Biashara ya kutengeneza na kuuza, ndio itakayo timiza ndoto zako

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,472
40,470
Biashara yoyote inahitaji uvumilivu; wengi wanaamua kufunga biashara zao na kulalamika kwa sababu wanakuwa wamekosa uvumilivu.

Na hasa ukiingia kwenye hii biashara ya kutengeneza na kuuza, muda mwingi wewe unakuwa unatoa pesa tu; mpaka uje uanze kuona faida inachukua muda mrefu.

Unapotaka kufanya biashara yenye mafanikio, ni lazima uwe na mtazamo wa mjasiriamali ''entrepreneur''; ambaye kwake kupata pesa, ni chaguo la pili na si la kwanza.

Biashara inaweza kuchukua miezi na miezi au miaka na miaka, mpaka kuja kukupa faida unayoitaka; muhimu uwe umeiwekea misingi mizuri ya kufika kule unakotaka kufika.

Mwanzoni ni lazima ukubali kupoteza pesa, ili baadaye ndio uje upate pesa.

Kwa mtu anayejiingiza kwenye biashara ya kutengeneza na kuuza; huyu anaingia gharama kubwa sana kuliko yule aliyeingia kwenye biashara ya kununua na kuuza (uchuuzi).

Ila huyu, anayetengeneza na kuuza (entrepreneur), huko mbeleni atakuwa na mafanikio makubwa sana, kwa sababu inampelekea kwenye kumiliki kiwanda kama sio viwanda.

Kama mjasiriamali, utajisikiaje pale unapotembelea duka la kwanza mpaka la 50 n.k, unakuta linauza bidhaa zako?

Kwa kifupi, hii biashara inalipa ingawa inachukua muda mrefu.

Karibu kwa maswali.​
 
Biashara yoyote inahitaji uvumilivu; wengi wanaamua kufunga biashara zao na kulalamika kwa sababu wanakuwa wamekosa uvumilivu.

Na hasa ukiingia kwenye hii biashara ya kutengeneza na kuuza, muda mwingi wewe unakuwa unatoa pesa tu; mpaka uje uanze kuona faida inachukua muda mrefu.

Unapotaka kufanya biashara yenye mafanikio, ni lazima uwe na mtazamo wa mjasiriamali ''entrepreneur''; ambaye kwake kupata pesa, ni chaguo la pili na si la kwanza.

Biashara inaweza kuchukua miezi na miezi au miaka na miaka, mpaka kuja kukupa faida unayoitaka; muhimu uwe umeiwekea misingi mizuri ya kufika kule unakotaka kufika.

Mwanzoni ni lazima ukubali kupoteza pesa, ili baadaye ndio uje upate pesa.

Kwa mtu anayejiingiza kwenye biashara ya kutengeneza na kuuza; huyu anaingia gharama kubwa sana kuliko yule aliyeingia kwenye biashara ya kununua na kuuza (uchuuzi).

Ila huyu, anayetengeneza na kuuza (entrepreneur), huko mbeleni atakuwa na mafanikio makubwa sana, kwa sababu inampelekea kwenye kumiliki kiwanda kama sio viwanda.

Kama mjasiriamali, utajisikiaje pale unapotembelea duka la kwanza mpaka la 50 n.k, unakuta linauza bidhaa zako?

Kwa kifupi, hii biashara inalipa ingawa inachukua muda mrefu.

Karibu kwa maswali.​
Mimi nitalima na kuongeza thamani ya mazao yangu na kuuza
 
Mimi naona biashara zote tu zinaushindani unaweza sema bidhaa za kula kama mkate,maji, nk au Viwanda vya tofali au mabati japo mtaji wake ni mzito kidogo hivyo kwa vijana wengi hatutaweza
Tengeneza bidhaa ambazo wasambazaji wako ni wenye maduka; wewe unawapelekea mzigo kwa bei elekezi, na kuweka utaratibu wa kuzungukia makusanyo ya mauzo.

Ukiwa na maduka yako 100 wewe tayari ni tajiri; na wenye maduka wanataka mzigo kwa mkopo, kama una uwezo wa kuzalisha mahitaji yao; huku ukisubiri malipo, itakuwa vizuri zaidi.​
 
Back
Top Bottom