Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Nadhani chapisho kukubalika inategemea malengo ya publisher vilevile mengine yakiwa nje ya kusudi la mwandishi....Pengine reviewer akaona inavutia wasomaji wengi na kusababisha debate kubwa na kwajinsi hiyo ni worthy for it to be published!

Lakini swali langu ni objective ya wewe kuiandika hiyo history upya nini? Ku promote hiyo category ya waleta uhuru, kuleta umoja wa kitaifa ama ku create academic debates? Ama ni for personal benefits, kama academic recognition, kutetea imani ama tu ni kufurahia religious debates?

Ame,
Lengo langu lilikuwa kuandika historia ya wazee wangu na mchango wao
katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
The big , nadhani Mohamed anapoweka paper na mabandiko yake nikufahamisha, kuelewesha na kutoa ufafanuzi. Na katika hayo lazima kuwe na ‘critique'

Kisomi si lazima kila mtu aende kufanya tafiti. Kupitia ‘critique'ndipo mambo mengine yanapojitkeza.
Labda kama imekusudiwa kuwa anayoandikaMohamed ni ya kumeza tu


Nyuzi nyingi tumewahi kumwambia Mohamed kuwa historia anayoandika imejikita katika upande mmoja. Huwezi kusahihisha kosa kwa kufanya kosa.

Kwa bahati mbaya, mzee ni mgumu sana wa kuelewa. Mag3 aliwahi kumuuliza nani alianzisha TAA. Mohamed kasema ni Kleist Sykes . Mag3 katoa ushihidi wa Mwalimu C.Matola ambao Mohamed hakuupinga.Ndicho anachosema prof kuwa historiailiyokuwepo ilikuwa na matatizo, na matatizo hayo yameendelezwa na Mohamed kwakuficha ukweli akiegemea katika Imani.

Mohamed mara nyingi na hasa uzi wake wa mwisho amesema anaandika historia ili watu waelewe.
Ukisoma bandiko lake moja hapo, kwa kiwewe anajikuta anazungumzia Imani badala ya historia.
Halafu anataka vitabu vyake view katika mtaala. Unaona makosa ya mzee


Tuliwahi kumuuliza kama Abdul alikutana na Mwl mwaka 1950.Mohamed kasema ndivyo ilivyokuwa.
Tukamwekea ushahidi kuwa walikutana kabla yahapo. Leo anarudia kile kile alichowahi kukoselewa.

Nguruvi3,
Unarudi tena na Cecil Matola na habari zilezile na kunitilia maneno mdomoni.

Fungua uzi mpya huu mwachie Prof. Hirji.
Abdul hakupata kumjua Nyerere.

Alipelekwa kwake na Kasella Bantu mwaka 1952.
 
Nyakageni,
Hakuna malalamiko.

Nimeweka takwimu za Mzee Kondo kuongezea zile zilizowekwa na Prof. Hirji
ili wanajamvi na wao wazione.

Kuna kitu kimoja tu ningependa kukutanabaisha.
Chunga lugha yako.

Andika kiungwana.
Huu mnakasha wengi watafaidika ila mimi huwa siwezi kujadiliana "kihuni.'

"Mara Mwembechai mara..." epuka staili hii.
Hiyo si staili ya wasomi wanapojadili.

Wasomi hawabughudhiani.

Sisi tuna lugha zetu.
Mimi sina sababu kukudhania vingine ila wewe ni msomi.

Usiniangushe.

spread facts not fear

hebu anza kujibu kuhusu Prof Hirji's premises and conclusion moja baada ya nyingine
 
Ame,
Lengo langu lilikuwa kuandika historia ya wazee wangu na mchango wao
katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ok thanks.... Kama lengo ni wewe kuweka kumbukumbu then its done; tatizo linakuja pale ambapo unatamani iwe historia ya wote hapo nadhani histroy ni selfish subject, depending on objective inabakiza records za wale ambao ni extra ordinary so kwangu mimi nadhani Nyerere aliwafunika wote ndiyo maana record zetu zimejaa issue zake kuliko hao wengine; what do you think?

Maana yeye aliwazidi maujanja mpaka akawa kiongozi na kwa hiyo kwa nafasi yake akaweza kusababisha yale aliyoyafanya yakawa ndiyo historia ya nchi yetu....Hao wengine Mungu awabariki kwa wema wao kwa Taifa letu lakini ni ukweli pia hawakupata bahati aliyoipata Nyerere kuweza ku influence nchi na hivyo kupelekea historia zao kuandikwa. Kwakua umeiandika basi nadhani kama ni historia inayokubalika itajitetea yenyewe na itaingia tu kwenye records!
 
Unataka tuwasome watu wanao taka kutumia dini ya kiislamu kuficha udhaifu wao na kutafuta utukufu? Kitwana Kondo ni mmoja wa trustees wa Morogoro Muslim University mbona chuo kinawafia mikononi? Achana na wendawazimu wako wa kuwagawa Watanzania.
Timbilimu,
Huu ni mjadala tu ndugu yangu huna haja ya kunitukana.
Dhulma ndiyo iliyotugawa siyo kalamu yangu.
 
kwani Mohamed Said ni mtume hadi hutaki akoselewe?

Prof Karim Hirji is a well established guru with objective opinion lakini si Mohamed Said a subjective islamic extremist
Wapi nimekuambia hayo maneno kuwa sitaki Mohamed Said akosolewe? Mohamed Said kasema wazi siyo lazima mtu akubali alichokiandika, wewe ndiyo unataka tukubali alichokiandika huyo prof.
 
Ame, yaani huyu watu wanasumbuka sana. Lengo lake ilikuwa ni kwa ajili ya wazee wake. Kosa lake jina la hilo kitabu kuwa kiujumla, a nation without heroes halafu yeye heroes ni wazee wake tu. Hapa amewavutia wengi. Pengine bila hilo jina leo tusinge jadili haya.
 
Last edited by a moderator:
ni masheikh tu hakukuwa na wanaharakati wengine? Prof Hirji anasema Nyerere bado alipata upinzani hata baada ya uhuru toka kwa wanaharakati

Prof Hirji anasema Mohamed Said hakueleza sababu za makundi yote kuungana bila kujali dini wala kabila

Zaidi ya hapo kuna masheikh wamo ndani hadi wanalawitiwa na marais wote watano wa pande mbili za muungano ni "ndugu katika iimaan"
Kwani huyo Prof kaelezea sababu hao Masheikh kukamatwa baada ya Uhuru? Tunajadli history wewe unaleta masuala mengine yafungulie uzi tuje kujadili usichafue mjadala.
 
Wapi nimekuambia hayo maneno kuwa sitaki Mohamed Said akosolewe? Mohamed Said kasema wazi siyo lazima mtu akubali alichokiandika, wewe ndiyo unataka tukubali alichokiandika huyo prof.

wewe hata hueleweki, nakupotezea
 
Kwani huyo Prof kaelezea sababu hao Masheikh kukamatwa baada ya Uhuru? Tunajadli history wewe unaleta masuala mengine yafungulie uzi tuje kujadili usichafue mjadala.

nitake radhi, stop jumping on to a moving wagon dude!
 
Nyakageni,
Mimi babu yangu mkuu Samitungo Mwekapopo alikuja Tanganyika baada ya Berlin Conference akiwa askari katika jeshi la Kijerumani na alikuwa Shirati Bomani. Hakutokea Kigoma.
 
Nguruvi3,
Unarudi tena na Cecil Matola na habari zilezile na kunitilia maneno mdomoni.

Fungua uzi mpya huu mwachie Prof. Hirji.
Abdul hakupata kumjua Nyerere.

Alipelekwa kwake na Kasella Bantu mwaka 1952.

Na hapa ndio upotoshaji wako ulipojikita. Umewafanya watu waamini kuwa Nyerere alikuja Dar mara ya kwanza mwaka 1952 na ndio alipoanza kutambuliwa. Abdul kumjua Nyerere mwaka 1952 haina maana Nyerere alikuwa mgeni Dar. Sivyo? Nyerere alikuja Dar mara ya kwanza mwaka gani na alipokelewa na kina nani?
 
Nadhani hapa unamnukuru Kitwana Kondo mwaka 1999. Kama ilikuwa kweli basi sidhani kuwa mambo yatakuwa yamebadilika hadi leo.

Kwa kweli imani yako imefunika kila kitu unabakia tu kuamini chochote kile mradi tu kielezee mambo ya kuonewa kwa waislamu. Hata kama kimetungwa. Hivi kweli unaamini kuwa wanafunzi waliofanya mtihani darasa la 7 mwaka 1999 walikuwa asilimia 71 ni waislamu na asilimia 29 ni wakristo? Ukifanya hesabu za haraka haraka tu utaona kuwa waislamu Tanzania bara wapo kwa asilimia kubwa mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Tanga. Mikoa ya DSM, Tabora, na Kigoma ni mchanganyiko. Mikoa iliyobakia wakristo ni wengi kwa mbali sana.
Suala jingine ambalo hakuchuja ni kwamba 29+71=100, ana ushahidi gani kuwa wote waliofanya mtihani mwaka huo walikua waamini wa imani hizo? Ilhali kuna watu kibao nchi hii hawa amini ktk imani hizo mbili, yaani hawapo kanisani wala msikitini na asilimia 100 wanafunzi hao walikuwepo wakati huo na hata sasa wapo.
 
Back
Top Bottom