Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Mohamed said Mudeeer maandiko yako yameufungua ulimwengu.

Reactions tunaziona sasa.
 
Wakati mwingine tubishana naye ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu. Anachojua ni kwamba waislamu wanaonewa basi. Kuna hoja nyingine kwa makusudi hataki kujibu. Tatizo anapotosha wengi.

To be honest kuna sehemu anakuwa na hoja lakini kamwe hawezi kuangalia upanda wa pili. Umeona Prof. Hirji alikuwa alikuwa anaangalia pande zote. Juzi imetokea ESCROW na watu wenye mawazo finyu wanasema wahusika ni wakristo. Kiongozi mkuu wa nchi na makamu wake ni waislamu. Ina maana wamekaa kimya wakati hao wakristo wanatafuna ma hela ya ESCROW.

Mzee Mwanakijiji anaita historia za hisia "HISTOHISIA"

Prof Karim anasema beating drums on one side confusing both
 
Mohamed Said
Huyo Njozi nimeshamsoma vizuri tu kwenye mahandishi yake ni tabia zile zile kulialia na iman yake akisema 'tunaonewa'.

Licha ya kumsoma nimemshudia utendaji wake wa kazi nilipofanya ziara chuo kikuu cha kiislamu Morogoro kihonda, ni aibu sana mtu aliyepiga kelele dunia yote kwamba waislamu wanaonewa kwenye elimu kakabidhiwa chuo chenye raslimali zote na sasa kinamfia mikononi. Ama kweli mchawi mpe mwana alee.

Hapa kulinda heshima yenu ni vyema ungejikita kwenye kumjibu Profesa ungekuwa umefanya la maana sana sababu unapoanza kukimbia 'kidizain' inaonyesha ni kiasi gani uongo uliojaribu kuupandikiza kwa wenzako umeanza kukutafuna huku ukitazama. Lakini sisi tulikuonya siku nyingi ipo siku utaumbuka hukutaka kutusikia ukawa unainjoi kelele za wasiojielewa.

Mswiba mkubwa huu.
 
Last edited by a moderator:
Mi nilimuelewa mzee Said aliposema lengo ilikuwa ni kueleza historia ya wazee wake waliosahaulika katika historia. Hilo jina la kitabu kaliweka kuvutia wasomaji, ila maelezo ya ndani ni kwa ajili ya wazee wake. Kwa lengo lake hilo alifunga fikra zake kufikiria kuwa 'heroes' waliosahaulika au wasiotajwa si wazee wake tu.

Nimependa Prof Hijri alivyoeleza kuwa kwenye jamii yetu hii waliosondwa vidole vya uovu wanatoka makundi yote. Sijafanya tafiti ila nimeona kwa jamii. Na siku zote huwa nawashangaa wanao nasibisha uovu katika jamii na imani tulizoletewa. Mi naamini hata huko waliko wakristo wengi au waislamu wengi lawama za uonevu kati yao zipo tu, sembuse sie tulioletewa.
 
Nimependa sana namna Prof alivyomalizia paper yake, the hypothetical example and peoples` views.Very realistic.

Kudos Hirji.
 
Mi nilimuelewa mzee Said aliposema lengo ilikuwa ni kueleza historia ya wazee wake waliosahaulika katika historia. Hilo jina la kitabu kaliweka kuvutia wasomaji, ila maelezo ya ndani ni kwa ajili ya wazee wake. Kwa lengo lake hilo alifunga fikra zake kufikiria kuwa 'heroes' waliosahaulika au wasiotajwa si wazee wake tu.

Nimependa Prof Hijri alivyoeleza kuwa kwenye jamii yetu hii waliosondwa vidole vya uovu wanatoka makundi yote. Sijafanya tafiti ila nimeona kwa jamii. Na siku zote huwa nawashangaa wanao nasibisha uovu katika jamii na imani tulizoletewa. Mi naamini hata huko waliko wakristo wengi au waislamu wengi lawama za uonevu kati yao zipo tu, sembuse sie tulioletewa.

Double R,
Nakushukuru kwa mchango wako lakini ningependa sana kusikia kutoka kwa Prof. Hirji mwenyewe kutoka kwenye kinywa chake ni lini alipokujajua kuwa historia ya uhuru wa Tanganyika ina upungufu.

Na baada ya kusoma paper yangu, "Tanzania: "Nation Without Heroes," au kabla ya hapo?

Inawezekana wako wengi waliodhulumiwa lakini dhulma dhidi ya Waislam ina historia yake ya pekee.

Katika uzi huu nimeweka kisa cha Sergeant Rashid Zahaki kama kilivyoandikwa na Prof. Njozi katika kitabu chake "Muslims and the State in Tanzania.''

Nimeweka pia hutoba ya Mzee Kitwana Kondo ndani ya Bunge mwaka 1999 alivyoonyesha dhulma katika elimu kwa vijana wa Kiislam.

Itakuwa bora badala ya mtu kuleta majibu ya kufagia akaja na majibu ya maana kujibu ushahidi huo nilioweka.
 
matumbo
Hilo la MUM na Prof. Njozi tujaalie tunaweza tukaliingiza hapa lakini naona
ingependeza tupate jibu kutoka kwa muhusika mwenyewe.

Mimi niko na nyinyi kwenye paper yangu: "Tanzania: "A Nation Without Heroes"
na "critique" ya Prof. Hirji iliyoletwa hapa.
 
Last edited by a moderator:
Prof. Hirji mwenyewe kutoka kwenye kinywa chake ni lini alipokujajua kuwa
historia ya uhuru wa Tanganyika ina upungufu.

Na baada ya kusoma paper yangu, "Tanzania: "Nation Without Heroes,"
au kabla ya hapo?

Inawezekana wako wengi waliodhulumiwa lakini dhulma dhidi ya Waislam
ina historia yake ya pekee.

Katika uzi huu nimeweka kisa cha Sergeant Rashid Zahaki kama kilivyoandikwa
na Prof. Njozi katika kitabu chake "Muslims and the State in Tanzania.''

Nimeweka pia hutoba ya Mzee Kitwana Kondo ndani ya Bunge mwaka 1999

kajibu hilo swali mwisho kwa kutaja status yake na pia katoa sababu ya kwa nini anadhani kuwa itakuwa si sahihi

kumbuka kuhusu uchache wa wasomi wakati tunapata uhuru na ni kwa kiasi gani UDSM walijitahidi kwa wakati huo

issue ya Kitwana Kondo kusema 1999 wanafunzi waislam walikuwa 71% na wakristo plus wengineo 29% ni uongo. Kama Pinda tu anadanganya bungeni iwe Kondo?
 
Matumbo,
Hilo la MUM na Prof. Njozi tujaalie tunaweza tukaliingiza hapa lakini naona
ingependeza tupate jibu kutoka kwa muhusika mwenyewe.

Mimi niko na nyinyi kwenye paper yangu: "Tanzania: "A Nation Without Heroes"
na "critique" ya Prof. Hirji iliyoletwa hapa.

Lakini umeshindwa kujibu hoja zake, unachofanya ni kuleta nukuu kuonyesha ni namna gani waislamu wamekuwa wakilalamika.

Prof Hirji ameonyesha jinsi ni kiasi gani history inazungumza kuwa watu walipata magumu mengi lakini haikuwa sababu ya imani zao. Ameonyesha ni kiasi gani waafrika wa Tanganyika waliunganishwa na kiu yao ya kupata uhuru, kinyume na upotoshaji wako.
 
Mzee Mwanakijiji anaita historia za hisia "HISTOHISIA"

Prof Karim anasema beating drums on one side confusing both

Nyakageni,
Mwanakijiji mweke pembeni.

Yeye nilimpa changamoto ya kuandika historia ya kweli kama anavyoiona
yeye.

Usimlete katika mjadala huu.
Huu ni uwanja wa Prof. Hirji na wengine.

Kuna ushahidi huu nimeuleta hapa nimependa kusikia majibu:

Katika uzi huu nimeweka kisa cha
Sergeant Rashid Zahaki kama kilivyoandikwa
na Prof. Njozi katika kitabu chake "Muslims and the State in Tanzania.''

Ningependa kusikia majibu labda kutoka kwa wahusika kuwa Wizara
ya Elimu haikuhujumu vijana wa Kiislam waliofanya mtihani ule mwaka ule.

Nimeweka pia hutoba ya Mzee Kitwana Kondo ndani ya Bunge mwaka 1999
alivyoonyesha dhulma katika elimu kwa vijana wa Kiislam.

Ningependa pia kusikia Wizara ya Elimu ikitoa kauli kuwa haihujumu vijana
wa Kiislam katika elimu.

Itakuwa bora badala ya mtu kuleta majibu ya kufagia akaja na majibu ya
maana kujibu ushahidi huo nilioweka.

Maelezo ya Zahaki kama yalivyoelezwa na Prof. Njozi yako hapa katika uzi.
http://www.mohammedsaid.com/2014/02/rashid-zahaki-na-mauaji-ya-mwembechai.html
MAUWAJI YA MSIKITI WA MWEMBECHAI 1998 - Mohamed Said

Maelezo ya Mzee Kondo pia yako hapa katika uzi.
Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999 - Mohamed Said

Napenda ndugu zangu wanajamvi wenzangu mkatambua kuwa mimi siko hapa
kucheza ndiyo maana anapokuja mtu kama Prof. Hirji akahoji maandishi yangu
mimi najitahidi kw akila hali kumueleza kila ninachojua kwani watu kama wao
wana nafasi kubwa sana katika jamii ya kueleza ukweli na ukasikika na kusikilizwa
na viongozi wetu.

Mzee Kondo na Zahaki wamesema kweli si waongo.
 
Lakini umeshindwa kujibu hoja zake, unachofanya ni kuleta nukuu kuonyesha ni namna gani waislamu wamekuwa wakilalamika.

Prof Hirji ameonyesha jinsi ni kiasi gani history inazungumza kuwa watu walipata magumu mengi lakini haikuwa sababu ya imani zao. Ameonyesha ni kiasi gani waafrika wa Tanganyika waliunganishwa na kiu yao ya kupata uhuru, kinyume na upotoshaji wako.

Matumbo,
Nukuu ndiyo ushahidi wa majibu ya maswali. Ukikataa nukuu yaani rejea sasa hapa tutatunia nini kutia uzito hoja zetu?

Critique haitoshi kujibu kitabu changu. Nitakupa mfano mdogo kutoka kwako mwenyewe.

Kabla ya mimi kuandika habari za Abdul Sykes wewe ulimjua na uliyajua yote aliyofanya katika TAA, TANU na kwa Nyerere mwenyewe?

Hutoweza hata siku moja kunijibu kwa "critique," ikiwa mimi katika hayo nimesema uongo.

Majibu ya uongo wangu utaweza kuyaleta kwa wewe kueleza ukweli. Ukweli huu hutaweza kuueleza ila uandike kitabu.

Mimi nimejibu kitabu cha Historia ya TANU ya Chuo Cha Kivukoni si kwa kupiga "critique" kile kitabu bali kwa kuandika ukweli.

Ndiyo leo tuko hapa tunajadili kitabu changu. Lakini kwa nyinyi kukaa na kupiga "critique," hamtafua dafu.

Jibu ni kuja na kitabu kingine kitakachoeleza "ukweli."
 
Matumbo,
Nukuu ndiyo ushahidi wa majibu ya maswali.
Ukikataa nukuu yaani rejea sasa hapa tutatunia nini kutia uzito hoja zetu?

Critique haitoshi kujibu kitabu changu.
Nitakupa mfano mdogo kutoka kwako mwenyewe.

Kabla ya mimi kuandika habari za Abdul Sykes wewe ulimjua na uliyajua
yote aliyofanya katika TAA, TANU na kwa Nyerere mwenyewe?

Hutoweza hata siku moja kunijibu kwa "critique," ikiwa mimi katika hayo
nimesema uongo.

Majibu ya uongo wangu utaweza kuyaleta kwa wewe kueleza ukweli.
Ukweli huu hutaweza kuueleza ila uandike kitabu.

hapana mzee, prof kakosoa hoja zako nawe hebu mjibu kuonesha kuwa yeye ndiyo kapotoka na si wewe

nukuu za malalamiko si hoja, na kuhusu Sykes Abdul kweli historia imemtupa lakini prof Karim Hirji kasema credit goes to he who organised all kwani kudai uhuru ilikuwa ni national issue naye alikuwa Katibu kama sijakosea
 
Mkuu Mohamed Said

Hoja alizotoa Prof. Karim Hirji zinazima madai yako yote unayotoa sehemu mbalimbali juu ya kile unachokiita "kuonewa kwa waislam Tz". Hisia za UDINI ndio zinakuongoza. Na kwa jinsi hii ni ngumu kushawishi umma wenye kuweza kupambanua ukweli ni upi. Hoja zako ziko bias sana hata mtoto wa primary atatambua wewe ni MDINI. Ndiyo, wewe ni mdini kwa sababu unafungamanisha hali mbaya za waislam hapa nchini kuwa ni matokeo ya "mfumo Kristu" kitu ambacho si kweli. UNAWAGAWA WATANZANIA.

ACHA MARA MOJA.
 
Mkuu Mohamed Said

Hoja alizotoa Prof. Karim Hirji zinazima madai yako yote unayotoa sehemu mbalimbali juu ya kile unachokiita "kuonewa kwa waislam Tz". Hisia za UDINI ndio zinakuongoza. Na kwa jinsi hii ni ngumu kushawishi umma wenye kuweza kupambanua ukweli ni upi. Hoja zako ziko bias sana hata mtoto wa primary atatambua wewe ni MDINI. Ndiyo, wewe ni mdini kwa sababu unafungamanisha hali mbaya za waislam hapa nchini kuwa ni matokeo ya "mfumo Kristu" kitu ambacho si kweli. UNAWAGAWA WATANZANIA.

ACHA MARA MOJA.

prof Hirji kamwambia, anapigia ngoma upande mmoja na kuchanganya pande zote
 
Mwelewa,
Hapana haja ya kuniandikia kwa herufi kubwa.

Kitaalamu katika uandishi ni kuwa unanipigia makelele.

Mimi nina hoja zangu kama wewe ulivyokuwa na zako na mwingine pia.

Umeniita mdini na wengi washafanya hivyo.

Sijawakemea kwa vitisho.vya ACHA MARA MOJA ila narudi na hoja na kuueleza ukweli.

Kilichotugawa Watanzania kina historia ndefu na hayo unaweza kuyasoma katika kitabu changu na paper nilizowadilisha ndani na nje ya nchi.

Unaweza ukipenda kuingia katika blog yangu www.mohammedsaid.com.

Dhulma ndiyo iliyotugawa.
 
Mohamned Said kaachwa mtupu. Kuna vitu viwili muhimu sana hapa. Kwanza hoja za kisayansi za Prof. Hirji. Pili prof sio Mkristo maana kwa kurunzi ya Mohamned Said hilo lingekuwa tatizo.
Wanyonge wa Tanzania ni dini zote. Mafisadi wa Tanzania ni dini zote.

My cousin K. HIRJI is an opportunist trying to sacrifice Prof. Mohammed Said at a behest of publicity that is all. Indeed if Mr. Mohammed Said had not dared written this version of history Karim would not peep out of his comfort zone.
 
Nadhani hapa unamnukuru Kitwana Kondo mwaka 1999. Kama ilikuwa kweli basi sidhani kuwa mambo yatakuwa yamebadilika hadi leo.

Kwa kweli imani yako imefunika kila kitu unabakia tu kuamini chochote kile mradi tu kielezee mambo ya kuonewa kwa waislamu. Hata kama kimetungwa. Hivi kweli unaamini kuwa wanafunzi waliofanya mtihani darasa la 7 mwaka 1999 walikuwa asilimia 71 ni waislamu na asilimia 29 ni wakristo? Ukifanya hesabu za haraka haraka tu utaona kuwa waislamu Tanzania bara wapo kwa asilimia kubwa mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Tanga. Mikoa ya DSM, Tabora, na Kigoma ni mchanganyiko. Mikoa iliyobakia wakristo ni wengi kwa mbali sana.

Angalia mtu mwenyewe aliyetoa hizo takwimu. Asilia 71 kwa Dar es Salaam au mkoa wa Pwani labda. Nadhani kuna mtu alimpa hizo takwimu kama Kibajaji anavyopewa ya kuropoka maana uwezo wa kupembua hana. Kwanza ni lini wanafunzi wanaomaliza la saba huulizwa dini yao? Hata katika baadhi ya mikoa yenye waislam wengi wengi, mahudhurio mashuleni ni hafifu sana. Jamani tukubali ukweli mwamko wa elimu unatofautiana sana Tanzania hii. Kuna mikoa (si ya waislamu) watu wanahonga mifugo ili watoto wao waache shule!
 
My cousin K. HIRJI is an opportunist trying to sacrifice Prof. Mohammed Said at a behest of publicity that is all. Indeed if Mr. Mohammed Said had not dared written this version of history Karim would not peep out of his comfort zone.

There is nothing resembling an opportunist in what Prof. Hirji has written. The facts are so obvious for anybody to see. We better agree not to agree on that!
 
My cousin K. HIRJI is an opportunist trying to sacrifice Prof. Mohammed Said at a behest of publicity that is all. Indeed if Mr. Mohammed Said had not dared written this version of history Karim would not peep out of his comfort zone.

is it bad? Wamekosolewa waandishi wa Biblia, Koran sembuse mzee Mohamed Said?
 
Back
Top Bottom