Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Hata historia aliyokuja nayo profesa si wengi tulipatamo kuisikia.
Tulipaswa kuisikia toka kwako ila wewe hukuambatanisha hicho kipande cha historia. Swali ni kwanini wewe hukuielezea? Were you biased? Sababu profesa haonyeshi kama kukupinga direct, ameongezea vitu ambavyo tulipaswa visoma toka kwako wewe muanzilishi wa hizi mada.
 
Sibonike,
Hujafikia makamu ya kufanya mnakasha na mimi. Toka mwanzo nilijua hutofika mbali.

Katika yote niliyokuwekea hapo mchango wako ndiyo huo? Basi nimekuwia radhi.

Ilitakiwa ujipime kwanza kabla.

Hiyo paper, "Tanzania a Country Without Heroes," niliitoa Nairobi kwenye kongamano la kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wa nchi za
Afrika ya Mashariki.

Watayarishaji walikuwa IFRA French Institute for Research in Africa /BIEA British Institute in East Africa.

Hawa jamaa ndiyo walionialika na kutoka Tanzania nilikuwa peke yangu.

Hili peke yake ingekujulisha moto wa maji unayotaka kuoga.

Pili paper yangu aliyepiga "critique," ni profesa. Sasa wewe hapa unaingiaje?

Hata ujanja huo huna?


Anza kujibu hayo madogo kwanza ndio uje kwenye mengine. Jibu hayo kwanza mengine yafuate!
 
Hata historia aliyokuja nayo profesa si wengi tulipatamo kuisikia.
Tulipaswa kuisikia toka kwako ila wewe hukuambatanisha hicho kipande cha historia. Swali ni kwanini wewe hukuielezea? Were you biased? Sababu profesa haonyeshi kama kukupinga direct, ameongezea vitu ambavyo tulipaswa visoma toka kwako wewe muanzilishi wa hizi mada.

haswaa na aliviacha makusudi kwa malengo ya ku incite uma wa kiislam
 
Haina shida nani alianza kuandika;...........

Umepotosha historia kwa kiwango kikubwa, . Unataka watu tuamini masimulizi hayo kwa sababu tu wewe umesema ukitumia kurunzi ya dini kutulazimisha kuona. Bahati mbaya wapo ambao wamekubali haya kwa sababu kutokubali kungewafanya wapoteze umoja ambao wanaamini unausimamia; umoja ambao msingi wake ni dini.

Mtu yeyote ambaye ataamua kukusoma kwa ukosoaji yakinifu kwa hakika atafikia mahitimisho hayo hayo aliyofikia Profesa na labda zaidi.

Mzee nwanakijiji unapojaribu kujadili masuala ya Mzee Mohamed Said basi jaribu kuwa makini sana na maneno yako.
Umeandika mengi yasio na tija lkn nataka nigusie point chache hapa.

Kwanza wewe kuandika kuwa maneno ya mzee mohamed ni ya kwake mwenyewe hilo Ni UONGO wa Wazi kabisa.
Mzee Mohmamed siku zote hutuwekea vitu ambavyo km wewe ni mtaka kujua ukweli wake basi atleast una pakuanzia na Vitabu vya historia Vipo vingi tu vya Waandishi Tofauti Na Yeye Mzee Mohamed ambavyo Unaweza kupata BAADHI ya reference japo Sio ZOTE.

Lkn Tatizo lenu kubwa umeliweka ktk Hio paragraph yako ya mwisho ambalo umesema, na nakuquote ".. Mtu yeyote ambaye ataamua kukusoma kwa ukosoaji yakinifu..."

Sasa toka lini atakae kuelewa anasoma kwa lengo la KUKOSOA?

Wewe na hao wenzako Kila akiandikacho Mzee Mohamed Said Mnakisoma kwa lengo la KUMKOSOA.!!

Nakuuliza, hii ni tabia Ya Mwenye kutaka kuelewa? Au Tabia ya Mlevi mpinzani wa timu za mpira?

Soma Kwa lengo moja tu! Nalo ni KUJIFUNZA.
Na Ikitokea Kuna issue ambayo Hukubaliani Nayo Basi Mzee Mohamed siku zote Yupo hapa Jukwaani kwa Ajili ya Kujibu Hoja zenu na maswali yenu.


Na mwisho hapo Unaposema Kuwa maneno yake mzee Mohamed Anayakubali Yeye peke yake. Hilo sio kweli hatta kidogo.

Kwa taarifa Tu Maneno ya mzee Mohamed Said Yanasomeka ulimwengu Mzima ktk Sehemu Mbalibali.
Na mzee huyu wala Hategemei JAMII Forum Kufikisha Ujumbe kwa jamii.

Sio km wengi wenu siku mlivyo,
Siku JF ikifungwa na Nyie wote mnakufa kifo cha Ghafla.

Siku njema.
 
Last edited by a moderator:
Prof Karim Hirji kanifurahisha aliposema wakati tunaandaa mitaala yetu UDSM kitengo cha Historia kilikuwa at its best in Africa! Tumepata uhuru wenye degree walikuwa wachache

Akapiga msumari kuwa

"Mohamed Said's claims are . . . . . . . . . EXTREME"

HUYU MZEE NI EXTREMIST

Tukiziita Sera za Chadema Extremist idea yule Dr wa tiba mbadala anarusha ngumi hewani.

We mtoto lini utaacha kuandika pumba?
 
Mohamed Said
There are many more people who can narrate a similar type of suffering under different circumstances. Your story does not tell us why the students managed to pass with Division One at O level. Was it because they were Christians or were taught in Islamic schools and the the headmaster was a Muslim? This person has decided to analyse everything using the lens of religion. Some students could analyse using the lens of witchcraft, gender, tribalism, political affiliation, etc. I went to school with some people who blamed their failure in school and life on someone else but nothing about themselves.

This person goes on to perform badly in life after school apparently because he was in a Mfumo Kristo. But there are many Christians who have a similar experience, whom should they blame? There are many Muslims who have done very well, what happened?

As for Prof. Njozi, I know what he stands for. He is a person I have interacted with many times but not in religious discussions. The government gave him to head the Morogoro Muslim University but my dear friend turned it into a Madrasa, again reflecting who he is.
 
Last edited by a moderator:
There are many more people who can narrate a similar type of suffering under different circumstances. Your story does not tell us why the students managed to pass with Division One at O level. Was it because they were Christians or were taught in Islamic schools and the the headmaster was a Muslim? This person has decided to analyse everything using the lens of religion. Some students could analyse using the lens of witchcraft, gender, tribalism, political affiliation, etc. I went to school with some people who blamed their failure in school and life on someone else but nothing about themselves.

This person goes on to perform badly in life after school apparently because he was in a Mfumo Kristo. But there are many Christians who have a similar experience, whom should they blame? There are many Muslims who have done very well, what happened?

As for Prof. Njozi, I know what he stands for. He is a person I have interacted with many times but not in religious discussions. The government gave him to head the Morogoro Muslim University but my dear friend turned it into a Madrasa, again reflecting who he is.

KVM,
Ningependa Prof. Njozi angekuwapo hapa akakujibu mwenyewe. Juu ya hayo...

Kwani madrasa ina ubaya gani? Mimi nimesoma mengi ninayochangia hapa katika madrasa.

Kubwa nililofunzwa katika madrasa ni adabu ya mnakasha.
Yaani adabu ya mjadala.

Elimu hii alinifunza Maalim Haruna. Allah amrehemu.

Sasa ni juu yako kunipima kama elimu ile imenifaa au vipi.

Dada yangu Faiza husema sisi tunakwenda chuoni tukiwa wadogo na nyie wenzetu mnaingia chuoni watu wazima.

Mengine nimeyaacha kuyajibu kwa makusudi.
 
KVM
"Lakini tuende kielimu. Ninayo ripoti ya mwaka huu. Waliofanya mtihani wa darasa la saba kuingia darasa la tisa, asilimia 71 Waislamu. Asilimia 29 ni wengine. Walioshinda katika wale asilimia 71 ni asilimia 21. Katika wale 29 walioshinda tena sema mwenyewe. Katika asilimia 29 waliokwenda shuleni ni asilimia 79.

Katika asilimia 71 waliokwenda darasa la tisa ni asilimia 21. Sasa kuna moja, ama Waislamu wajinga ama akili yao haifanyi kazi, ama mtu ukiwa Muislamu wewe huna kitu, ama kuna kitu. Sasa namwomba Waziri anayehusika, anaposema aseme ya kwamba kwa hali ilivyo Waislamu wameumbwa wajinga. Au kwa hali ilivyo kuna sababu kadha, kadha.

Mwalimu Nyerere alisema zamani ifanywe bidii ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Sasa bidii hii siyo ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Bidii hii ni ya kuwakandamiza waliokuwa chini."

(Hotuba ya Kitwana Kondo Bungeni, 1999)
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mohamed Said, naona hata wafuasi wako humu wamekimbia! Nakupa ushauri kuhusu swala la prof Karim Hirji

MTU MZIMA AKIVULIWA NGUO HUCHUTAMA

Nyakageni,
Sina mfuasi hapa.

Nimeweka majibu na maelezo kadhaa kuhusu aliyosema Prof. Hirji. Sijapata jibu hata moja.

Bado sijavuka nguo. Sidhani kama Prof. Hirji anaweza akanivua msuli wangu.

Sijui nini ushauri wako.

Nyakageni,
Inaelekea wewe hunijui... Mimi naitwa Mohamed Said Salum Abdallah.

Ikutoshe kuwa nimeingia ukumbini na jina langu halisi. Sikujificha.

Hili halikuelezi jambo? Ihangaishe akili yako kidogo.

Au waulize wenzako hapa jamvini.
 
Mohamed Said
Nakufahamu sana, una wafuasi wengi sana humu hasa ukianza kutoa histohisia zako.
ritz, faiza, big show, kahtaan

Waliopo muda huu ni ritz na kahtaan

Nitapitia mabandiko yako baadaye kwa sasa niko na wafuasi wako wanaotoa matusi kwangu na kwa mama yangu
 
Last edited by a moderator:
Hao ndio wengine wenye mtazamo kama wa kwako. Kila kitu kinaangaliwa kwenye kurunzi ya kidini. Hivi Nyerere asingetaifisha shule za mission ili kila mtu bila kujali dini yake asome, hali ingekuwaje leo?

Tatizo la Said ni kuamini kuwa yeye pekee yuko sahihi na alichokiandika kana kwamba anachokihubiria wengine hawawezi kukijua. Afahamu kuwa kulikuwa na watu wengi walioshiriki ukombozi wa nchi hii wakiwa na watoto na wajukuu wanaokumbuka historia
 
KVM
"Lakini tuende kielimu. Ninayo ripoti ya mwaka huu. Waliofanya mtihani wa darasa la saba kuingia darasa la tisa, asilimia 71 Waislamu. Asilimia 29 ni wengine. Walioshinda katika wale asilimia 71 ni asilimia 21. Katika wale 29 walioshinda tena sema mwenyewe. Katika asilimia 29 waliokwenda shuleni ni asilimia 79.

Katika asilimia 71 waliokwenda darasa la tisa ni asilimia 21. Sasa kuna moja, ama Waislamu wajinga ama akili yao haifanyi kazi, ama mtu ukiwa Muislamu wewe huna kitu, ama kuna kitu. Sasa namwomba Waziri anayehusika, anaposema aseme ya kwamba kwa hali ilivyo Waislamu wameumbwa wajinga. Au kwa hali ilivyo kuna sababu kadha, kadha.

Mwalimu Nyerere alisema zamani ifanywe bidii ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Sasa bidii hii siyo ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Bidii hii ni ya kuwakandamiza waliokuwa chini."

(Hotuba ya Kitwana Kondo Bungeni, 1999)

Nadhani hapa unamnukuru Kitwana Kondo mwaka 1999. Kama ilikuwa kweli basi sidhani kuwa mambo yatakuwa yamebadilika hadi leo.

Kwa kweli imani yako imefunika kila kitu unabakia tu kuamini chochote kile mradi tu kielezee mambo ya kuonewa kwa waislamu. Hata kama kimetungwa. Hivi kweli unaamini kuwa wanafunzi waliofanya mtihani darasa la 7 mwaka 1999 walikuwa asilimia 71 ni waislamu na asilimia 29 ni wakristo? Ukifanya hesabu za haraka haraka tu utaona kuwa waislamu Tanzania bara wapo kwa asilimia kubwa mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Tanga. Mikoa ya DSM, Tabora, na Kigoma ni mchanganyiko. Mikoa iliyobakia wakristo ni wengi kwa mbali sana.
 
Hata historia aliyokuja nayo profesa si wengi tulipatamo kuisikia.
Tulipaswa kuisikia toka kwako ila wewe hukuambatanisha hicho kipande cha historia. Swali ni kwanini wewe hukuielezea? Were you biased? Sababu profesa haonyeshi kama kukupinga direct, ameongezea vitu ambavyo tulipaswa visoma toka kwako wewe muanzilishi wa hizi mada.

Na angetakiwa kumshukuru Prof kwa kuongezea pale penye mapungufu
 
KVM
"Lakini tuende kielimu. Ninayo ripoti ya mwaka huu. Waliofanya mtihani wa darasa la saba kuingia darasa la tisa, asilimia 71 Waislamu. Asilimia 29 ni wengine. Walioshinda katika wale asilimia 71 ni asilimia 21. Katika wale 29 walioshinda tena sema mwenyewe. Katika asilimia 29 waliokwenda shuleni ni asilimia 79.

Katika asilimia 71 waliokwenda darasa la tisa ni asilimia 21. Sasa kuna moja, ama Waislamu wajinga ama akili yao haifanyi kazi, ama mtu ukiwa Muislamu wewe huna kitu, ama kuna kitu. Sasa namwomba Waziri anayehusika, anaposema aseme ya kwamba kwa hali ilivyo Waislamu wameumbwa wajinga.

I doubt the authenticity of your data au guru wako uliyem quote, kwanza umejuaje waislam na wakristo waliomaliza darasa la saba? Hakuna form inayoonesha dini, TSM9 haziandiki dini na pia ni siri

pili, hebu fanya na utafiti kuhusu matatizo ya wanafunzi hapa Dar hasa yanayotokana na kutengana kwa wazazi hivyo kuingia kwenye ngono at teen age
 
Last edited by a moderator:
Nadhani hapa unamnukuru Kitwana Kondo mwaka 1999. Kama ilikuwa kweli basi sidhani kuwa mambo yatakuwa yamebadilika hadi leo.

Kwa kweli imani yako imefunika kila kitu unabakia tu kuamini chochote kile mradi tu kielezee mambo ya kuonewa kwa waislamu. Hata kama kimetungwa. Hivi kweli unaamini kuwa wanafunzi waliofanya mtihani darasa la 7 mwaka 1999 walikuwa asilimia 71 ni waislamu na asilimia 29 ni wakristo? Ukifanya hesabu za haraka haraka tu utaona kuwa waislamu Tanzania bara wapo kwa asilimia kubwa mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Tanga. Mikoa ya DSM, Tabora, na Kigoma ni mchanganyiko. Mikoa iliyobakia wakristo ni wengi kwa mbali sana.

KVM, mimi ninachokiona kwenye akili ya mzee wetu ni GARBAGE IN, GARBAGE OUT kwani kalishwa matango pori naye analisha matango pori wafuasi wake

ni kweli mikoa ya Pwani ina birth rate kubwa sana ila pia death rate ni kubwa
 
Last edited by a moderator:
I doubt the authenticity of your data au guru wako uliyem quote, kwanza umejuaje waislam na wakristo waliomaliza darasa la saba? Hakuna form inayoonesha dini, TSM9 haziandiki dini na pia ni siri

pili, hebu fanya na utafiti kuhusu matatizo ya wanafunzi hapa Dar hasa yanayotokana na kutengana kwa wazazi hivyo kuingia kwenye ngono at teen age
Na hawa hapa ni wa Dar es Salaam.

WANAFUNZI 1067 wa shule za sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma wameacha masomo katika miaka minne kutokana na tatizo la mimba na utoro, imeelezwa. Ofisa Elimu Sekondari wa Halmashauri hiyo Saverina Misinde alisema hali inaendelea kudumaza elimu hasa kwa watoto wa kike.

Alikuwa akitoa mada katika kikao cha wadau wa elimu katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Kikao hicho kiliwashirikisha wakuu wa shule, waratibu elimu na wadau wengine kuangalia hali ya elimu katika halmashauri hiyo.

Alisema mwaka 2009 wanafunzi 46 waliacha masomo kwa mimba huku watu waliohusika kufanya vitendo hivyo hawakuchukuliwa hatua za sheria baada ya wazazi kutotoa ushirikiano kwa walimu na vyombo vya dola.

Misinde alisema hakuna hatua madhubuti ambazo zinachukuliwa kuwawajibisha wahusika kwa vile wanapofikishwa mahakamani wanafunzi waliopewa mimba hukataa kutoa ushahidi.

Alisema mwaka 2009 wanafunzi 331 walikatisha masomo kwa utoro huku lawama pia zikielekezwa kwa wazazi ambao wamekuwa wakiwaona watoto wao wakikaa nyumbani bila kuchukua hatua.

Ofisa elimu huyo alisema mwaka 2010 wanafunzi tisa walipata mimba wakati mwaka 2011 wanafunzi wanane walipata mimba na mwaka 2012 wanafunzi 10 walikumbwa na tatizo hilo huku katika kipindi hicho, wanafunzi 663 walikatisha masomo kwa utoro.

Akichangia katika suala hilo, Ofisa Elimu mstaafu wa Mkoa wa Mara, Nashon Otieno alisema tatizo la mimba kwa wanafunzi ni jambo kubwa linalohitaji kila mdau kuona kuwa ni changamoto inayohitaji mkakati wa ushirikiano kutoka kwa kila mmoja.



Chanzo: MTANZANIA.
 
Teh teh teh.

Mudeeer bila shaka weeengi watatoka mapangoni kuja kuuzima moto huu uliouwasha na kujaribu kupoza joto ya jiwe.

Lakin ndiyo basi tena.

Ukweli ukishasemwa huwa kinachobakia ni kutapa tapa kwa wale waliokawa wanakumbatia uwongo na kujitamba nao.

Huyo Propesa kama alikuwa anayajua hayo mapungufu miaka yoote hiyo kipi kilimfanya asiandike??


Teh teh teh

Mudeer nimefurahi sana kwa majibu yako pia NIMESTAAJABU KUMUONA MZEE MWANAKIJIJI AKISHUPALIA MAANDIKO YA HUYO PROPESA KINDAKI NDAKI NAMNA HIYO TEH TEH TEH

YEYE SI ALISEMA ATAANDIKA KITABU KUANDIKA UKWELI??


MBONA MIAKA INAZID KWENDA HANA ANDIKO LOLOTE??

TEH TEH TEH

MUDEER SISI TUPO HAPA TUNAKUSOMA.
Sibonike,
Usiwe na haraka ya kutoa hukumu.
Mjadala ndiyo kwanza unaanza.

Ila nitakudokeza moja tu.
Prof. Hirji awe kama atakavyokuwa.

Hakubeba mzigo waliobeba Waislam katika ukoloni toka Wajerumani
hadi Waingereza.

Ukitaka kujua mtoto yatima anahisi vipi kufiwa na wazazi wake wawili
muulize mwenyewe.

"mwanangu siku ya Iddi watoto wenzako wamevaa nguo
mpya wamenunuliwa na baba zao wewe huna umejikunyata kibarazani
na matambaa?"

Jibu lake litakusogeza kwenye ukweli na uhakika.
Prof. Shivji hajapita tulipopita sisi.

Atazungumza na shingo kutoa kwa kuwa hana hata uzoefu wa mtoto
wa shangazi yake katika haya Waislam wanayolalamika.

Suali moja nitapenda Prof. Hirji anijibu.
Upungufu katika historia ya Tanganyika aliujua lini?

Aliujua kabla au baada ya Mohamed Said kuusema?
Ikiwa aliujua kabla kipi kilimfanya akae kimya siku zote hizi?

Uoga au kitu gani?
 
Tatizo la Said ni kuamini kuwa yeye pekee yuko sahihi na alichokiandika kana kwamba anachokihubiria wengine hawawezi kukijua. Afahamu kuwa kulikuwa na watu wengi walioshiriki ukombozi wa nchi hii wakiwa na watoto na wajukuu wanaokumbuka historia

Wakati mwingine tubishana naye ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu. Anachojua ni kwamba waislamu wanaonewa basi. Kuna hoja nyingine kwa makusudi hataki kujibu. Tatizo anapotosha wengi.

To be honest kuna sehemu anakuwa na hoja lakini kamwe hawezi kuangalia upanda wa pili. Umeona Prof. Hirji alikuwa alikuwa anaangalia pande zote. Juzi imetokea ESCROW na watu wenye mawazo finyu wanasema wahusika ni wakristo. Kiongozi mkuu wa nchi na makamu wake ni waislamu. Ina maana wamekaa kimya wakati hao wakristo wanatafuna ma hela ya ESCROW.
 
Back
Top Bottom