Bei ya unga yapaa

Bei ya unga yapaa

Mbona imepanda toka kitambo zaidi ya miezi mitano katika kipindi ambacho nimenunua me mwenyewe bei ilikuwa 6000 na sasa kwingine ndio imefika 6500 mpaka 7000 mbona tutanyooka.
 
Kwani ukisema na bado mkuu ww utakuwa unakula mavi......au ww unaishi kwa shemeji yako?
Niishi kwa shemeji.....!!! Nalea wajukuu tafadhali. Ni mkulima ambaye nina akiba ya chakula cha kunitosha na wajukuu zangu muda mrefu.
 
Hamuelewi maisha ni magumu watu wamepunguza vyakula vya anasa mfano viazi, mchele, Na vyakula vingine Kama chips ambavyo watu walikuwa wanakula nyakati za jioni pia wababa wengi na familia zao walikuwa wakila kwenye migahawa, bar, na mahotelin. Sasa pesa hakuna watu wote wanakula sembe na dona majumani tena familia nzima wote chakula ni nyumbani. Hivyo mahitaji ya unga yameongezeka bei lazima ipande.
 
Tumezidi kulalama bwana. Hatuna jema wala baya cc nikulalamika tu
Tatizo hakuna mtatuaji... wote mpaka anayetakiwa au mwenye madaraka ya kutatua naye analalamika... SI UNAKUMBUKA BWANA YULE WA MUDA ULIOPITA ALIKUWA HAJUI KWA NINI TANZANIA NI MASIKINI, NA VILE VILE ASINGEWEZA KUFANYA MVUA INYESHE ILI UMEME UWEPO
 
~Kama kilo 5 ilikuwa 3500/= basi kilo moja ilikuwa 700/= na siyo 1000/= kama ulivyosema


~ Kwa sasa kama kilo 5 imepanda hadi kufikia 6000/= basi kilo moja itakuwa 1200/= na siyo 1400/= kama ulivyosema.

Now which is which!
Ww ndio unajichanganya,mwenzako katoa bei za jumla,na reja reja,mfn. 3500 ni jumla na ikiuzwa reja reja inauzwa 1000/kg
 
Zimepanda pengine ni msimu wa sikukuu, nadhani hii ni habari njema kwa wakulima wanaolia bei za mazao yao haiendani na kazi wanayofanya
Pia watu wengi watavutiwa kulima pia
Wiki 2 zilizopita nilikuwa wilaya ya Liwale mkoa wa Lindi, debe la mahindi liliuzwa sh. 16,000/=.
 
Jaman Uchumi umepanda hamjasikia jana Dr Mpango akisema walkja kuhakikiwa na Shirika la fedha Dunian(IMF)
 
Wafanyabiashara wa jumla na rejareja jijini Dar-es-salaami waalalamikia kupanda kwa bei ya unga wa sembe.

Kwa mujibu wa wafanyabiashara hao, mfuko wa kilo 5 umepanda bei kutoka shilingi 3500 mpaka kufikia shilingi 6000 na kilo moja ya unga imepanda kutoka shilingi1000 mpaka shilingi 1400.

Chanzo:
ITV
Ni ile ile eee ni ile ile x 2....Dar es Salaam mnasemaje?
 
Jaman Uchumi umepanda hamjasikia jana Dr Mpango akisema walkja kuhakikiwa na Shirika la fedha Dunian(IMF)
Ni kweli kabisa mkuu...ukisikia mtu analalamika ujue alikuwa mpiga DEAL tu. CCM mbele kwa mbele!
 
Back
Top Bottom