Biashara ya kusafirisha matunda Ulaya

Mkuu tafuta uwezekano wa wewe kuanza kuuza bidhaa au hayo matunda toka TZ. Ukweli ni kwamba hata kahawa ya TZ watu wanai-pack vizuri na kuandika kuwa ni product za kwao. Vile vile machungwa. machungwa ya Muheza wale wa kutoka jirani wanakuja wanayachuma kwa umakini ili yasipate mikwaruzo wanaya-pack na kuandika ni produce za kwao na kuuza. Sisi wa TZ tumekalia kulalamika. Na malalamiko hayaleti tija bali uchungu na akili kutokufanya kazi vizuri na kutokuona fursa zilizopo. Watu wachangamke!

Mkuu machungwa ya Muheza hayauzwi Ulaya hata siku moja, yale machungwa huwa wakenya wanachukua wanaenda kukamua juice zao na mengine wanauza mazima lakini ni within kenya, tembelea TAHA wakupe ni aina gani ya matunda na mboga ambazo zinaweza meet viwango vya kuuzwa Ulaya,

Mkuu kuingiza matunda au mboga ulaya si swala la kitoto hata siku moja, na huwezi jidanganya kwamba utakuwa unanua kwa wakulima wewe unasafirisha tu hakuna kitu kama hichio

Tafuta procedure za kufuata ili kuingiza matunda Ulaya ndo utagundua kwamba unacho ongea hakipo
 
Kuna mswahili mmoja anaongoza board of external trade anafikiria kazi ya board yake ni kuandaa maonyesho ya sabasaba tu.

Mkuu usiwalaumu wale Board of External trade, nasema kusafirisha Bidhaa kwenda masoko ya ulaya haihitaji siasa wala haitaji kupigiwa pande mkuu, wale wanacheza na procedure pekee, ngoja kuna docoment moja ya procedure nilikuwa nayo nitaitafuta niwawekee humu muon kwamba hakuna short cut

 
Hay

Nimependa sana topic yako ni nzuri sana na inamvuto wa ajabu tatizo letu watanzania ni tunaogopa kuthubutu kufanya biashara au kitu cha kutupatia riziki tunabaki tukiilaaumu serikali mbona haijatupa ajira wakati ajira tunazo na tunazikalia tu bila hata kuthubutu kufanya kwani ukithubutu kuuza matunda nje ya nchi serikali haitakuangalia na kukupunguzia ushuru kwa vile imetambua jinsi ulivyo na unao uwezo wa kufanya biashara hivyo?
 
Wengi wetu wanaogopa ushuru unaotozwa na complexities za uzalishaji wa bidhaa zenye viwango vinavyohitajika huko.
Yaan hata baada ya ile mipango ya AGOA na ... inayoturuhusu kuuza bidhaa njebila vikwazo vyovyote (hasa Marekani na Ulaya) kuanzishwa bado mwitikio ni mdogo ukilinganisha na wenzetu wa Kenya na Uganda.

Nadhani Mamlaka zinazohusika kama BET, TIC, MITM, ..bado hazijatoa elimu ya kutosha kwa wajasiriamali wetu. Hata BDSP (kama AMKA) nao wanahusika kwan sector hii bado ipo nyuma sana ukilinganisha na wenzetu wa Kenya na Uganda.

Cha msingi kwa sasa ni kuanza personally pale unapoona fursa

ule mpango wetu unaendeleaje? Nashangaa stakeholder mimi sipati updates.
 
Cchallenge huwa ni ubora na kukidhi hizo taratibu kwenye uchumi Kama wetu ambapo umeme (refrigeration) na gas (transportation) is unreliable. Juu ya hapo miundombinu haikosupportive for a small farmer to produce at competitive volume, size, pesticides, mbolea etc all at levels that compete internationally.

A few years back nilinunua green beans Tesco (UK)... Nakumbuka kuwa very excited to see beans from Tanzania! Well, nilipofika home natoa kwa pack nakutana na udongo mwekundu kibao! Wakati quality control ya wengine isingepitisha pack ya namba hiyo... Hata kuosha tu alishindwa supplier Huyo wabTz?! Anyway, since then nikarudi kwenye kasumba yangu kuwa made in TZ is inferior quality... Najua huu ni upungufu kimtazamo hivyo ninalifanyia kazi. Naamini TZ tunaweza kuwa serious na kutengeneza vitu vyenye ubora wa kimataifa!
 
Personally nimeanza na shamba la miembe eka kumi lazima nije export
NI miembe ya kisasa toka SUA pale.
\Piga ua galagaza lazima einde pande za mbali

habari mkuu.

ni two years tangu uweke hiyo comment yako,vipi project yako ya maembe ina progress gani?natamani na mimi kufanya ya maembe na machungwa huko kisarawe...pia ukinipm ur mobile namba itakuwa poa zaidi tuangalie jinsi ya kushare bness info.

Thanx
 
mkuu umeongea point nzuri sana hata mm napenda kufanya biashara nje ya tnzania nichukue samaki hapa na kusafirisha ulaya au chochote hapa kinacholimwa na kuuza ulaya ila kinachotucost zaidi ni mtaji na vilevile kupata masoko huko au uwezekano wa kuweza kuingia katika soko huria ala nje kama kuna mtu anaweza kutuconnect huko itakuwa njema nasi tukaweza uza biadhaa zetu huko

Wakuu naomba ushauri wenu.
Nimekuwa nitembelea maduka mbali mbali katika nchi za Ulaya hasa UK na kukuta bidhaa kazaa za kutoka Uganda na Kenya lakini sijawahi kuona bidhaa zozote kutoka Tanzania katika maduka ya UK. Nikiwa Tanzania naona kuna matunda mengi kama Machungwa, Mahembe, Nanasi, Mapalachichi, nk zimerundikwa tu barabarani na vinauzwa kwa bei ya chini sana kulinganisha na bei ya Ulaya. Je kwa nini Watanzania hatuna akili ya kuweza kupeleka hivi vitu Ulaya na kupata soko zuri.
Mimi napenda sana ndizi Bukoba na huwa nazipata kwa urahisi sana katika Maduka ya UK zikiwa zina nembo ya (Product of Uganda). Hawa jamaa wananunua ndizi hata kutoka Bukoba na Karagwe. Sisi kwa nini tusifanye hivyo tena kutoka hata Mbeya? Waganda wanauza majimbi, viazi na hata nyanya chungu katika soko la Ulaya. Sisi tumelogwa?
Wakenya wametawala soko la maua, sisi kwa nini hatuwezi?
Naomba mawazo yenu
 
You r the typical Tanzanian only talk, you saw an opportunity n u have started complaining and looking for Mchawi. Anza kazi , umeliona soko lollipop na unajua bidha zinapopatikana kwa urahisi, sasa wangoja nini ???? Au unataka kuilaumu serekali ya ccm?????

Watanzani tuuwazembe mnoo tujualo no kashfa na lawama. Nyerere alisema uchumi tunao lakini tumeukalia, wajanja tulatafsiri vingine.

Mimi nimeona wakenya wakinunua pilipili na ndimu Tanga na zinapelekwa Kenya.

Mir hivi nasafirisha korosho na mbaazi kupeleka India na ninajua Kuwa tuna bidhaa bringing tuu zenye soko njee
 
mfano halisi ni bakheresa
Cchallenge huwa ni ubora na kukidhi hizo taratibu kwenye uchumi Kama wetu ambapo umeme (refrigeration) na gas (transportation) is unreliable. Juu ya hapo miundombinu haikosupportive for a small farmer to produce at competitive volume, size, pesticides, mbolea etc all at levels that compete internationally.

A few years back nilinunua green beans Tesco (UK)... Nakumbuka kuwa very excited to see beans from Tanzania! Well, nilipofika home natoa kwa pack nakutana na udongo mwekundu kibao! Wakati quality control ya wengine isingepitisha pack ya namba hiyo... Hata kuosha tu alishindwa supplier Huyo wabTz?! Anyway, since then nikarudi kwenye kasumba yangu kuwa made in TZ is inferior quality... Najua huu ni upungufu kimtazamo hivyo ninalifanyia kazi. Naamini TZ tunaweza kuwa serious na kutengeneza vitu vyenye ubora wa kimataifa!
 
mm naisubiria sana hiyo procedure yako kwani umesema utaitafuta na kutuletea hapa

Mkuu usiwalaumu wale Board of External trade, nasema kusafirisha Bidhaa kwenda masoko ya ulaya haihitaji siasa wala haitaji kupigiwa pande mkuu, wale wanacheza na procedure pekee, ngoja kuna docoment moja ya procedure nilikuwa nayo nitaitafuta niwawekee humu muon kwamba hakuna short cut

 
Wakuu,tujuzeni soko la nje ya Tanzania kwa mazao ya matunda kutoka kanda ya kati yenye matunda mengi ya ubuyu na zabibu
 
Mkuu machungwa ya Muheza hayauzwi Ulaya hata siku moja, yale machungwa huwa wakenya wanachukua wanaenda kukamua juice zao na mengine wanauza mazima lakini ni within kenya, tembelea TAHA wakupe ni aina gani ya matunda na mboga ambazo zinaweza meet viwango vya kuuzwa Ulaya,

Mkuu kuingiza matunda au mboga ulaya si swala la kitoto hata siku moja, na huwezi jidanganya kwamba utakuwa unanua kwa wakulima wewe unasafirisha tu hakuna kitu kama hichio

Tafuta procedure za kufuata ili kuingiza matunda Ulaya ndo utagundua kwamba unacho ongea hakipo
Mkuu kati ya watu wanafiki na Wewe utakuwamo! Eti machungwa ya Muheza hayauzwi nje? Hivi unakijua kile wa-Kenya hawa wanakifanya na matunda kutoka Tz? Kwa taarifa yako hayo machungwa yakishafikishwa Kenya huwa wanafanya packaging kwenye makasha safi kabisa yenye nembo za Kenya! Wenzetu wanachotuzidi ni kuzingatia ubora maana EU standards siyo mchezo. Wakenya wakichukua hayo machungwa ya Muheza wanachambua vizuri kabisa wanayaosha vizuri kabisa na ku-pack. Hata maua ya arusha wanayalangua wao na kufanya packaging upya kwenye makreti safi kabisa yakifika Amsterdam kwenye mnada Wa maua yanaonekana yote yametoka Kenya kumbe kuna mengine yametoka Tz.
 
Anzisha uonee kama hutowekewa vikwazo kama Arabic states juu ya marikaniii cyooo tz wewee, natoka Tanzania aka tz bongo aka nchii iliyojaa viongozii wenye cv za uongo aka aslimia sabini wananchi ni maskini aka kaa chini fanya tathmini aka nambie unachokionaa niini????
 
kwa kweli ni wakati wa sisi kubadilika , hizi regulations za EU nafikiri inatakiwa kuzijua , tusitegemee serikali , watu wenyewe wanaofanya serikalini ni kama mimi na wewe wamejichokea hawana motivation , wakenya wametushinda kwa hili aisee lakini sisi tuna nafasi kubwa ya kufanikiwa zaidi yao
 
Watanzani tunangoja kufanyiwa, akili zetu finu, kazi kulalamika kwenye mitandao tu. Ngoja aje Mhindi, Mwarabu, Msomali Mchina au Mzungu afanye halafu sisi tulalamike kuwa anatorosha matunda!

Kumbuka, hizo unazoziona zinatokea Kenya nyingi ni kutoaka Tanzania, wanakuja Wakenya kuzinunuwa Tanzania, wanapeleka kwao wan pack vizuri wanapeleka nje kama zao.

Wewe mleta mada, kama umeiona hiyo fursa kwanini usianze wewe kufanya hiyo biashara badala ya kulalamika kwenye mitandao?
 
habari mkuu.

ni two years tangu uweke hiyo comment yako,vipi project yako ya maembe ina progress gani?natamani na mimi kufanya ya maembe na machungwa huko kisarawe...pia ukinipm ur mobile namba itakuwa poa zaidi tuangalie jinsi ya kushare bness info.

Thanx
Mdau mgogoro wa fedha ulikwamisha project yangu maana kuna mkopo nilikuwa nafukuzia ukagonga mwamba ila bado nina moyo one day itatic
 
Kuna siku nimeona documentary katika television ya ujerumani inaelezea biashara ya maua. Documentaru hii ilikuwa inaonyesha jinsi wakulima wa maua wa ujerumani wana vyoathirika na maua yanayoingizwa kutoka kenya hadi wengine kufikia hatua ya kufunga mashamba yao kwa sababu hawezi ku compete.

Katika upande mwingine ilionyesha jinsi wananchi wa kenye wanavyoathirika kwa kilimo cha high scale cha mashamba ya maua, ikiwemo kulipwa ujira kidogo, uharibifu wa mazingira kutokana na kemikali za madawa na athari ambazo wafanyakazi wa mashamba haya wanakutana nazo kutokana na madawa hayo.

Kwa kifupi documentary ililenga kuharibu soko la maua ya kenya ujerumani.

Ninachotaka kusema hapa linapokuja swala la biashara za kimataifa ni lazima serikali iwe mstari wa mbele kuhakikisha na kudhibiti ubora. Ni lazima serikali iwahakikishie walaji hao wa nje kuwa bidhaa zinazalishwa katika hali salama na zina ubora unaotakiwa. Refer sakata la minofu yasamaki eu.

Kwa upande wa matunda na mboga mboga ni dhahiri kuwa serikali yetu haijafanya kazi ya kutosha kutafuta na kudhibiti soko.

Mara nyingi nikinunua matunda kama ndizi na machungwa kutoka supermarket za majuu ni dhaifu sana sana kulinganisha na yanayopatikana hapa TZ. Ndizi za tarime, bukobana mbea ni nzuri na tamu kuliko zinazotoka jamaica.

Nilijaribu kuuliza nikaambiwa eti tatizo letu ni kwamba hatuna uwezo wa kusupply kwa kiwango kinachotakiwa kwa mwaka mzima. Uaani production yetu iko chini kuliko demand nani ya msimu wakati watu wanataka mwaka mzima. Sina uhakika na hili, ila ninachohisi ni kwamba serikali na wafanyabiashara wa TZ hawajachangamkia fursa.

Kama minofu ya samaki inasafirishwa kutoka mwanza hadi ulaya, iweje ndizi zisitoke bukoba na tarime kwenda majuu.

Nakumbuka wakati sangara walikuwa hawana soko pale mwanza, na jinsi tulivyofanya kazi katika idara ya uvuvi kutengeneza soko la ulaya. Hadi leo sangara wamekuwa ni bidhaa adimu. Tuli organize wafanyabiasha na ku lobby kwa mabalozi wa EU. The same thing inatakiwa ifanywe na wizara ya kilimo.

Hakuna mtu mmoja mmoja anaweza kukidhi soko la ulaya la matunda. Ila wafanyabiashara wakiwa organized, kutoka sehemu mbalimbali wakasafirisha bidhaa zao kwa pamoja inawezekana.

Tunahitaji kufanyia kazi hii fursa. Huwezi kukwepa mkono wa serikali katika hili.
 
Back
Top Bottom