Mimi nafikiri una tatizo la ushabiki na unaipenda range rover na umeshajiaminisha kwamba Range Rover ndiyo gari na hakuna na haitakaa itokee gari kama range rover ambapo ni sawa kwa maana ni maoni yako lkn kwa taarifa yako tu range rover ina matatizo sana na siyo gari reliable, ina technical problem nyingi sana na wanashindwa kuuza kufikia malengo na kutengeneza faida na ndio maana hata Ford waliiuza kwa TATA kwa maana walishindwa kutengeneza faida kutokana na mauzo hafifu, wateja wengi wa Range Rover wanashindwa kuiuza baada ya muda fulani kwa maana ina resale value ndogo sana ukilinganisha na bei uliyonunulia sasa kwenye Car industry hivi ni vitu muhimu sana Mtu anaponunua gari huwa anaangalia resale value ya gari anayonunua kama unanunua gari kwa Dola 90 000 halafu baada ya miaka mitano huwezi hata kuiuza kwa dola 20 000 hiyo ni hasara!
Lakini ukinunua BMW X5 leo kwa dola 50 000 baada ya miaka mitano bado utaweza kuiuza kwa hata Dola 30 000 ina resale value kubwa na ndio maana BMW X5 wanauza sana kwa sababu iko reliable technically kwa wateja wao!
Hivyo Range Rover ni gari nzuri lakini technically bado hawaja perfect na wana matatizo sana kwenye reliability kwa wateja wao!