utafiti wa hali ya juu na usio na haraka ni muhimu kabla hujafikia uamuzi wa kuchimba

c) Kuchuuza au trading

Hii ni hatua rahisi kuliko zote kwani hapa unahitaji vitu viwili tu
  1. Utaalamu wa madini unayotaka kuchuuza
  2. Mtaji wa kuanzia

d) Kutoa Huduma na Ushauri (Service and Consultancy)

Hii ni pale unapoamua kutumia ujuzi, uzoefu na vipawa vyako kwa kuwasaidia waliopo au wale wanaotaka kuingia kwenye biashara hiyo.
Huduma zinaweza kuwa ni
  1. Kufanya sorting
  2. Huduma za Umeme na maji
  3. Huduma za usafiri ndani na nje ya mgodi
  4. Huduma za chakula na
  5. Huduma za usafi
  6. Huduma za maduka
  7. Masoko na Kuuza
  8. Kuhudumia vifaa vya uchimbaji
  9. Kuwafundisha wataalamu /wafanyakazi wa migodi nk

2.0 Hatua 9 za Kufuata Ili Kuanzisha Biashara ya Madini​

  1. Kusajili Kampuni BRELA
  2. Kijiandikisha Mlipa Kodi
  3. Kuchukua Leseni
  4. Kuchukua Hati ya Usalama wa Mazingira
  5. Kuajiri wafanyakazi na wataalamu wengine
  6. Kununua na kuandaa vifaa mbalimbali
  7. Kutafuta masoko
  8. Kuanza uchimbaji wa majaribio
  9. Kuanza Uchimbaji Wenyewe
1. Kusajili Kampuni
Shirkisha mshauri wa biashara na mwanasheria wa upande wa makampuni ili wakusaidie kwa ushauri na utengenezajiwa MEMART ambayo ni muhimu katika kusajili kampuni

Unaweza kwenda mwenyewe BRELA kusajili au ukamtumia mhsauri mtaalamu wa mambo hayo. Nashauri umtumie mshauri mataalam ili kuokoa gharama za pesa na muda

2. Kijiandikisha Mlipa Kodi kwa kuchukua TIN TRA
Kujiandikisha TIN ni bure na inapatikana kwenye matawi yote ya TRA Tanzania

3. Kuchukua Leseni Wizara ya Nishati na Madini
Baada ya kukamilisha vigezo vya wizara unayo haki sasa ya kuomba leseni ya utafutaji au uchimbaji wa madini ambayo inatolewa na wizara ya Nishati na Madini

4. Kuchukua Hati ya Usalama wa Mazingira
Biashara ya madini ni mojawapo ya biashara inayoharibu mazingira kwa hali ya juu. Ni utaratinu wa mataifa yote duniani kutaka kuwa na uhakika wa utunzaji wa mazingira na hivyo bodi au mamlaka husika watahitaji kuingia mkataba na wewe ili wawe na uhakika kuwa mazingira yatakuwa salama wakati na baada ya uchimbaji.

5. Kuajiri wafanyakazi na wataalamu wengine
Biashara ya madini itahitaji wafanyakazi wa takriban nyanja zote kuanzia wahudumu, maofisa wataalamu na washauri. Hawa wote ni lazima uwaajiri au uwe na uhakika utawapata wapi kwa gharama muafaka

6. Kununua na kuandaa vifaa mbalimbali
Uchimbaji wa madini unatumia technolojia ambazo ndizo zitakazoamua kama wewe ufanikishe mradi au la. Teknolojia ya zamani ianweza kukupa hasara japo rahisi, teknolojia za kienyeji nazo zinaweza kukupa hasara. Teknolojia za kisasa zina faida japo ni ghali kununua. Unashauriwa kuwa na wataalamu washauri wa kukushauri tangu mwanzo namna ya kuamua juu ya teknolojia utakayotumia.
Kwa nini teknolojia za kienyeji au za zamani zina hasara?
  1. Nyingi ya hizo zinatumia muda mrefu kuleta matokeo
  2. Zina gharama kubwa za uendeshaji
  3. Zinaharibu mazingira
  4. Zinahitaji wafanyakazi wengi
  5. Nk
7. Kutafuta masoko
Kulingana na ukubwa wa uchimbaji au utafutaji, ni vyema kutafuta masoko ambayo utauza madini. Ikiwezekana uingie na mikataba ili uwe na uhakika wa kuuza punde utakapovuna.
8. Kuanza uchimbaji wa majaribio
Fanya uchimbaji wa majaribio angalau kwa miezi mitatu hadi sita kwa uchimbaji mkubwa kidogo unaweza kwenda hadi mwaka mmoja. Uchimbaji wa majaribio itakupa fursa ya kujua yafuatayo:
  1. Je, vifaa vitafaa kwa malengo yako
  2. Je, wafanyakazi uliowaajiri wanaweza kufanya uzalishaji wenye tija
  3. Je, biashara nzima italeta tija iliyokusudiwa
9. Kuanza uchimbaji Halisi
Baada ya uchimbaji wa majaribio, sasa unaweza kwa ujasiri kabisa kuanza kuchima madini. Muhimu tu ni kwamba yafanyie kazi changamoto zote zilziojitokeza kwenye uchimbaji wa majaribio
 
Kununua dhahabu

Sent using Jamii Forums mobile app
MAMBO YA KUFAHAMU NA KUZINGATIA KATIKA BIASHARA YA MADINI

Hii biashara inakubidi uwe

1. Mwizi wa macho kbs (kuchezea mzani)
2. Roho mbaya (utapeli kwa wateja wako) esp kwenue calculations.

I have been there, niliamua kuiacha!
Na serikali ya Magu mnagawana faida mnoo!
Shida kuu iko kwenye soko hawa wenye majiko wanachzea sana bei, yaan matajiri wanaambizana leo tutanunua kwa bei hii. Wanaweza panga kununia kwa 85000/ lakini soko la dunia linasoma figure nyingine!

Ukitaka kumake labda uwe na jiko...ila kununua dhahabu na kwenda kuuza faida ni ndogo (kule jikoni kama huna uzoefu watakuibia had utabasamu hata kama umepewa habari mbovu)

Unaweza nunua kwa 80000 jikoni ukakuta 77000 na pia ubora wa dhahabu (purity). Unauziwa mzigo kwa 80000@gramu lakini jikoni purity ikisoma 78%, 77% jua imekula kwako. So unajikuta mtaji unakatika polepole!

Kifupi toka serikali hii iingie imeharibu. Kodi zimekua juu mnooo labda ukutane na jiko wasilojua kucalculate unaweza ondoka na super profit!

Ushauri: Nenda kwanza migodini kasome kwamza mchezo kwa hao wanunuaji dhahabu( kota), then utaamua mwenyewe!na usiwe mbahili kuwezesha watu. Usipompa hela mteja wako jioni anaenda uza kwingine unakosa mzigo ukipata ufate faida atleast kwa siku ukusanye gramu kuanzia 25 hivi bila kodi kodi zao za wizi unaondoka hata na 100k & 120k! daily.

Kodi hapo unaweza acha zaidi ya 40!ila kama wenye majiko waelewa mnapoozeana! (Sasa hapa na wenyewe wanaogopa wanajua wewe mpelelezi, mie had leo wanajua ni mpelelezi -- very dangerous), tena kama ndo una sura sio ya kimgodi utakwepwa had ujute, watajua ww mpelelezi, watakukata kodi kama ilivyo ada.

Kuna makota wanapeleka kwa wahindi ananunua kwa shiling 80000 anaenda uza 87 (mfano)lakini hawakupi deal hata siku moja. Kifupi uwe mwizi mwizi (Kuonea wateja kuwaibia hela kbs) mjanja mjanja utatoka!ukiwa humble hiyo 5m itaisha august tu.

HELA YA DHAHABU TAMU SANA!
 
Mkuu umeelezea vyema. Hayo majiko kuanzisha ni gharama shillings ngapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umeelezea vyema.. hayo majiko kuanzisha n gharama shillings ngap

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna mchizi wangu analo aliniambia nitafute 30m! Bt cost kubwa ni mzani. Nadhan sasa utakuwa unaenda 8m-10m! Km sikosei. Huyu kaka akikuhadithia alivyoanza unasismka, kule sasa kuna hela!

Kuke ndo unaweza kucheza na hizi kodi mradi usishtukiwe! Ukishtukiwa wanabeba mzigo wooote😄😄! Na lesen wanapokonya
 
Mkuu hebu nipe mchanganuo hilo jiko unaliweka wap na linakupa VP faida? Nime kuchek PM naona msg haziendi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
M
Mkuu hebu nipe mchanganuo hilo jiko unaliweka wap na linakupa VP faida? Nime kuchek PM naona msg haziend

Sent using Jamii Forums mobile app
Mie ni mnunua dhahabu machimboni, nikinunua 20gms nakuja uzia kwako wewe mwenye jiko! Ww una mzani wa kusoma purity ya dhahabu. Kwahyo ww ukiniambia mie kuwa leo nanunulia shilingia kadhaa sina ujanja!

Nadhan ni km beaure de change, mgodini kuna headache sn kununua dhahabu(ulizwaji) huku jikoni ngumu kulizwa maana had ichomwe! Na dhahabu haiongopi ikipita kwa moto.

Naomba nikupm asbh sina chaj kwasasa!

Huku jikoni unaweza kula zaidi ya 200000/=kwa kila manunuzi ukiamua kuwa SMART i know you know😊😊!
 
Kwa kiasi Fulani nimeanza kupata idea kuhusu hizi dhahabu, je huko migodini ulizwaji upo kwenye nini na namna ya kukwepa ni vipi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kiasi Fulani nimeanza kupata idea kuhusu hizi dhahabu, je huko migodini ulizwaji upo kwenye nini na namna ya kukwepa ni vipi

Sent using Jamii Forums mobile app

KAMA HUIJUI DHAHABU, UNAUZIWA FEKI

Kama huzijui unauziwa kitu fake. Kuna dhahbu hichafuka tu..kwasababi ya mwamba kule chini au mercury kuwa chafu. Sasa ukinunua kwa bei elekezo utazika hela yako. Dhahabu chafu ina bei yake, maana had ioshwe na acid. Mambo mengi tu unapigwa huku jua linawaka!

Na upigaji mwingine uko jikonwakt wanachoma, so ni bora kucjomea jiko moja kuliko kuhama hama..kuna majiko kila unapopeleka mzigl wanawez kukuibia had point 8!..na huki ikichoma inabid ipungue kias kidg mayb .3(approx point 3)! Sasa hizl point 5 walizoiba ni approx 50000! Imagine uibiwe j3 had j3!

Hapo ndo mtaji unapokata!.kuchoma dhahabu lazima point fulani zipungue. Sababu ni nyinge esp kama haikuchomwa vizuri bado ina mercury...na jinsi ya kupma purity pale unaweza lia...unahakakika hii dhahabu safi na unajua hia zinasoma range hii had hii(mf, 80-87!) Majibu yanakuletea inasoma 78! Ikisoma hivuo unauza kwa hyo hyo bei78!labda wakuonee huruma wakununulie kwa 80!

Mambo ni mengi..ila ukipata chocho la kununua kwa bei elekez ukaenda uza kwa bei ya dunia uhakika wa kumake zaido ya lak 3 @ upo mkubwa! Tatizo connection, lakin ukisema ufate process ukate kodi hizi mpya mpya hapana...utaishia faida za 40000/-90000/= daily! Kama niko wrong wengine mtarekebisha!
 
Msiende PM mkuu, mwaga madini hapa hapa, tupo wengi tunaojifunza hayo Mambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Musiende pm mkuu, mwaga madini hapa hapa, tupo wengi tunaojifunza hayo Mambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kila biz ina changamoto zake. We kwa kuwa ni mzoefu, ni machimbo yapi yanafaa kwa mtu anayeanza ununuzi wa dhahabu!? Yaani maeneo ambayo ushindani wa kununua siyo mkubwa sana, kiasi kwamba unapata mzigo mkubwa kwa siku!
 
Kila biz ina changamoto zake. We kwa kuwa ni mzoefu, ni machimbo yapi yanafaa kwa mtu anayeanza ununuzi wa dhahabu!? Yaani maeneo ambayo ushindani wa kununua siyo mkubwa sana, kiasi kwamba unapata mzigo mkubwa kwa siku!
WEKEZA KWENYE HAYA KAMA UNATAKA KUFANIKIWA KATIKA BIASHARA YA MADINI

Kuna vimigodi vidogo vidogo lakini changamoto yake unapata mzigo mchache. Kwa mfano, kwa siku ukikusanya 4gm-10! Ni hasara.
Huko Geita mie machocho niliyopita atleast Kanegele hakukua na msongamano sana na purity kule iko juu, plus ntambalale.

Ukweli kama unataka kutoka wekeza kwenye
1. Plant (hapa kama unaaminiana na mtu ingia naye share) weka mkemia mzuri na mzoefu..hapa utapata kipato cha maana..hakikisha na wewe unakuwepo, sio unakaa Dar plant iko Mwambomba utapigwa had ushangae!
2. Nunua Crusher fukuzia kifusi kuza kifusi uza au peleka plant
3. Kuwa na sonara yako .means uwe na jiko lako la kuchomea dhahabu
4. Nunua vifusi (sasa hapa itakubid kuwa na urafiki na mwenye plant naye unamgea %..ukinunua vifusi vizuri una hakika wakuwa na faida ya 5-7m every month ukikatika sana ni 3-5m (sasa ukiwa na plant yako next year tutakuita don bila wewe kupenda)

All in all itakupasa kukaa migodini kusoma Michezo kwanza! Kujua magumashi yanatokeaje!

La mwisho haya mamigodi yana uccm sana walotoka sana kifedha lazima CCM iwahusu ia sivyo utasumbuliwa sana na TRA, polisi Weka urafiki na polisi wa migodini, usijioneshe mpinzani in any means!

Kifupi sina hakika kama kuna hela tamu kama ya dhahabu😄😄! Ukiingia ukapata hutoki! So ni kuwa smart uje utafute mtaji!
 
Asante mkuu. Ila ukipata chimbo ambalo kwa siku unaweza kukusanya kuanzia gram 20 inakuwa poa sana!

Hekaheka za U CCM na polisi hazina shida kwani wote lengo leo ni pesa. Na wengi wao wanaojificha kwenye ukada wanamaghumashi kibao. Kikubwa labda ni kupata leseni ya broker!

Ununuzi wa vifusi nasikia wanapata hasara kubwa sana. Nasikia kwenye final processes wengine huzimia kwa sababu ya kupata hasara kubwa! So changamoto kwenye uchenjuaji wa vifusi si haba pia!

Vipi machimbo ya Mbeya na Mpanda una uzoefu nayo?
 

Mpanda na Mbeya hapana sina uzoefu nako, kiukwel Geita nadhani ndo mambo yote!

Hapo mafinga kuna kamgodi wanasema kamechangamka yuko bro huko sema bado haujasettle. Lakini umelipuka!

Ndo hayo hayo nimesema inabid ujue michezo ya plant. Ukae kwa muda usome Michezo zao. Wengi ndio wanalizwa lakini ukipata connection utafurahi! Tena siku hi wamepungza sana kuliza coz ya utawala huu!

All the best
 
Mkuu vipi kwa mtu asiye na mtaji kabisa lakini anataka kuingia katika kazi za madini ili akiweza kukusanya mtaji na yeye aje afanye uwekezaji we tija Migodini kuna ajira gani kwenye migodi midogo vipato vya wanaochimba vikoje?

Na kama kijana nataka kujilipua kuanza kutafuta maisha ya madini ni maeneo gani ya migodi unayoona yana potential
 

SHUGHULI ZA MGODINI KWA WASIO NA MTAJI

Kiukweli kule ujitoe tu ufahamu kama huna mtaji! Kazi zipo ila za kutumia nguvu especially kuosha unga, kuchenjua dhahabu (hapa lazima ujifunze kwwli kweli) na ni ngumu mtu kukupa tope lake umchenjulie, wanaiba sana hapa kwa kuchenjua.

Kazi nazoona wanafanya zaidi kina kaka wasio na .mtaji ni kupiga moko(kuzamaa huko chini kupiga mwamba) ni kazk ngumu kiukweli, ila ukibahatika ukatoka na kajiwe uongo! Mistake za kule ni zile zile kwasababu kazi ni ngumu bas mtu akipata hela anatumia hovyo sana!

Kuosha unga ni 2000@ mzunguko mmoja. Mzunguko mmoja unaweza chukua ndoo zile ndogo 5-8!inategemeana na ukubwa wa ile machine(crusher )na inaweza zidi pia kidogo. So unga ni mwingi kiukwel. Sasa vibarua ni hela ya kula tu..mayb uombe uoperator na mkubaliane mlipane mkishauza kifusi. Hapo makubaliano ni yenu wewe na mwajiri wako! Bt haizid 500k had kaz kufunga!

Mie nachoamini pia ni bahati! Kuna dogo ndugu yangu alifika kule mwaka 2017! Akitokea chuo, alifika hana kitu akaomba kwa mzee 200k! Leo hii kila miezi miwili ana faida ya kuanzia 6-8m!so alianza na , 200k akinunua mawe ya bei ya chini(fello) akapanda had kumiliki crusher! Means akianza leo 14th kazi anafunga 14 July anauza kifusi yy hana mpango na plant kbs.faida ndo hizo 6-8m! Ikigoma sana 4m. Kule naona wasomi kama wanatoka mapema eti! Mradi uwe serious na usmart fulani!

Na ukitaka kufanikiwa mapema nenda kwenye mgodi ulolipuka. Sio mgodi uliodormant!
 
August mbona mbali mkuu. Ataanza may 16 halafu kufikia june 1 hana hata mia mbovu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fikra potovu mkuu
! Toa sababu boss
Kuna sehemu umeeleza kuuziwa madini feki. Kwetu wanapima kwa viroba (mifuko ya 25k) labda unauzwa kwa 200k@ halafu linakuja tajiri moja feki (wakikuona mgeni na una wenge wanakuchezea) huyu tajiri feki atajifanya anataka kununua mawe yote.

Tuseme kuna viroba 100x200000=20,000,000. Mara nyingi kama mawe yana sample sana wtu hugombania (kota wenye mitaji midogo). Hapo bei aidha itapanda au mtanunua kwa kukomoana. Unanunua viroba 10.

Kimbembe ni kwenye kuosha. Umetoa 2m halafu unapata 100000 (iliwahi kunitokea mara mbili sitakaa nisahau na ndio ilikuwa mwisho kununua mawe) Utabaki na 3m kuna siku utapata ila faida haiwi kubwa. Niambie itachukua muda gani kukuweka chini


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…