Benki zikizuiwa kukopesha wafanyakazi walioajiriwa hasa wa serikali zitakufa mara moja

Benki zikizuiwa kukopesha wafanyakazi walioajiriwa hasa wa serikali zitakufa mara moja

Uponyaji na uzima

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2015
Posts
1,000
Reaction score
2,129
Kitu kinaitwa Salaried Workers Loan (SWL) ndio chanzo cha mateso ya wafanyakazi maana wengi wanakopa kwa kufuata mkumbo.

Ukipata nafasi ya kuongea na maafisa mikopo wa benki na namna wanavyowawahi staff wapya wanapoajiriwa utaelewa namna nchi ilivyo na wajinga wengi.

Mtu katoka kuajiriwa na hapohapo anaingizwa kwemfumo wa utumwa. Siku serikali ikipiga marufuku hii mikopo benki nyingi zitapotea.
 
Hata kama Benki zinawafuata mwisho wa siku hazi walazimishi... Kukopa..
 
Hata kama Benki zinawafuata mwisho wa siku hazi walazimishi... Kukopa..
Watu waliposhawishiwa kwenye forex serikali iliingilia kati kuzuia watu kutuma dola nje kwa ajili ya hiyo biashara.

Serikali inalojukumu la kulinda wafanyakazi dhidi ya poachers wanaowaeleza watu uzuri bila kuwaonesha changamoto ya riba.
 
Mtu umemaliza degree hujui hata hesabu za riba tulizojifunza shule ya msingi bora uwe mtumwa tu? Saa nyingine watu wakishaajiriwa ni kama kuna ujinga unawaingia automatic. Unachukua mkopo bila kupiga hesabu za riba si upuuzi huo? Mbaya zaidi wengi wanachukua mikopo kwa mambo yasiyozalisha pesa.. wafanyakazi wapya huchukua mikopo ya kununulia magari kwa kisingizio "itarahisisha mizunguko"... pumbav sana. Nazipongeza benki kwa kazi nzuri.
 
Mtu umemaliza degree hujui hata hesabu za riba tulizojifunza shule ya msingi bora uwe mtumwa tu? Saa nyingine watu wakishaajiriwa ni kama kuna ujinga unawaingia automatic. Unachukua mkopo bila kupiga hesabu za riba si upuuzi huo? Mbaya zaidi wengi wanachukua mikopo kwa mambo yasiyozalisha pesa.. wafanyakazi wapya huchukua mikopo ya kununulia magari kwa kisingizio "itarahisisha mizunguko"... pumbav sana. Nazipongeza benki kwa kazi nzuri.
Elimu ya masuala ya fedha ni muhimu sana kuokoa vijana maana benki zinajipigia hela nje nje.
 
Elimu ya masuala ya fedha ni muhimu sana kuokoa vijana maana benki zinajipigia hela nje nje.
Mkuu hesabu za riba zinafundishwa shule ya msingi na sekondari. Kama mtu anashindwa hesabu rahisi hivyo naona aendelee tu kuwa mtumwa wa mabenki. Na ninachopenda maafisa mikopo huwa wanawaambia riba ni 4% kwa mwezi kumbe ni 4% ya mkopo wote na sio lile rejesho la mwezi. Ukipiga hesabu kwa miezi 6 unajikuta riba ni 24%. Ila hii 24% hawaitaji kabisa.
 
Back
Top Bottom