Hello friends ...
Naomba nijibu maswali yenu hapa. Kama nilivosema mwanzo kuna aina nyingi za icecream ila pendwa sana ni za maziwa. Mie hutengeneza za maziwa na za ubuyu, nianze na za maziwa.
MAHITAJI
1. Maziwa ya unga
2. Sukari
3. Maji
4. Ladha (vanila)
5. Rangi ya chakula ( mie hutumia yellow)
6. Kilainishi(optional)
7. Vifungashio
Sasa hapa unakua na vipimo vyako mwenyewe mfano kwa mahitaji ya icecream 70 za maziwa
1.Maji lita tano( yalochemshwa au weka water guard kurahisisha)
2. Maziwa ya unga robo kilo (tsh 3250)
3. Sukari robo kilo (tsh 650)
4. Ladha ya vanila (tsh1,000) hii utatumia vifuniko viwili tu au vitatu vya kichupa....
5. Kilainishi(tsh 500) kijiko kimoja cha chakula changanya material yako hayo namba moja hadi nne, kisha weka rangi yako (tsh 100 tu) kidogo tu. Baada ya hapo kilainishi unakiweka kwenye blenda unachanganya maji nusu kikombe ule uji wake weka kwenye mchanganyiko wako. Congratulations bidhaa yako ipo tayari funga ktk vifungashio (tsh 500) vyako kisha weka kwa fridge yako tayari kupokea pesa.
Mahitaji 3250+1000+650+500+500+100 =600
Mapato 70@200 =14,000
14,000-6,000= 8,000
net profit 6,000
Mahitaji kama ladha, rangi, vifungashio na kilainishi utatumia hadi mara 5 bila kununua tena imagn unaweza kuuza icecream 100 tu kwa siku.
100 x200=20,000 kwa siku mara siku 30 sawa na 600,000 kwa mwezi toa gharama za uendeshaji unacheza kwenye laki nne. Fikiria sasa kutanuà soko lako. Ni zaidi ya mshahara wa degree holder.
Ubuyu ndo cheaper zaidi. Oh I love this biz nakushawishi ufikirie. Mkihitaji ya ubuyu nitaelekeza pia.