JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
Dalili ya kuongezeka kwa wafanyabiashara katika eneo hilo imekuwepo kabla hata ya ujenzi wa barabara ya mwendokasi, hakuna hatua zilizochukuliwa, sasa barabara imekamilika, hakuna hatua zinazochukuliwa.
Wafanyabiashara wamefurika kuanzia Kituo Kipya kwenye eneo la kugeuzia magari, kwenda mpaka barabara ya kuingia Kampala International University. Unaweza kuwahi huko ulikotoka, lakini ukifika Gongolamboto unaweza kutumia hata saa nzima kupita kama una gari.
Kinachosaidia kwa sasa ni kwa sababu mabasi ya mwendokasi hayajaja, lakini kama yatakuja, maana magari ya kawaida hayataruhusiwa kupita kwenye njia zake.
Tunajua Gombolamboto hakuna soko kubwa la kuwachukua hao Wamachinga, lakini TANROADS wanapaswa kulinda eneo lao la barabara litumike kama lilivyokusudiwa.
Manispaa ya Ilala pia wanawajibu wa kuwapanga wafanyabiashara hao, kama wameshindwa kuwajengea soko. Haiwezekani tukaishi kama nchi haina Sheria.