Ben Saanane anastahili Tuzo CHADEMA

Ben Saanane anastahili Tuzo CHADEMA

Wassira ni shekhe? Nabii Danieli alikuwa shekhe?Wewe unamjua Yehoyakimu mfalma wa yuda? amin amin nakuambia.Haitachukua muda mrefu Ben tutakuwa naye CCM.

I am convinced so as well. CHADEMA ni kama tawi la CCM maana viongozi wake karibu wote wanaonekana mapandikizi.
 
Ataishia kujifungulia thread hivi mnafiki huyu Ben Saanane yupo? Tulishamsahau hebu tuhabarishe tuzo la mnafiki wa kaliba ya Ben Saanane ni nini?

Chama
Gongo la mboto DSM

Wewe CCM ni lazima umchukie kwa sababu ndiye alivuruga mpango wenu kuiua Chadema.Ni lazima utoke mapovu
 
Last edited by a moderator:
Wewe CCM ni lazima umchukie kwa sababu ndiye alivuruga mpango wenu kuiua Chadema.Ni lazima utoke mapovu

Mimi ni CCM wala halina kilificho ila sina sababu ya kumchukia mtu ambaye hata kumjua simjui zaidi ya kusoma unafiki wake JF; unajua mnafiki husahaulika haraka sana ndani ya mioyo ya waungwana na ndio sababu amekutumia wewe ili utuandikie utumbo kama huu; tuzo la mnafiki ni nini?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Kutokana na INTELEJINSIA ya Chadema ilivyo, ninaamini kabisa Zitto ameshatoswa na CCM baada ya kuwaacha kwenye Mataa. Nina imani kuwa alikuwa kiungo kizuri sana ili kupata SIRI za CCM na sasa hivi Kikwete kachukia na kaifuta POAC. Kwa hili ninakubaliana na Mchambuzixxx kuwa inawezekana. Hili nilishawahi kuliandika zamani kidogo ingawa sikuwa na ushahidi. Kama ni kweli, basi inabidi SISI WOOTE tuliomshambulia Zitto , basi tumuombe Msamaha kwa kufanya kazi nzito sana ya Chama kwa hatari hata ya kupoteza maisha kwa ajili ya WALIPA KISASI.

Ila hawa Chadema, isije kuwa wameenda hatua moja kubwa zaidi na siku moja ukaja kuta Juliana na Mwapamba nao ni Mashushushu ya Chadema (Trojan) waliokaribishwa ndani na Mwenyekiti mwenyewe na ukaja kuta siku za mwisho za mwaka 2015 kabla ya Uchaguzi, wakarudi Chadema kwa Nguvu kubwa na kumwaga siri zoote za CCM.

Viongozi watasema tu nini vijana walienda kukifanya na kwamba madhara waliyoyafanya ilibidi ili kuthibisha kuwa kweli wameichukia Chadema ingawa ukweli ukiangalia, hakuna madhara yoyote waliyofanya zaidi ya kurusha vimatusi na viskendo vya hapa na pale ambavyo havina miguu wala kichwa.

OGOPA SANA INTELEJENSIA YA CHADEMA. Huu ujumbe umfikie Rutashobanyuma .
 
Last edited by a moderator:
zitto ametafakari then kaona njia mbili moja ya hatari na nyingine yenye matumaini, hongera zitto
 
waswahili wanasema
"kikulacho ki nguoni mwako" na jini likujualo halikuli......................
 
Mimi ni CCM wala halina kilificho ila sina sababu ya kumchukia mtu ambaye hata kumjua simjui zaidi ya kusoma unafiki wake JF; unajua mnafiki husahaulika haraka sana ndani ya mioyo ya waungwana na ndio sababu amekutumia wewe ili utuandikie utumbo kama huu; tuzo la mnafiki ni nini?

Chama
Gongo la mboto DSM

Vipi utabiri wenu Chadema itakufa ndani ya mwaka mmoja bado ipo? Unacheza na Intelejensia ya Chadema nini!
 
Mnamuona saa8 ni mwema lakini huyo ni ndumbulakuwili hafahamiki undani wake yeye ni salia pia baada kuona mambo hayendi anavyotaka ndio akaamuwa kutaja hilo kundi la masalia kama yangekwenda vizuri amini mpaka leo bado angelikuwemo. mchawi mara nyingi humjua mchawi mwenzake.

Ni mtazamo wako, ila hata kama utakuwa sahihi kwa sasa Ben hero mtu anahukumiwa kwa yale anayoyatenda na sio hisia. Tusubiri atende hayo unayoyafikiri ndo tuje tumhukumu.Hizi tabia za utabiri zinaanza kuota mizizi kwa Watanzania kwa sababu ya kutojipa muda mzuri wa kufikiri. Ahsante kamanda Ben kwa kazi ya kufichua usaliti katika Chama.
 
Nami naungana na mleta mada Greenwhich kwa pongezi kwa Ben Saanane. Hata mimi nimempongeza sana wakati nikichangia thread ya hao masalia kuhamia CCM leo hii. Kuhusu Zitto Kabwe sikubaliani na wewe kwamba atakuwa amebadilika kwa kushiriki kazi za chama hasa matembezi ya tarehe 10/2/2013!! Naweza kusema ni fix tu!!! Zitto hayuko na CDM kizalendo, yuko pale kwa maslahi ya wanaomtumia!! Kilichamfanya Zitto pengine ashiriki yale maandamano na kumshambulia spika ni kwa bile ule ulaji wake kupitia Kamati aliyokuwa anaiongoza ya kuandalia utendaji na matumizi ya mashirika ya umma POAC ilibomolewa na yule Spika wetu mpendwa!!!! Hii si dalili njema kwa Zitto na SSM yake!!! Kwa mantiki hi alikuwa analilia ulaji na si kulaani ama uendeshaji mbovu wa bunge from his heart au kushutumu kuwa Dr. Slaa alikuwa Rais halali kama Science ya Uchakachuaji isingekuwepo!!!! It doesn't click in my head!!! Ninaamini sana yale aliyoyasema Ben Saanane na sasa yanatimia!!! Kwani ile evidence ya communication ya simu na Zitto si iko wazi? Ni kwa vile CDM si chama cha kukurupuka hata Zitto alitakiwa awe kundi la kupokelewa SSM leo japo his mission failed!!! or aborted!!!

Long Live CDM!!! Hakuna kukata tamaa, wahamie SSM na vyama vingine vyote ili wabaki wazalendo wenye uchungu na hii nchi!! Maisha yamekuwa magumu na umaskini wa kukithiri kwa sababu watu wachache kupitia katika mirija ya kinyonyaji wananyonya watanzania bila huruma!!! Bora hata mbu na kupe, hata kunguni wakinyonya sana huwa wanazidiwa damu wanakufa!!!! Deeply, regreting tunakoelekea!!!

Ule umoja na uzalendo umekufa na tulichofanya ni kuliua Azimio la Arusha na kuja na Azimio la Zanzibar lililosabisha ubepari wa hali ya juu, wizi, ubadhirifu wa mali ya umma na matabaka lukuki, yakiwemo, maskini wa kutupwa leo hii hana nafasi kwa tajiri wa nchi hii, ni second citizen!!!
 
Haki ya nani hawa masalia watatapika pesa ya masisiem maana ule mwaka mmoja wa chadema ife umepita na haijafa sasa wamerudi kwao.......waandike maumivu!!!Hongera kamanda ben kwa kuyalipua haya masalia a.k.a nyoka la kibisa lisilokuwa na madhara!!!
 
Kazi haijaisha, namtia moyo kamanda asihofu vitisho,

Vergaz Marshal, Vitalius Meyers na Chung Lee walishinda na walisherehekea baada ya ujasusi wao kuzaa matunda ya ukombozi!

Falsafa hii naitoa kuwa baraka kwa Ben Saanane na kitengo chetu maalumu cha chama!

Ninawathibitishia wanachadema na wanachama wa chadema kuwa chama kinamuona mpaka rohoni binadamu yeyote muovu dhidi ya Chama chetu!

Tupo imara na tutakuwa imara daima katika nyanya zote kutetea na kulinda mapinduzi haya ya fikra za mtanzania na 2015 taifa litakuwa huru!
 
Kazi haijaisha, namtia moyo kamanda asihofu vitisho,

Vergaz Marshal, Vitalius Meyers na Chung Lee walishinda na walisherehekea baada ya ujasusi wao kuzaa matunda ya ukombozi!

Falsafa hii naitoa kuwa baraka kwa Ben Saanane na kitengo chetu maalumu cha chama!

Ninawathibitishia wanachadema na wanachama wa chadema kuwa chama kinamuona mpaka rohoni binadamu yeyote muovu dhidi ya Chama chetu!

Tupo imara na tutakuwa imara daima katika nyanya zote kutetea na kulinda mapinduzi haya ya fikra za mtanzania na 2015 taifa litakuwa huru!

Mkuu ujumbe wako ni mzito umeandika kama mwanamapinduzi hasa!
 
Tuzo ya nini? hapo huenda ni tofauti ya interest ndo maana akawalipua wenzie!!!
interest zingeendelea kuwa sawa angesema? tusifanye mind zetu kuwa cheap kiasi hiki.....

Dada yangu, toka lini mind za vijana wanaojipambanua kama ni wapiganaji wa kweli hapa JF zikawa expensive (proficient).

Wamarekani (CIA) wao walishaliona tatizo kama hili siku nyingi sana.. ukimaliza hiyo mission waliyokutuma na wewe wanakumaliza kwa vile wanajua huko mbeleni utakuwa ni tatizo. Sijui kama Ben Saanane alitumwa, lakini kwa jinsi inavyoonekana, aliamua kuwa kinyonga baada ya mission kudoda na akaamua kurudi na kujipenyeza ndani ya inner circle ya CDM kwa njia ya kuwasaliti wenzake. Kwa hilo amefanikiwa na hata kwa wenye fikra haba kama huyu aliyeleta uzi nao amewapata.

Kuna mengi yanakuja kwa Ben Saanane zaidi ya haya. Mtazidi kuandika sana pongezi na ku flood mate nyuzi kuonekana kama kuna positive response.

Kwa Kufanikiwa kucheza na vichwa vya vijana ambao ni political immaturity,, kwa hili Ben Saanane nakugongea LIKE
 
Ndio, ujasiri wa Ben ulitupa kujua undani wa mambo ambayo vingineyo yangebaki sirini kwa miaka mingi ijayo. Kwa hilo anastahili pongezi nyingi.

Personal message to Ben: Please keep your feet on ground. Politics just like many aspects of life is unpredictable and ruthless.
 
hamna kutoa tuzo,adhabu ibak palepale ili kila mtu ajifunze na awe na adabu!hata Zitto nahc atakua kwene adhabu nzito ndani ya chama aliyopewa kimyakimya ndo maana amebadilika siku hizi!CDM sio genge au kijiwe cha wahuni ambao unafikiri unaweza ukawasaliti kirahisi, it can cost even your last breath trying to do that.
TULIANZA NA MUNGU,TUNAENDELEA NAE NA TUTAMALIZA NAE..LONG LIVE CDM, LONG LIVE TZ.
 
Ukitafakari kwa umakini utagundua kuwa hili kundi limeanza kujipanga muda mrefu nadhani ni zaidi ya mwaka likiwa in the process to establish itself.
Kwa maana hiyo CCM wamefail kukamilisha mission yao waliyoipanga na kwa hakika walikuwa na matarajio makubwa kiasi kwamba ile PAYOFF projection iliwatia kiwewe akina wasirra hadi wakaropoka kuwa cdm has no life.

Lakini kwa sasa it will take them another two years ku-establish another dubious project, na tayari 2015 itakuwa imefika.
ccm imekula kwao ndiyo maana hata body language imetuonyesha jinsi walivyokuwa wamesinyaa wakati wa kuikao chao cha nec pamoja na kujiriwaza kwa kuwapokea masalia.KAAAAZI KWELI KWELI
 
Back
Top Bottom