Bei za Vifaa vya ujenzi wa nyumba

Bei za Vifaa vya ujenzi wa nyumba

aspen

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2011
Posts
501
Reaction score
166
Wana JF nimeuanzisha huu uzi makusudi kujua bei ya vifaa mbalimbali ya ujenzi wa nyumba naomba tuwe tunaweka bei ya vifaa tofautitofauti kusudi wanayojenga kwa awamu wajue pa kuanzia

Mod naomba usiunganishwe na ile ya Gharama ya kujenga tanzania
 
Last edited by a moderator:
Vifaa vya Ujenzi viko vya aina nyingi! Kuna vyakuanzia ujenzi na finishing we unataka kujua vyaaina gani?

Tuanze na vifaa vya kuanzia ujenzi, yaani matofali, cement, nondo, mchanga, kokoto, I-beam na mbao.
Wadau tunaomba bei zake na wapi vinapatikana ili tupeane urahisi wa kujenga.
Kila mchangiaji aseme bei anazotoa ni za wapi (yaani kama bei ni za Dar, Dodoma, n.k).
 
Mimi nadili na vifaa vya finishing hasa mabomba na maSink hivyo vyakuanzia cna ujanja navyo ngoja tuwasubiri wadau wengine!
 
Mimi nadili na vifaa vya finishing hasa mabomba na maSink hivyo vyakuanzia cna ujanja navyo ngoja tuwasubiri wadau wengine!

Mkuu weka gharama ya plumbing kwa nyumba ya kawaida
 
Inatakiwa useme nyumba ya kawaida kwa maana gan! Ili kujua rum ngapi kuna toilete ngapi hii itafanya kujua pia zitahitajika Hand wash Basin ngapi Ukishajua hivyo ndo unapiga Hesabu Pipe ngapi utatumia pamoja na Fittings zake! Ukisema nyumba2 yakawaida watu tunatofautiana Wengine nyumba ya kawaida kwao ni Ghorofa 1 or ya chini bt Rum 12 nk! Funguka Kiongoz!
 
~Tofali linaanza bei 700 mpaka 2000
~Cement mfuko 13500 mpaka 14000
~mchanga yebo 45000(evarage unaweza kupiga tofali mifuko 4),selela 90000 mifuko 10 na mende 180 vol 15.8m3 mifuko 22
~nondo mm12 sh 16000 na mm16 sh 30000
~kuchimba msingi wa sq110 ardh ya kawaida ni 60000
~kujenga tofali kozi ya chini mpaka ya 4 ni sh 200 kujenga ya 5 mpaka ya 8 sh 250 hadi 300 za juu
~kumwaga zege ni sh 10000 kwa kichwa mpaka liishe fundi atakushauri idadi ya watu ili liishe mapema si unaju zege halilali.
 
~Tofali linaanza bei 700 mpaka 2000
~Cement mfuko 13500 mpaka 14000
~mchanga yebo 45000(evarage unaweza kupiga tofali mifuko 4),selela 90000 mifuko 10 na mende 180 vol 15.8m3 mifuko 22
~nondo mm12 sh 16000 na mm16 sh 30000
~kuchimba msingi wa sq110 ardh ya kawaida ni 60000
~kujenga tofali kozi ya chini mpaka ya 4 ni sh 200 kujenga ya 5 mpaka ya 8 sh 250 hadi 300 za juu
~kumwaga zege ni sh 10000 kwa kichwa mpaka liishe fundi atakushauli idadi ya watu ili liishe mapema si unaju zege alilali.

Mkuu la 700 linapatikana wapi si litakua ni mchanga mtupu?Mkuu mbona bei zako ndogo sana hiyo nyumba inayojengwa ni ya kiwango cha kijijini au ni kwenye miji mikubwa kama Dar?
 
Mkuu la 700 linapatikana wapi si litakua ni mchanga mtupu?Mkuu mbona bei zako ndogo sana hiyo nyumba inayojengwa ni ya kiwango cha kijijini au ni kwenye miji mikubwa kama Dar?

Mzinga ukivuka daraja kutoka mbagala, upande wa kushoto jirani na ghala la mabomba ya gesi.
 
Bei ya vifaa inategemea na maeneo unayojenga,maeneo mengine mchanga/maji vinapatikana kiurahisi so bei inashuka

Experience yangu ya Chamazi/Mbande

Cement 14000-15000
Tofali 700-1000
Maji -3500-5000 @ pipa
Misumari -3500-4000 @kg
Mbao ft 10-12,000-13,000 kukodisha mbao 1500-2000 kwa siku
Nondo mm 12-16,000-17,000,mm 16 29,000-30,000
Mchanga lori tani 18-120,000-140,000
 
Mkuu la 700 linapatikana wapi si litakua ni mchanga mtupu?Mkuu mbona bei zako ndogo sana hiyo nyumba inayojengwa ni ya kiwango cha kijijini au ni kwenye miji mikubwa kama Dar?

Pesa yako kama una hela unaweza pata hata tofali la 2000,jamaa amekupa mchanganuo mzuri wa bei nafuu.Bei ya vifaa inatofautiana kutokana na maeneo kujenga mbezi haiwezi kuwa sawa na Kigamboni au Mbagala
 
Bei ya vifaa inategemea na maeneo unayojenga,maeneo mengine mchanga/maji vinapatikana kiurahisi so bei inashuka

Experience yangu ya Chamazi/Mbande

Cement 14000-15000
Tofali 700-1000
Maji -3500-5000 @ pipa
Misumari -3500-4000 @kg
Mbao ft 10-12,000-13,000 kukodisha mbao 1500-2000 kwa siku
Nondo mm 12-16,000-17,000,mm 16 29,000-30,000
Mchanga lori tani 18-120,000-140,000

Asante sana.
Vipi marine board na mirunda.?
 
Wana JF nimeuanzisha huu uzi makusudi kujua bei ya vifaa mbalimbali ya ujenzi wa nyumba naomba tuwe tunaweka bei ya vifaa tofautitofauti kusudi wanayojenga kwa awamu wajue pa kuanzia

Mod naomba usiunganishwe na ile ya Gharama ya kujenga tanzania

Mkuu Aspen umefanya jambo la maana sana kuanzisha uzi huu.

Mie niko kwenye ujenzi nasikia kuna watu mahali wanakodisha vifaa vya ujenzi kama mirunda na marine sheets.

Wanajamvi kama kuna mtu yeyote anaejua watu wanaokodisha vifaa hivyo naomba anijulishe.

Vilevile nasikia kuna mahali marine sheets na mirunda used vinapatikana kwa bei nafuu. Wanajamvi naomba tupeane taarifa za vifaa hivyo; mahali vinapopatikana pamoja na bei zake.
 
Last edited by a moderator:
Inatakiwa useme nyumba ya kawaida kwa maana gan! Ili kujua rum ngapi kuna toilete ngapi hii itafanya kujua pia zitahitajika Hand wash Basin ngapi Ukishajua hivyo ndo unapiga Hesabu Pipe ngapi utatumia pamoja na Fittings zake! Ukisema nyumba2 yakawaida watu tunatofautiana Wengine nyumba ya kawaida kwao ni Ghorofa 1 or ya chini bt Rum 12 nk! Funguka Kiongoz!

Au mwngine ni ya kawaid bt vyumba vyote vitatu ni self contained so lazma gharama za plumbing ziwe kubwa kuliko
 
ME NAANZA NA PLUMBING,BEI HIZI NI KUTOKA INDIAN STREET PANDE ZA CITY CENTER.
IPS Pipe 1/2 @ 13,000
Elbow 1/2@ 1000
Tee1/2@ 1000
Nipple 1/2@ 1000
Union 1/2 @ 1000
Socket 1/2 @ 1000
Get valve 1/2 9000
PVC Pipe 1 1/4 @ 7000
Elbow 1 1/4 @ 1000
Tee 1 1/2 @ 1000
Plug 1 1/4 @ 1000
PVC pipe 1 1/2 @ 8000
Elbow 1 1/2 @ 1500
Tee 1 1/2 @ 1500
Plug 1 1/2 @ 1000
Tan Jint kopo @ 5000
Nahan Trap 2500
Seal Tep @ 500
Kila la heri katika ujenzi wako mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Mimi nadili na vifaa vya finishing hasa mabomba na maSink hivyo vyakuanzia cna ujanja navyo ngoja tuwasubiri wadau wengine!
Mkuu naona umevitundika hapo kwenye avatar yako, naomba tafadhali unipe mchanganuo wa vifaa na gharama ya ufundi wa plumbinh, kibanda changu kipo katika hatua za kuingiza maji ndani
 
Mimi nyumba yangu ina vyumba 3 vya kulala, kati ya hivyo kimoja ni self contained, sitting 1,dinning 1, public toilet na public bathroom 1 na jiko 1.

Nyumba ina ukubwa wa 11.7m x13.4 yaani square mita 156.78

Je, hapo ninahitaji gypsum kiasi gani na itani-cost bei gani na pia tiles za kihispania au za kichina grade 1 za kiasi gani na zitani-cost bei gani?

Makadirio ya-base ktk bei maximum na minimum.

Nyumba ipo Dar es Salaam
 
Back
Top Bottom