Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,302
- 12,851
Mambo mawili yanaua biashara mikoani na kukuz biashara Dar.
1. Mitandao ya kijamii.
2. Urahisishaji wa kusafirisha bidhaa.
1. Mitandao ya kijamii imerahisisha sana mawasiliano ya muuzaji na mteja Imerahisisha sana namna ya kutangaza biashara. Mteja anaweza kuona biashara maduka mbalimbali na akafananisha bei kwenye mtandao tu. Anafanya window shopping akiwa katulia hapohapo alipo.
Sasa mara nyingi mtu anapotaka bidhaa ya pesa nyingi kama TV, music system nk, anafanya sana utafiti. Hapo akiingia mitandaoni atakuta maduka ya Dar yamejaa tele. Maduka mengi yanauza hizo bidhaa wakati mkoani unakuta duka moja tu.
Tena unakuta watu wa Dar wanaelewa teknolojia mpya vizuri tofauti na mkoani. Na kwa sababu maduka haya ni makubwa, yanakuwa yanauza bei poa. Mitandao imerahisisha sana window shopping. Mtu hata akitaka suti, viatu na vitu vingine kama hivyo anaingia mtandaoni na kuagiza.
2. Usafirishaji
Bei za usafirishaji na uaminifu vimekua sana. Mtu akinunua kitu Dar na kusafirisha bado bei inakuwa chini kuliko kununua kitu hichohicho mkoani. Na kawaida kinachukua siku moja au mbili max kufika. Tulipofikia inawezekana kuna maduka yana wateja wengi wa rejareja kutoka mikoani kuliko wa Dar hapohapo.
Tunakoenda maduka ya mikoani yatabaki kuuza vitu vidogovidogo, nyanya, vitunguu, simu jinga na vile ambavyo ni ngumu kusafirisha.
Nini kifanyike kuokoa biashara za mikoani zinazodorora kila siku?
1. Mitandao ya kijamii.
2. Urahisishaji wa kusafirisha bidhaa.
1. Mitandao ya kijamii imerahisisha sana mawasiliano ya muuzaji na mteja Imerahisisha sana namna ya kutangaza biashara. Mteja anaweza kuona biashara maduka mbalimbali na akafananisha bei kwenye mtandao tu. Anafanya window shopping akiwa katulia hapohapo alipo.
Sasa mara nyingi mtu anapotaka bidhaa ya pesa nyingi kama TV, music system nk, anafanya sana utafiti. Hapo akiingia mitandaoni atakuta maduka ya Dar yamejaa tele. Maduka mengi yanauza hizo bidhaa wakati mkoani unakuta duka moja tu.
Tena unakuta watu wa Dar wanaelewa teknolojia mpya vizuri tofauti na mkoani. Na kwa sababu maduka haya ni makubwa, yanakuwa yanauza bei poa. Mitandao imerahisisha sana window shopping. Mtu hata akitaka suti, viatu na vitu vingine kama hivyo anaingia mtandaoni na kuagiza.
2. Usafirishaji
Bei za usafirishaji na uaminifu vimekua sana. Mtu akinunua kitu Dar na kusafirisha bado bei inakuwa chini kuliko kununua kitu hichohicho mkoani. Na kawaida kinachukua siku moja au mbili max kufika. Tulipofikia inawezekana kuna maduka yana wateja wengi wa rejareja kutoka mikoani kuliko wa Dar hapohapo.
Tunakoenda maduka ya mikoani yatabaki kuuza vitu vidogovidogo, nyanya, vitunguu, simu jinga na vile ambavyo ni ngumu kusafirisha.
Nini kifanyike kuokoa biashara za mikoani zinazodorora kila siku?