Taifa_Kwanza
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 443
- 86
Rafiki Bernard Saanane
Nimejawa na masikitiko makubwa sana baada ya kupata habari za kuenguliwa kwako
kwenye kinyang'anyiro cha Uenyekiti wa BAVICHA kwa sababu za kukiuka maadili ya uchaguzi.
Kitu pekee kinachonipa faraja ni kwamba kama binaadamu, Mwenye Mungu ameishaweka
msimamo wake juu ya makosa yote tuyafanyayo, kwamba Tukitubu na kuomba msamaha
atatusamehe hata tukiwa tumechafuka na kuwa wekundu kama damu.Nafarijika sababu
natambua kwamba unanafasi ya kutubu na kusamehewa, Ni mategemeo yangu kwamba
utaitumia fursa hii adhimu.
Naleta maombi haya kwako, kwamba zaidi ya kuomba msamaha kwa Mwenye Mungu, uje
pia hapa jamvini na kuomba msamaha, sio kujitetea - sababu sisi hatuna mamlaka ya kuku
samehe wala kufanya maamuzi yoyote juu ya maswahibu yaliyokukuta,lakini kwa nafasi
uliyokuwa nayo katika mioyo ya watu wengi hapa jamvini, kutokana na misimamo, itikadi,
ufahamu, uelewa, uungwana na machungu uliyotuaminisha kuwa nayo juu ya mstakabali
wa nchi yetu umetuacha vinywa wazi kwamba hata wewe ulikuwa radhi kukiuka taratibu
za uchaguzi ndani ya chama chako ili upate ushindi.
Nasikia ulifikia hatua ya kusema unaweza kujitoa, sina hakika kama ni kujitoa kwenye
chama au kwenye uchaguzi, kama ni kweli ulitoa kauli na ya namna hii basi inaonyesha
kwamba utoto bado unakusumbua.
Nisikuchoshe kwa maneno mengi sana, lakini nakukumbusha wajibu wako wa kurudi hapa
jamvini na kutuomba msamaha sababu wakati unatangaza nia, uliweka hapa maelezo yako
ya kina, yenye kuvutia na kutia moyo juu ya uwezo wako wa kuwa kiongozi.
Naomba utambua kwamba nakuandia wewe sababu ni wewe pekee ndiye uliyetabulika
hapa kama mgombea huko BAVICHA, wengine sikuwaona, hao watawajibika katika
communities ambazo waliziamisha kuwa ni tunu kwa taifa letu.
Jitie nguvu kama Mwanamme uombe msamaha, maisha yaendelee.
Nimejawa na masikitiko makubwa sana baada ya kupata habari za kuenguliwa kwako
kwenye kinyang'anyiro cha Uenyekiti wa BAVICHA kwa sababu za kukiuka maadili ya uchaguzi.
Kitu pekee kinachonipa faraja ni kwamba kama binaadamu, Mwenye Mungu ameishaweka
msimamo wake juu ya makosa yote tuyafanyayo, kwamba Tukitubu na kuomba msamaha
atatusamehe hata tukiwa tumechafuka na kuwa wekundu kama damu.Nafarijika sababu
natambua kwamba unanafasi ya kutubu na kusamehewa, Ni mategemeo yangu kwamba
utaitumia fursa hii adhimu.
Naleta maombi haya kwako, kwamba zaidi ya kuomba msamaha kwa Mwenye Mungu, uje
pia hapa jamvini na kuomba msamaha, sio kujitetea - sababu sisi hatuna mamlaka ya kuku
samehe wala kufanya maamuzi yoyote juu ya maswahibu yaliyokukuta,lakini kwa nafasi
uliyokuwa nayo katika mioyo ya watu wengi hapa jamvini, kutokana na misimamo, itikadi,
ufahamu, uelewa, uungwana na machungu uliyotuaminisha kuwa nayo juu ya mstakabali
wa nchi yetu umetuacha vinywa wazi kwamba hata wewe ulikuwa radhi kukiuka taratibu
za uchaguzi ndani ya chama chako ili upate ushindi.
Nasikia ulifikia hatua ya kusema unaweza kujitoa, sina hakika kama ni kujitoa kwenye
chama au kwenye uchaguzi, kama ni kweli ulitoa kauli na ya namna hii basi inaonyesha
kwamba utoto bado unakusumbua.
Nisikuchoshe kwa maneno mengi sana, lakini nakukumbusha wajibu wako wa kurudi hapa
jamvini na kutuomba msamaha sababu wakati unatangaza nia, uliweka hapa maelezo yako
ya kina, yenye kuvutia na kutia moyo juu ya uwezo wako wa kuwa kiongozi.
Naomba utambua kwamba nakuandia wewe sababu ni wewe pekee ndiye uliyetabulika
hapa kama mgombea huko BAVICHA, wengine sikuwaona, hao watawajibika katika
communities ambazo waliziamisha kuwa ni tunu kwa taifa letu.
Jitie nguvu kama Mwanamme uombe msamaha, maisha yaendelee.