micro_almunia
Senior Member
- Jan 16, 2011
- 134
- 37
Imefahamika kuwa, pamoja na kusajiliwa na TCU, kozi ya BCom inayotolewa na UDOM haitambuliwi na bodi za wataalamu (Professional Bodies kama NBAA, NBMM etc).
Hilo bado halijathibitishwa kwa kozi nyingine ukiacha BCom.
Habari za kuaminika kutoka NBAA zinasema UDOM bado hawakidhi 'vigezo' vya kutambulika japo haikutanabaishwa kwa wazi vigezo ni vipi.
Imeelezwa kuwa NBAA walikuwa na vyuo viwili vinavyoomba kutambulika (UDOM na St.John), lakini ilipitisha uamuzi wa kukitambua St.John na kukikataa UDOM.
Department inayohusika na BCom walipojaribu kuulizwa kuhusu hilo swala walisema, "hawajui". Vilevile, mkuu wa hiyo idara (anayefahamika kwa jina la Anna Njiku) amekuwa mara kadhaa akikata simu za wanafunzi waliomaliza wanaoulizia hilo suala.
Zaidi ya yote, idara hiyo imeelezwa kusambaza taarifa za uongo kwa wanafunzi wa BCom walioko chuoni kuwa tayari wamepata usajili. Mpaka sasa wanafunzi hao wanafikiri mambo yao ni mazuri, huku bodi zikithibitisha tofauti.
Taarifa kutoka NBAA zinaeleza kuwa, wao wanatambua Diploma ya biashara itolewayo na CBE ni bora kuliko BCom itolewayo na UDOM. Watu waliomaliza hiyo Diploma wameruhusiwa kuanzia ngazi ya module C, lakini watu toka UDOM wameambiwa wao ni ngazi ya module B.
SWALI: Je, waajiri wataendelea kuwachukua wahitimu waliokataliwa na professional bodies?
Hilo bado halijathibitishwa kwa kozi nyingine ukiacha BCom.
Habari za kuaminika kutoka NBAA zinasema UDOM bado hawakidhi 'vigezo' vya kutambulika japo haikutanabaishwa kwa wazi vigezo ni vipi.
Imeelezwa kuwa NBAA walikuwa na vyuo viwili vinavyoomba kutambulika (UDOM na St.John), lakini ilipitisha uamuzi wa kukitambua St.John na kukikataa UDOM.
Department inayohusika na BCom walipojaribu kuulizwa kuhusu hilo swala walisema, "hawajui". Vilevile, mkuu wa hiyo idara (anayefahamika kwa jina la Anna Njiku) amekuwa mara kadhaa akikata simu za wanafunzi waliomaliza wanaoulizia hilo suala.
Zaidi ya yote, idara hiyo imeelezwa kusambaza taarifa za uongo kwa wanafunzi wa BCom walioko chuoni kuwa tayari wamepata usajili. Mpaka sasa wanafunzi hao wanafikiri mambo yao ni mazuri, huku bodi zikithibitisha tofauti.
Taarifa kutoka NBAA zinaeleza kuwa, wao wanatambua Diploma ya biashara itolewayo na CBE ni bora kuliko BCom itolewayo na UDOM. Watu waliomaliza hiyo Diploma wameruhusiwa kuanzia ngazi ya module C, lakini watu toka UDOM wameambiwa wao ni ngazi ya module B.
SWALI: Je, waajiri wataendelea kuwachukua wahitimu waliokataliwa na professional bodies?