My cousin K. HIRJI is an opportunist trying to sacrifice Prof. Mohammed Said at a behest of publicity that is all. Indeed if Mr. Mohammed Said had not dared written this version of history Karim would not peep out of his comfort zone.
Mzee Mwanakijiji anaita historia za hisia "HISTOHISIA"
Prof Karim anasema beating drums on one side confusing both
jiulize tena mzee Mohamed Said kwa nini kitabu chako hakipo Tanganyika Library? UDSM ni marufuku kukitumia kama rejea! Kwa nini?
Nyakageni,
Mwanakijiji mweke pembeni.
Yeye nilimpa changamoto ya kuandika historia ya kweli kama anavyoiona
yeye.
Usimlete katika mjadala huu.
Huu ni uwanja wa Prof. Hirji na wengine.
Kuna ushahidi huu nimeuleta hapa nimependa kusikia majibu:
Katika uzi huu nimeweka kisa cha Sergeant Rashid Zahaki kama kilivyoandikwa
na Prof. Njozi katika kitabu chake "Muslims and the State in Tanzania.''
Ningependa kusikia majibu labda kutoka kwa wahusika kuwa Wizara
ya Elimu haikuhujumu vijana wa Kiislam walifanya mtihani ile.
Nimeweka pia hutoba ya Mzee Kitwana Kondo ndani ya Bunge mwaka 1999
alivyoonyesha dhulma katika elimu kwa vijana wa Kiislam.
Ningependa pia kusikia Wizara ya Elimu ikitoa kauli kuwa haihujumu vijana
wa Kiislam katika elimu.
Itakuwa bora badala ya mtu kuleta majibu ya kufagia akaja na majibu ya
maana kujibu ushahidi huo nilioweka.
Maelezo ya Zahaki kama yalivyoelezwa na Prof. Njozi yako hapa katika uzi.
MAUWAJI YA MSIKITI WA MWEMBECHAI 1998 - Mohamed Said
Maelezo ya Mzee Kondo pia yako hapa katika uzi.
Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999 - Mohamed Said
Matumbo,
Nukuu ndiyo ushahidi wa majibu ya maswali.
Ukikataa nukuu yaani rejea sasa hapa tutatunia nini kutia uzito hoja zetu?
Critique haitoshi kujibu kitabu changu.
Nitakupa mfano mdogo kutoka kwako mwenyewe.
Kabla ya mimi kuandika habari za Abdul Sykes wewe ulimjua na uliyajua
yote aliyofanya katika TAA, TANU na kwa Nyerere mwenyewe?
Hutoweza hata siku moja kunijibu kwa "critique," ikiwa mimi katika hayo
nimesema uongo.
Majibu ya uongo wangu utaweza kuyaleta kwa wewe kueleza ukweli.
Ukweli huu hutaweza kuueleza ila uandike kitabu.
Mimi nimejibu kitabu cha Historia ya TANU ya Chuo Cha Kivukoni si kwa
kupiga "critique" kile kitabu bali kwa kuandika ukweli.
Ndiyo leo tuko hapa tunajadili kitabu changu.
Lakini kwa nyinyi kukaa na kupiga "critique," hamtafua dafu.
Jibu ni kuja na kitabu kingine kitakachoeleza "ukweli."
Nyakageni,
Uongo unasema wewe.
Wahusika wako kimya.
Alimaanisha Prof Hirji, kiwewe kina mambo!!! mtu kashikwa tembe, inauma bwana!Mohamed Said Unamuuliza Prof. Hirji swali ambalo amekwisha lijibu katika makala yake tena kwa umakini mkubwa sana. Amezungumzia distortion ya historia sio Tanzania peke yake bali sehemu nyingi sana na mifano ametoa.
Hili pia linajibu hoja yako kwamba kwa nini hakuanza kueleza hadi wewe ulipotoa mawazo yako. Bila shaka amekerwa na upotoshaji wako. Kila kitu unakieleza kama uonezi kwa kwa waislamu. Angalia kumbe wakati wa utawala wa mjerumani waislamu walitumika sana na wakoloni hao kufanikisha mambo yao. Waingereza waliofuata waliwatumia wakristo. Katika awamu hizo, wakoloni hawakuwa na mapenzi na ama waislamu au wakristo - waliangalia maslahi yao tu.
Sina uhakika Prof. Shivji ameingiaje katika hoja yako!
Mohamed Said anazeeka vibaya, ona sasa anavyoumbuka.
Nyakageni,
Mbona hili swali umelipeleka sipo?
Swali hili ungewauliza Tanganyika Library na Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Kongwamaji,
Mimi naijua historia ya TANU kuliko mtu yoyote hapa JF.
Ikiwa wewe unamjua yeyote yule anaeweza kupambana na mimi katika historia hii mlete.
Nyakageni,
Uongo unasema wewe.
Wahusika wako kimya.
Wahusika ni akina nani? Its people who make history
Prof Hirji kagundua premises zako, moja ni hii kuwa the government is against islam!
na kasema conclusion yako ni animosity inayolenga kugawa watu kidini
Matumbo,Wanasema mara nyingine ukimya ndio jibu la mjinga . Uhenda wametumia falsafa ya mpuuzi mpuuze.
Alimaanisha Prof Hirji, kiwewe kina mambo!!! mtu kashikwa tembe, inauma bwana!
Tulichowahi kusema ndicho alichosema Prof. Tukaambiwa hatupo Oxford library
nyakageni,
hayo mimi si wa kwanza kuyasema.
Msome bergen (1981), msome sivalon (1992), msome njozi (2000).