BBC Swahili Tumewachoka!

BBC Swahili Tumewachoka!

Yaani kila mifano ya ovyo ni Tanzania tu? Katika News report yao usiku huu wanatoa mifano ya sarafu zilizoporomoka na haraka wamekimbilia kutoa mfano wa shilingi ya Tanzania. Ni nini ninyi?

Tumewachoka sana kutudhalilisha kila siku! Kila jambo jema mnakimbilia Kenya. Mnatuudhi sana sana msione tumenyamaza!

Ndugu ukisemwa rudi ujipange ili umnyamazishe aliekusema kwa kurekebisha mapungu yako.
Ukisharekebisha hana cha kuandika hivyo BBC waliona upungufu wetu.
 
Usipende kudanganywa na tbc futa tabia ya kitanzania ya kupenda kudanganywa,bbc hawana upendeleo wowote wametangaza mabaya ya Kenya na mazuri halikadhalika na Tanzania hivyo hivyo , mfano leo wameongelea habari ya mila ya wanawake wakurya kuoana ,juzi waliongelea Tanzania ni ya nne Africa kuzalisha gold kwa kiasi cha dola bilioni 1.6 kwa mwaka,wameongelea sehemu maarufu duniani za ngorongoro,Serengeti na kilimanjaro nk vile vile wamemzungumzia lowasa alivyovuta kiasi kikubwa cha watanzania kuelekea uchaguzi mkuu.sasa unaposema wanapendelea Kenya una ushahidi gani kama sio lawama zisizo na mashiko?
 
In economic point of view they are absolutely right! Stop being like those mainstrem Chinese officials who created the stock crash by encouraging people to purchase more but now are silence and blemming others!
 
Ya kenya nayo inashuka ukilinganisha na dola na paundi kwa nini hawasemi? Kipindi hiki cha uchaguzi BBC wanatumika na Lowasa kuponda serikali.tunawajua.Washapokea mshiko

Hebu wewe jibu hili swali shilingi yetu imepanda au imeshuka?
wewe ulitaka BBC watumie lugha gani ili kueleza ukweli?
Tatizo ni mahaba mlio nayo kwa CCM,
Mbona mnalialia kwani nyie mmejipangaje?
 
Yaani kila mifano ya ovyo ni Tanzania tu? Katika News report yao usiku huu wanatoa mifano ya sarafu zilizoporomoka na haraka wamekimbilia kutoa mfano wa shilingi ya Tanzania. Ni nini ninyi?

Tumewachoka sana kutudhalilisha kila siku! Kila jambo jema mnakimbilia Kenya. Mnatuudhi sana sana msione tumenyamaza!
wewe hujiulizi twiga alipandaje ndege na urefu wake ule unashangazwa na BBC kusema pesa yetu imeshuka. Nyie kweli mmeleweshwa na mahaba mazito. Hamsikii la muhazini wala shehe msikitini mmenogewa

Mmezoea kudanganywa na kulembwalembwa huku Tembo wanateketea, mnapitisha meno ya tembo kwenye uwanja wa ndege wenu wakifika huko wakisema Tanzania kunani, mnakuja juu.

Yaani Mgombea wenu wa uraisi,raisi na wewe pia mnashangaa kwa nini hospital hazina madawa wakati serikali ni yenu, sasa kati ya CCM na ukawa wapi WAPUMBAVU Na malofa?
Endeleeni kudanganyana tu mtauona mwisho wake
 
Yaani kila mifano ya ovyo ni Tanzania tu? Katika News report yao usiku huu wanatoa mifano ya sarafu zilizoporomoka na haraka wamekimbilia kutoa mfano wa shilingi ya Tanzania. Ni nini ninyi?

Tumewachoka sana kutudhalilisha kila siku! Kila jambo jema mnakimbilia Kenya. Mnatuudhi sana sana msione tumenyamaza!
kwa hiyo hata ukujinyea usifiwe tu .. watu wa aina yako ndiyo wameifikisha Tanzania hapa ilipo
 
BBC wakitangaza Tanzania kwa uhalisia lazima utalia na kusaga meno.Nchi imeoza.
 
Kwani wanadanganya? Tuna jambo lipi jema mpaka watusifie? tubadilike watatusifu lkn sio kwa namna unavyotaka kamwe haitawezekana.
 
Asante k-boko.hata mm wananikera sana.naona kuna upungufu bbc, wako biased sana kwa sababu katika matangazo yao ya ukanda wa maziwa makuu, kiasi kikubwa ni habari za kenya na ni kila siku.hata ukija kwenye coverage ya uchaguzi wetu ni kama hakunakinachoripotiwa.labda kwa sababu watangazaji wao wengi ni wakenya!

Kwa sasa deutsche welle wana coverage nzuri ya habari za maziwa makuu na africa lkn sio bbc swahili.

May b kuna haja ya kuna wa watangazaji wengi zaidi watanzania kwenye vyombo hivi vya kimataifa la sivyo tutapotezwa!

Sasa kama wakenya wanafanya vizuri kwanini wasisifiwe? Tanzania hatuna ya maana ya kujisifia mbele ya wakenya
 
Kweli inaboa,hao wengine vp hawana baya yao yote mazuri?.Mleta mada big up kwa kuliona hilo na kulikemea.Wajinga kila kitu wanaona ni siasa tu.

Ila ukweli utabaki kuwa tzs haina thamani kubwa kama ilivyokuwa miaka 10 iliyopita ukilinganisha na kshs.

Ukweli ni ukweli
 
BBC Swahili wanabakwa na mashetani...... kazi kuipendelea kenya hata katika web yao wameiweka kenya BBC ni vibaraka wa Kenya manina zao....halafu Tulivowajinga tunawapenda hao kina kikeke
 
Hawa jamaa ni mabogas kabisa, mfano hii michezo inayoendelea Beijing kila anayeshinda medali wanasema ni Mkenya as if sisi wabongo tumedanja.

Mimi sasa hivi siangalii kabisa, na kama ni lazima niangalie basi naziba ile B ya mwanzo naweka T, ili isomeke TBC.
 
Washenzi hawa wakenya,bbc swahili wameifanya kijiwe,na kupendelea kenya,wakati mie naona wasikilizaji wengi wapo Tanzania,na baadhi ya watanzania waliopo bbc ni kama mananga,hawana uzalendo,yaani wakenya wasiojua hata kiswahili ndo wanawaburuza kwa kupendelea habari za kenya,kweli mkuu wanakera sana.

Acha kupanic ndugu, walichosema BBC ndiyo hali halisi kama hutaki acha.
 
Wamekuudhi wewe na nani?sie wengine tunaona ni ukweli kutokana na hali halisi ilivyo.
 
Bbc wanatoa taarifa za kweli. Mm naona zinasaidia kuimarisha nchi sema sasa viongozi wetu wabishi,wanaangalia matumbo yao tu
 
Back
Top Bottom